Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Ndugu waandishi wa habari karibuni katika kikao hiki muhimu ambacho ninatarajia kupitia kwenu taarifa hii itaufikia Umma wa watanzania kwa wepesi na kwa haraka (The power of media).
Ndugu zangu
waandishi wa habari, mwaka huu wa 2015 Mkoa wetu wa Mwanza umepata heshima
kubwa ya kuwa mwenyeji wa sherehe za Madhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Kitaifa. Awali Mkoa wa Mwanza ulipewa heshima
hii mwaka 2007, ambapo Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania alikuwa mgeni rasmi na kwa bahati ya pekee Mkoa wa Mwanza unapata
fursa nyingine tena ya kuwa na Mhe. Rais
akiwa anahitimisha kipindi chake cha Uongozi wa miaka kumi. Kwetu sisi wana
Mwanza kwetu sisi hii ni heshma kubwa sana.
Tunategemea
maadhimisho haya kuwa na uzito wa kipekee yakilinganishwa na yale ya mwaka 2007
kwani utakuwa ni wakati mzuri kwa Mkoa wetu kujitathimini hatua tuliyopiga hadi
hivi sasa lakini pia kuagana na Rais wetu.
Ndugu
waandishi wa habari , Kauli mbiu kwa mwaka huu wa 2015 ni “MFANYAKAZI JIANDIKISHE, KURA YAKO INATHAMANI KWA MAENDELEO YETU” Kauli mbiu hii inawakumbusha wafanyakazi kuona
umuhimu wa kura zao katika kufanya maamuzi sahihi wakati wa uchaguzi mkuu wa
mwaka huu hapo baadae, kwani kupitia sanduku la kura mfanyakazi ataweza
kujikomboa kwa kuchagua viongozi watakaoleta tija kwenye utendaji lakini pia
kuboresha maslahi yao. Rai yangu nawaomba wafanyakazi wajitokeze kwa wingi
wakati wa kujiandikisha lakini pia watumie haki yao ya msingi ya kwenda kupiga
kura na kuwachagua viongozi wao kwenye maeneo yao pindi muda utakapofika.
Aidha maadhimisho
haya kwa mwaka 2015, yanaratibiwa na Chama cha Wafanyakazi wa Migodi, Nishati,
na Ujenzi (TAMICO) chini ya usimamizi wa shirikisho la Vyama vya wafanyakazi
nchini TUCTA kwa kushirikiana na Uongozi wa Serikali Mkoa wa Mwanza.
Aidha maadhimisho
haya yataenda sambaba na maonesho ya huduma
zinazotolewa na Wafanyakazi na bidhaa
wanazo zalisha na yatakayofanyika katika viwanja vya Furahisha kwa muda wa siku tano kuanzia tarehe 25,Aprili
hadi 30,Aprili, 2015
Nichukue
wasaa huu, kuwaalika wadau wote wanaohitaji
kufanya maonesho ya shughuli zao kujitokeza na kupata mabanda ya kufanya
maonesho hayo.
Aidha
tunawatangazia wananchi wa Mkoa wa Mwanza , Mikoa jirani na watanzania kwa
ujumla kutenga muda wao kutembelea maonesho hayo kwa lengo la kujifunza,
kujielimisha na kupata huduma zinazotolewa na Serikali, mashirika na makampuni
mbalimbali hapa nchini.
Ndugu
waandishi wa habari, nipende kuwahakikishia wananchi kwamba hadi sasa
maandalizi kwa ajili ya sherehe hizo yanaendelea vizuri. Wadau mbalimbali
watakaoshiriki katika maadhimisho hayo wamepelekewa mialiko na wengine wamesha
thibitisha kushiriki. Tunawaomba hata wale ambao mialiko yetu bado haijawafikia
kama wako tayari wawasiliane nasi kwani nafasi bado zipo.
Sambamba na
hilo tunawasihi waajiri waendelee na zoezi la uteuzi wa wafanyakazi hodari,
ununuzi wa sare kutoka kwenye vyama vyao, lakini pia wawaruhusu wafanyakazi
kushiriki katika maadhimisho hayo, kwani hiyo ni siku yetu yakujitathimini na
kuona hali zetu za utendaji kazi.
Ndugu
waandishi wa habari, katika siku ya
kilele kutakuwa na Matembezi ya mshikamano yatakayo anzia kwenye Ofisi za
wafanyakazi zilizopo karibu viwanja vya Nyamagana kuelekea kwenye viwanja vya CCM-Kirumba mapema saa
2.00 kamili asubuhi na kupokelewa na Mgeni Rasmi.
Nirudie
tena kuwaomba tumieni kalamu zenu kuufikishia umma taarifa hii kwani tunaamini
katika nguvu ya vyombo vya habari mtaweza kuufikia umma kwa haraka na kwa
ukubwa zaidi.
Asanteni
sana.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.
YUSUPH SIMBAULANGA
MWENYEKITI
WA TUCTA MKOA
MWANZA