May 2016
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

WAZIRI WA VIWANDA NA UWEKEZAJI CHARLES MWIJAGE WAKATI WA MKUTANO ULIOANDALIWA NA WAKALA WA VIPIMO NCHINI, HAPA ALIKUWA AKIJIBU BAADHI YA HOJA ZA WAJUMBE WA MKUTANO HUO
MKUU WA WILAYA YA MSOMA, HAMPHREY POLE POLE WAKATI AKICHANGIA JAMBO KWENYE MKUTANO HUO, POLE POLE ALIMWAKILISHA MKUU WA MKOA WA MARA MAGESSA MULONGO.
PICHA YA PAMOJA NA WAZIRI ALIYE KETI WANNE KUTOKA KUSHOTO WALIOKETI AKIWA NA WAKUU WA MIKOA ILIYO HUSIKA KATIKA MKUTANO HUO.
 
Na: Atley Kuni- Mwanza

Waziri wa Viwanda Biashara na uwekezaji Charles Mwijage, amesema hayupo tayari kurudi kwenye makongamano, semina wala warsha ambazo hazina tija kwa manufaa kwa mustakabali wa zao la pamba nchini na badala yake amesema, kuanzia hivi sasa nguvu itaelekezwa kwenye utendaji zaidi ili kuleta matokea chanya kwa zao hilo ambalo lilikuwa mkombozi wa mkulima wa Tanzania katika miaka ya nyuma.