Rais akipokelewa katika uwanja wa Ndege wa Mwanza.
 
 
Na Atley Kuni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, ameanza ziara ya siku tano Mkoani Simiyu kwa ajili ya ziara ya Kiserikali.
 
Hivi leo katika siku yake ya kwanza ameweka jiwe la Msingi katika mradi wa barabar wenye km. za mraba 71 kutoka Ramadi hadi Maswa kwa kiwango cha Lami kwa kutumia fedha za ndani.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kutoka kwenye mamlaka ya Mawasiliano Ikulu, imesema rais akiwa Mkoani Simiyu atazindua, kuweka mawe ya Msingi na kufungua miradi mbali mbali ya Maendeleo inayo tekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Wananchi.
 
Mkoa wa Simiyu unaundwa na Wilaya za Maswa na Bariadi zilizomegwa kutoka  Mkoani Shinyanga pamoja na jimbo la Busega lililokuwa Mkoani Mwanza.
 
Aidha kukamilika kwa barabara hiyo itakuwa ni kichocheo kikubwa cha maendeleo katika ukanda huo na Mkoa huo kwa ujumla, Mkoa ambao huzalisha zao la Pamba kwa wingi.
Axact

Post A Comment: