Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
WAZIRI WA VIWANDA NA UWEKEZAJI CHARLES MWIJAGE WAKATI WA MKUTANO ULIOANDALIWA NA WAKALA WA VIPIMO NCHINI, HAPA ALIKUWA AKIJIBU BAADHI YA HOJA ZA WAJUMBE WA MKUTANO HUO |
MKUU WA WILAYA YA MSOMA, HAMPHREY POLE POLE WAKATI AKICHANGIA JAMBO KWENYE MKUTANO HUO, POLE POLE ALIMWAKILISHA MKUU WA MKOA WA MARA MAGESSA MULONGO. |
PICHA YA PAMOJA NA WAZIRI ALIYE KETI WANNE KUTOKA KUSHOTO WALIOKETI AKIWA NA WAKUU WA MIKOA ILIYO HUSIKA KATIKA MKUTANO HUO. |
Na: Atley Kuni- Mwanza
Waziri
wa Viwanda Biashara na uwekezaji Charles Mwijage, amesema hayupo tayari kurudi
kwenye makongamano, semina wala warsha ambazo hazina tija kwa manufaa kwa
mustakabali wa zao la pamba nchini na badala yake amesema, kuanzia hivi sasa
nguvu itaelekezwa kwenye utendaji zaidi ili kuleta matokea chanya kwa zao hilo
ambalo lilikuwa mkombozi wa mkulima wa Tanzania katika miaka ya nyuma.