Articles by "Afrika"
Showing posts with label Afrika. Show all posts
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
MAKAAZI YA RAIS ZUMA NDIO HAYA.



















Rais Jacob Zuma anatarajiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge la A-Kusini kujieleza kuhusu kashfa ya kufuja pesa za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake ya kifahari.

Ukarabati huo uligharimu dola million 23 na Bw Zuma ameamrishwa na mkaguzi au mlinzi wa mali ya umma nchini humo alipe baadhi ya pesa hizo .

Zuma alisema Jumatatu kuwa sio sawa kwake kutakiwa alipe sehemu ya pesa zilizotumiwa kwa ukarabati wa nyumba yake kwani sio yeye aliayeamuru ukarabati huo.

Alisema kuwa maafisa wa serikali ndio walioagiza ukarabati huo bila ya kumshauri.

Zuma alizungumza kwa mara ya kwanza Jumatatu tangu kashfa hiyo kujulikana akisema kuwa halipi chochote kwani hakuomba ukarabatai kufanywa.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Mshambuliaji wa TP Mazembe, Mbwana Samata.

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samata alifunga bao pekee na kuiongoza TP Mazembe ya DR Congo kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, huku mabingwa watetezi Al Ahly wakiaga mashindano kwa kuchapwa 3-2 nyumbani na Al Ahly Benghazi ya Libya.

Samata aliingia akitokea benchi na kufunga bao hilo dakika ya 68 na kuipa ushindi wa 1-0 dhidi ya Sewe Sport ya Ivory Coast na kusonga mbele kwa sheria ya bao la ugenini baada ya matokeo ya jumla kuwa 2-2 baada ya awali Mazembe kutunguliwa mabao 2-1 jijini Abidjan.

Samata ndiye aliyefunga bao la kufutia machozi Abidjan wiki moja iliyopita pamoja na bao pekee la Jumamosi jijini Lumbumbashi. Sasa Mazembe itasubiri kujua wapinzani wake katika droo itakayopangwa Aprili 29 mjini Cairo.

Nao mabingwa watetezi Al Ahly ya Misri wameaga mashindano hayo baada ya kuchapwa mabao 3-2 nyumbani na Al Ahly Benghazi katika pambano la marudiano lililopigwa mwishoni mwa wiki jijini Alexandria.

Kipigo hicho kinaifanya Al Ahly iondolewe mashindano hayo kwa jumla ya mabao 4-2, baada ya mechi ya kwanza iliyopigwa jijini Tunis, Tunisia ambako Benghazi wanatumia kama uwanja wa nyumbani kutokana na machafuko kushinda 1-0.

Kutoka: Mwananchi.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
  • Robert Mugabe amefikisha miaka 90 hii leo na wikendi hii kutakuwa na sherehe si haba nchini Zimbabwe kusherehekea maisha marefu ya kiongozi huyo.
HONGERA MIAKA 90 UMEFIKA MZEE.
 
Alizaliwa katika kijiji cha Kutama, kusini-magharibi mwa jiji kuu, alisomeshwa na wayesuti, na baadaye akawa mwalimu kabla kujiingiza katika harakati za kupigania uhuru wa Zimbabwe.
Uwanaharakati wake ulimfanya afungwe gerezani kwa miaka 11, na baadaye mwaka 1980 akawa Rais wa kwanza wa Zimbabwe.
Yafuatayo ni mambo tisa ambayo huenda hukuwa unayajua kumhusu kiongozi huyu na ambayo huenda yamemuwezesha kuwa rais kwa muda mrefu mno.

1) Zoezi na vyakula vya kienyeji

Mugabe akionekana kuwa na furaha mno
“Nakuwa mgonjwa wakati sijafanya mazoezi ya viuongo vya mwili,” Bw. Mugabe alisema miaka mitatu iliyopita. Huwa anaamka kati ya saa kumi na kumi na moja alfajiri, na kutoka na jamaa zake wa karibu, huwa anasikiliza BBC idhaa ya dunia mara kwa mara.
Siri nyingine ya kuishi kwake kwa muda mrefu ni kuwa hupenda sana-vyakula vya kienyeji kinacholiwa sana Zimbabwe lakini pia, havuti sigara, ilahunywa pombe kidogo anapokula chakula cha jioni na hasa Wine.

2) 'NI kweli alifufuka?'

Ingawa kumekuwa na uvumi mara nyingi kuwa Mugabe hana afya nzuri, afya yake na kazi yake ya kisiasa inaendelea vema kabisa. “ Nimekufa mara nyingi-hapo ndipo namwelekea Yesu Kristo. Yesu alikufa mara moja, na akafufuka mara moja,” alisema alipotimiza miaka 88.

Ingawa alilielewa kwa familia ya kikatoliki-mamake alikuwa mcha Mungu-alisema alipohojiwa na kituo cha habari cha Afrika Kusini, SABC, miaka michache iliyopita, kuwa si Mkristo anayetumikia dini kwa sana.

3) Je Unajua ni shabiki mkubwa sana wa kriketi?

Kwa muda mrefu amedhihirisha hadharani mapenzi ya mchezo wa kriketi. Ni patroni wa jumuiya ya mchezo wa kriketi wa Zimbabwe, ambapo nyumba yake ipo karibu na uga wa michezo wa Harare, ambapo anaweza kutazama kwa makini kriket wakati wa michezo ya kitaifa.
“Kriketi yafanya watu wawe wangwana, na pia inawafanya watu kuwa wema,” Bw. Mugabe alisema miaka kadhaa baada ya Zimbabwe kujinyakulia uhuru. “Nataka kila mtu acheze kriketi Zimbabwe; nataka nchi ya Zimbabwe iwe nchi ya wangwana.”

4) Hapendi kushindwa

“Alipokuwa kijana, Mugabe alikuwa “mmakinifu na mzuri kabisa” katika mchezo wa tennis,” alisema aliyekuwa mwalimu katika shule ya Wakatoliki aliposomea Mugabe. Ila, aliposhindwa katika mchezo huo, aliitupa raketi yake chini kwa hasira.
Mugabe amekiri kuwa hakuwa mzuri katika mchezo wa kandanda alipokuwa mdogo, ila kwa sasa, anapenda kuutazama mchezo huo. Yeye ni shabiki wa vilabu vya Chelsea na Barcelona vilivyoko Uingereza na Uhispania  “ Ninapotazama kandanda, sitaki usumbufu kutoka kwa mtu yeyote,” alisema mwaka wa 2012. “Hata mke wangu anajua mahala pa kukaa juu wakati wanapofunga bao uwanjani, hata mi pia nafunga bao kwangu kwa kupiga mateke vitu vyovyote vilivyoko mbele yangu.”

5) Kumbe alipata mtoto akiwa miaka 73!

Familia ya Mugabe
Ana watoto watatu na mke wake wa pili, Grace Marufu, aliyekuwa karani wake. Mtoto wao wa tatu alizaliwa 1997, mwaka mmoja baada ya wao kufunga ndoa.
Mwanawe wa kwanza, Nhamodzenyika, alikufa kutokana na Malaria akiwa miaka mitatu bado wakiwa Ghana. Bw. Mugabe hata hivyo hakupata ruhusa ya kwenda Accra kuungana na mkewe kwa mazishi ya mwanawe, kwani alikuwa mfungwa wa serikali ya enzi hiyo ya Rhodesia.

6) Anampenda Cliff Richard kumliko Bob Marley

Mwanasiasa wa Zimbabwe ambaye kwa sasa ni hayati, Edgar Tekere, alimwambia mwandishi wa BBC, Brian Hungwe, kuwa alipokuwa akitayarisha kadhia ya kusherehekea uhuru wa Zimbabwe 1980, Bw. Mugabe hakumtaka muimbaji Bob Marley aalikwe kutumbuiza watu, ila alimtaka muimbaji maarufu wa Uingereza, Cliff Richard. Pia anampenda Muimbaji, Jim Reeves.
Mugabe anawachukia sana wanamitindo wa rasta, na waimbaji wa mitindo ya reggae. Aliwaonya vijana wa Zimbabwe: “ Nchini Jamaica, wana uhuru wa kutumia bhangi, na wanaume huwa wakati wote wamelewa. Hawataki kuenda shule; wanataka tu kuimba, na kuwekea rasata nyweleni. Kama Zimbabwe, tusielekee hapo.”

7) Mvaaji wa nguo maridadi

Anapenda sana suti zinazoutosha mwili wake visawasawa na tai zinazofanana na kitambaa. Jinsi anavyovaa, imewavutia sana wanamitindo nchini Zimbabwe. Ila, mwanamitindo anayemvisha, Khalil Parbhoo anasema: “Bado anavaa kama mabwana wa Uingereza –hivyo ndivyo anavyopenda."

8) Anamtazama Kwame Nkrumah kama kielelezo kwake

Taarifa kuhusu hali ya kiafya ya Mugabe zimekuwa zikigonga vichwa vya habari karibuni
Bw. Mugabe alipata azma ya siasa akiwa Ghana alipokuwa mwalimu; mahali alipokutana na mke wake wa kwanza, Sally Hayfron.
Aliporudi Zimbabwe, aliwaambia wananchi jinsi Ghana ilivyojinyakulia uhuru, na jinsi uhuru ni kitu kizuri. Katika mahojiano mwaka 2003, Mugabe alisema: “Niliwaambia pia kuhusu Kwame Nkrumah jinsi alivyojitolea na kuiiongoza Ghana kupata uhuru;Kwame aliwaambia wa Ghana kuwa Ghana haingekuwa nchi huru bila ya jitihada na kujitolea kwa kila mtu.”

9) Ni mtu mwenye shahada nyingi

 
Kwa jumla, Mugabe ana shahada saba. Digrii yake ya kwanza ni kutoka katika chuo kikuu cha Fort Hare kilichoko Afrika Kusini. Alisomea digrii zake zingine kwa namna ya mtandao-mbili akiwa gerezani-shahada hizo ni za: ualimu, sayansi, sheria na usimamizi au utawala.
Amejikuta akiwa na “shahada katika ujuhula” alipokuwa akivionya vyama vya kutetea haki za wafanyakazi nchini Zimbabwe 1998 kila vilipotishia kugoma.

Habari hii ni kwa msaada wa Idhaa ya Kingereza ya BBC, Imetafsiriwa.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Sudan, waasi wapewa siku 10 kuanza mazungumzo.  

Thabo Mbeki.
   
Thabo Mbeki, mkuu wa kamati ya upatanishi ya Umoja wa Afrika katika mgogoro wa Sudan  
ametangaza kuwa, umoja huo umeipa serikali na waasi wa nchi hiyo muda wa siku 10. Sambamba na kuashiria kusimamia mazungumzo kati ya serikali ya Khartoum na waasi yaliyokuwa yakifanyika kwa lengo la kuhitimisha vita katika eneo la Kordofan na Blue Nile, Umoja wa Afrika umezipa pande mbili hizo hasimu muda wa hadi siku 10 ili kuanza tena mazungumzo hayo. Akielezea sababu za kusimama mazungumzo hayo, Mbeki amesema kuwa mazungumzo hayo yamesimama kutokana na Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Sudan, tawi la kaskazini (SPLM-N) kusisitiza kufikiwa makubaliano kuhusu masuala yote, huku upande wa serikali ukisisitiza kufikiwa tu makubaliano juu ya maeneo ya Kordofan na Blue Nile.
Tangu mwaka 2011 maeneo ya Kordofan kusini na Blue Nile ya kusini mwa Sudan yamekuwa yakishuhudia mapigano kati ya waasi wa harakati ya SPLM kaskazini na serikali ya Khartoum.


 



Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (wa nne kulia) akiwa na  Jenerali wa Magereza Tanzania John Minja (katikati)  wakimsiliza kwa makini Mnadhimu wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mmeta Manyara akijitambulisha. Kamishna Chato  ametembelea Makao Makuu ya Magereza ikiwa kni ziara ya siku sita nchini Tanzania.Wa tatu kulia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza John Yumbe, wa pili kulia ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Tebuho Nyambe na wa kwanza ni Mrakibu Msaidizi wa Magereza James Nkoloma wote kutoka Makao Makuu ya Magereza nchini Zambia.


Kamishna wa Magereza nchini Zambia yuko katika ziara ya siku sita nchini kufuatia mwaliko uliotolewa kwake na Kamishna Jenerali wa Magereza wa Tanzania John Minja mwezi Septemba mwaka, 2013 alipotembelea Magereza nchini Zambia. Ziara ya Kamishna Percy pamoja na maafisa wengine watatu ni kudumisha ushirikiano uliopo kwa muda mrefu baina ya nchi hizi mbili na magereza kwa ujumla. Akiwa nchini Tanzania Kamishna Percy atatembelea baadhi ya Magereza na Vyuo vya Mkoa wa Dare es salaam, Kilimanjaro na Arusha ili kujionea shughuli za urekebishaji wa wafungwa zinavyofanywa kwa vitendo na kuona maeneo ambayo taasisi hizi mbili zinaweza kubadilishana uzoefu.
 
Askari wa Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani (KMKGM) cha Ukonga jijini Dar es salaam wakionesha aina mbalimbali za mzoezi ya kujihami na kuanguka bila kuumia katika kukabiliana na hatari yoyote, mblele ya Kamishna wa Magereza nchini Zambia Percy Chato (hayupo pichani)

Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (mwenye suti) akikagua paredi maalum lililoandaliwa kwa heshima yake katika Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Dar es salaam.
 
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (mwenye suti) akipokea salaam ya heshima kutoka kwa Paredi maalum (halipo pichani) lililoandaliwa maalum kwa jairi yake katika uwanja wa paredi wa Chuo Cha Maafisa wa Magereza Ukonga.Nyuma yake ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Dkt Juma Ali Malewa na mwenye nguo za kijani ni Kaimu Mkuu wa Chuo  Kamishna Msaidizi wa Magereza Erasmus Kundi
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato wa (pili kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa mmoja wa mafundi katika Karakana ya magari ya Magereza iliyoko Ukonga Dar es salaam, wa kwanza kulia ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Dkt Juma Ali Malewa.
: Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (katikati) akifurahia kukaa katika moja ya samani zinazotengenezwa kiwandani Ukonga, kushoto ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza Tanzania, Dkt Juma Ali Malewa na kulia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza wa Zambia John Yumbe.
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato ( wa nne kushoto), akipokea taarifa fupi kutoka kwa mmoja wa maofisa  kiwandani Ukonga. Kamishna Percy alitembelea Kiwanda cha Magereza Ukonga, Dar es salaam kuona shughuliza za urekebishaji wa wafungwa zinavyofanyika.
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato akisaini kitabu cha wageni Kiwandani Ukonga, wa pili kushoto ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Tanzania Dkt Juma Ali Malewa
 Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato ( wa nne kushoto), akipokea taarifa fupi kutoka kwa mmoja wa maofisa  kiwandani Ukonga. Kamishna Percy alitembelea Kiwanda cha Magereza Ukonga, Dar es salaam kuona shughuliza za urekebishaji wa wafungwa zinavyofanyika.

PICHA NA HABARI KNY. YA JESHI LA MAGEREZA KITENGO CHA HABARI.

 

 

 

 

 

 

 

 
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

 

Na: Bosire Boniface, Garissa

Maofisa wa Kenya wamepuuza Ripoti ya Dunia ya hivi karibuni kabisa ya kila mwaka ya shirika la haki za kibinadamu la Human Rights Watch (HRW), ambayo ilitoa tathmini ya ukosoaji uliyo mkali kabisa kuhusu maendeleo na kinga ya haki za binadamu nchini Kenya kwa mwaka uliopita,

Hatua ya taratibu ya mabadiliko ya polisi nchini Kenya, utamaduni wa kutoadhibiwa kwa unyanyasaji unaofanywa na vikosi vya usalama na serikali kushindwa kuwawajibisha wakosoaji wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008 kumebakia kuwa kero kubwa, kwa mujibu wa ripoti hiyo.

Miongoni mwa mambo mengine, ripoti hiyo ilihoji kiwango cha ushirikiano wa serikali na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) katika uhalifu dhidi ya ubinadamu wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Makamu wa Rais William Ruto.

"Serikali ya Rais Uhuru Kenyatta na makamu wake, William Ruto, imekuwa ikitumia ushindi wake mdogo wa kura asilimia 50.7 ikikwepa duru ya pili ya uchaguzi kusambaza rasilimali zote za nchi katika kusimamisha mashtaka yao kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Uhalifu wa Kivita kwa majukumu yao ya uongozi yanayodaiwa katika vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-08," ripoti hiyo inasema.

"Kenya iliapa kuendeleza ushirikiano na ICC, lakini kutoka uchaguzi, serikali mpya imepiga kampeni kubwa katika Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika kufutwa kwa mashtaka yao, kuahirishwa au kupelekwa katika njia za sheria za ndani," inasema.

Katika kujibu, Waziri wa Mambo ya Nje Amina Mohamed aliitaja ripoti ya HRW kuwa "ya kukasirisha na isiyoeleweka".

"Kwamba nchi haishirikiani na ICC siyo kweli kabisa," aliiambia Sabahi. "Mahudhurio ya Makamu wa Rais Ruto katika mahakama wakati anapohitajika ni ushahidi kwamba kuna ushirikiano. Rais Kenyatta hajasema kwamba hatahudhuria kesi yake wakati itakapofikia kusikilizwa mwezi Februari."

Bado mashtaka ya Kenyatta, ambayo yamepangiwa kuanza tarehe 5, Februari, yameairishwa bila kuja siku ya kuendelea baada ya Mwendesha mashtaka mkuu Fatou Bensouda kutaka muda zaidi kukusanya ushahidi na utetezi kuomba kusimamisha mashtaka.

"Kesi za ICC nchini Kenya zimekuwa zikizuiwa na kujitoa kwa mashahidi wa mashtaka, ikituhumiwa kwa sababu ya rushwa na vitisho; walalamikiwa pia wametuhumu kuharibiwa kwa ushahidi au vitisho kwa mashahidi," ripoti hiyo ilisema, ikiongeza kwamba mwendesha mashtaka wa ICC alikiita kiwango cha kuwachezea mashahidi katika kesi kuwa "hakijawahi kutokea".

Kwa kampeni ya Kenya kujitoa katika ICC  na kuziomba nchi nyingine za Umoja wa Afrika kufanya hivyo, Mohamed alisema kulifanyika ndani ya muundo wa sheria za ndani na za kimataifa.

Kenya inafuata taratibu zote zinazofaa katika hatua hiyo "kwa uwazi na sio kwa siri," Mohamed alisema. "Waandishi wa ripoti hiyo wana ajenda ya siri lakini tutaendelea na uhusiano unaojenga na ICC."

Polisi wa Kenya watuhumiwa

Polisi pia ilipuuza matokeo ya ripoti ambayo ilituhumu vikosi vya usalama kwa mauwaji ya bila kushtakiwa, mateso na ukiukaji mwingine wa haki za binadamu.

"Utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu ya Kenya uligundua kwamba polisi waliwaua kinyume cha sheria watu 120 kati ya Mei na Agosti 2013 katika hali ambayo ingeweza kuzuilika, na kwamba polisi haikuripoti mauaji hayo kwa mamlaka ya kiraia inayoisimamia, Mamlaka Huru ya Usimamizi ya Polisi, kwa ajili ya uchunguzi kama inavyotakiwa chini ya sheria," ripoti ilisema.

Ripoti hiyo pia iliitaja polisi kwa "mateso, upoteaji, na mauaji kinyume cha sheria ya wanaotuhumiwa kwa ugaidi na watu wa asili ya Kisomali".

Inspekta Jenerali wa Polisi wa Kenya David Kimaiyo aliiambia Sabahi madai katika ripoti ya Tume ya Haki za Binadamu ilizingatia mwenendo wa vikosi vya usalama miaka mingi iliyopita, ikiongeza kwamba katika miaka ya hivi karibuni, maofisa wa usalama wamekuwa waathirika wa magenge ya wahalifu na makundi ya magaidi ambayo ripoti imekwepa makusudi kutaja.

"Nchi inakabiliwa na vitisho vya vurugu kutoka pande zote," alisema. "Katika matukio kadhaa maofisa usalama imebidi wachukue hatua kwa kujizuia na pale ilipolazimu kutumia nguvu. Baadhi ya wahalifu hawawezi kutendewa kwa upole."

Katika kujibu tuhuma za ripoti ambazo wanaharakati wa chama cha kiraia wako katika shinikizo la kuacha kutetea haki kwa waathirika wa vurugu za baada ya uchaguzi, Kimaiyo alisema kwamba polisi ingeweza kutoa ulinzi kwa Wakenya wote, ikiwa ni pamoja na wanaharakati wa vyama vya kiraia na familia zao.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Idara ya Polisi Johnstone Kavuludi alikiri kwamba mchakato wa marekebisho ya idara ya polisi ulikuwa unachelewa, lakini alisema tahadhari ilikuwa lazima.

"Ni kweli kwamba marekebisho yako nyuma kiasi, lakini sasa tunajipanga na kufanya kazi ya kuharakisha marekebisho," aliiambia Sabahi. "Mchakato unaweza kwenda taratibu, lakini pia tunataka kuendesha uchunguzi wa haki kwa wale wote ambao uadilifu wao na rekodi ya haki za binadam vimetiliwa mashaka”

Uhuru wa vyombo vya habari wahojiwa

Kwa upande wake, Waziri wa Habari Habari, Mawasiliano na Teknolojia Fred Matiang'i alikanusha tuhuma za ripoti hiyo kwamba serikali ilikuwa ikizuia uhuru wa vyombo vya habari kwa kuanzisha  “ zuio kali kuhusu vyombo vya habari na mashirika yasiyo na ingiza  faida Alisema kusudi la serikali lilikuwa sio kuvizuia vyombo vya habari. "Sheria ambazo serikali imeanzisha zinamaanisha kuimarisha utoaji wa ripoti sahihi na kuzuia uovu," aliiambia Sabahi.

"Baadhi ya mashirika ya habari yanapotosha kile ambacho sheria mpya zinaeleza kuulaghai umma, na ninashangazwa na mashirika yenye [hadhi] ya Human Rights Watch yameleta uongo kwamba serikali inajikita katika kuzuia vyombo vya habari," alisema.

Hata hivyo, wawakilishi kutoka katika vyombo vya habari na makundi ya jumuiya za kiraia wameiunga mkono ripoti hiyo ya HRW, wakisema inaonyesha ukweli wa hali nchini Kenya.

Makamu Mwenyekiti wa Editors Guild ya Kenya David Ohito aliiambia Sabahi kwamba idhini ya Kenyatta ya sheria mpya kwa vyombo vya habari inatishia kikamilifu uhuru na uhai wa vyombo vya habari nchini.

"Ripoti ya Human Rights Watch iliandaliwa [kabla] sheria hizi hazijatungwa, lakini serikali imetimiza tishio lake na kusaini sheria na kudhibiti vyombo vya habari kabisa," alisema Ohito, ambaye ni mhariri wa gazeti la The Standard.

Alisema wadau wa vyombo vya habari wamekwenda mahakamani kupinga sheria  Marekebisho ya Habari na mawasiliano ya Kenya ya mwaka 2013 na Sheria ya Baraza la Vyombo vya Habari Kenya. Kama sheria hizi hazitapitiwa tena, vyombo vya habari vitakabiliwa na ukaguzi na adhabu kali kutoka serikalini, alisema.

Mwandishi wa habari za picha na mwanaharakati Boniface Mwangi alisema rekodi ya Kenya kuhusu haki za binadamu, nidhamu ya utawala wa sheria na kupambana na rushwa ni mbaya.

"Kutoadhibiwa kumekuwa ni kawaida. Msukumo wa serikali ya Kenya kuondolewa kwa mashtaka ya uhalifu dhidi ya rais na makamu wake ni picha mbaya kwa wengine, hususan kwa vikosi vya usalama," aliiambia Sabahi.

Rais ana nafasi ya kujisafisha yeye mwenyewe katika mahakama ya sheria na anapaswa kuwadhibiti viongozi wa serikali wanaotoa msukumo dhidi ya kesi ya ICC, alisema Mwangi.

"Kenya iko katika hatari ya kujiunga na nchi ambazo hazina uvumilivu katika uhakiki na uwiano," alisema. "Ndiyo sababu sheria mpya zimeharakishwa kutungwa kuzuia uhuru."

 
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, AU, Nkosazana Dlamini-Zuma, ameelezea kusikitishwa na hali ilivyo Sudan Kusini, kufuatia kuzuka kwa mapigano katika mji mkuu wa nchi hiyo, Juba, siku ya Jumapili.

Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu na kuchapishwa katika gazeti la Sudan Tribune, mwenyekiti huyo amesema ana wasiwasi hasa na hali ya usalama wa wananchi.


Mapigano yalizuka katika mji wa Juba, Jumapili jioni kati ya vikundi vyenye silaha katika kambi ya jeshi na mapigano hayo yaliripotiwa kuendelea Jumanne, huku milioni ya bunduki ikisikika katika maeneo yote ya mji wa Juba mbali na kuhakikishiwa na serikali ya Sudan Kusini kuwa imedhibiti hali hiyo.

Dlamini-Zuma ameitaka serikali ya Sudan Kusini na makundi mengine yanayohusika katika mapigano hayo kujizua na aina yoyote ya kuendelea kwa mgogoro huo.

Pia amezitaka pande zinazohusika na mgogoro huo kutafuta suluhisho la amani kutokana na tofauti zao, "kwa kuheshimu utawala wa sheria, haki za binadamu na uhalali wa kikatiba", akisema AU iko tayari kusaidia kutafuta suluhisho la hali ya sasa.

Wito wa AU umekuja wakati Marekani ikizitaka pande zinazohusika katika mgogoro wa Sudan Kusini kujizuia na ghasia na kutafuta suluhisho la amani.

Mjumbe maalum wa Marekani Donald Booth alitumia mawasiliano ya Twitter siku ya Jumatatu akitaka kuwepo kwa hali ya utulivu, akisema migogoro ya kisiasa lazima imalizike kwa njia ya mazungumzo na sio vurugu.

Rais Salva Kiir amemshutumu naibu wake wa zamani, Riek Machar, kwa kuchochea jaribio la kutaka kuiangusha serikali yake.

Mawaziri kadha wa zamani wamekamatwa, wakihusishwa na jaribio hilo, ambapo mawaziri wengine hawajulikani walipo.

Bwana Kiir ametangaza amri ya kutotembea ovyo usiku katika mji wa Juba, ambapo maeneo mengi yenye pilikapilika za kibiashara, yamekimbiwa kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo, mazingira ya jaribio hilo hayako bayana, huku kukiwa na taarifa zinazokinzana na kauli rasmi ya serikali kuhusu tukio hilo, zikidai kuwa msuguano wa uongozi katika chama tawala, SPLM katika wiki za karibuni ulisambaa hadi katika jeshi, SPLA, na kuchochea mapigano kati ya wafuasi wa Bwana Kiir na Machar.

Jumatatu, walinzi wa rais waliizingira nyumba ya Bwana Machar katika eneo la Amarat, na kuharibu sehemu kubwa ya nyumba hiyo. Hakuwa nyumbani wakati huo na mpaka sasa hajulikani alipo.

Maafisa wa afya wanasema watu wapatao 26 wamethibitika kufariki dunia katika hospitali ya Juba, wakati zaidi ya watu 113 wametibiwa kutokana na majeraha ya risasi.

 
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

.NA  FRANCIS GODWIN -- IRINGA
Tanzania yazibagwa nchi sita barani Afrika katika mashindano ya vyuo  vikuu ya  kuwania tuzo ya heshima   ya sheria  za  vita  yaliyomalizika  hivi karibuni .


Katika  shindano hilo lililofanyika   kati ya Novemba   16-23 mwaka  huu  jijini  Arusha chuo  kikuu  cha Iringa  kiliwakilishwa na  washiriki  watatu  ambao ni Anneny Nahum ,Janeth Nagai   na Joanna Mcintype vijana  hao  waliweza kufanya  vema  kiasi  cha  kuiwezesha nchi ya Tanzania kuibuka mshindi  wa kwanza wa  tuzo hiyo.

Wakizungumza leo chuoni  hapo katika hafla  fupi ya kukabidhi  tuzo hiyo kwa uongozi wa  chuo hicho ,washirikia hao  walisema  kuwa  ushindi  huo  umetokana na ushirikiano  ulioonyeshwa na nidham iliyotukuka miongoni mwao.

Hata  hivyo  walisema  kuwa  tuzo  hiyo  ni  heshima kubwa kwa Tanzania  na ni heshima kwa  chuo  hicho .

mkuu msaidizi wa  kitivo cha  sheria chuo kikuu cha Iringa Jane  Massey alisema  kuwa washiriki hao  wamepata kushinda kutokana na kuonyesha  uwezo wa hali ya  juu katika mashindano hayo na  kuwa  heshima kubwa ambayo  chuo hicho  imepata  ni jambo na kujivunia na kumshukuru Mungu  pia. Alisema  kinachoangaliwa katika mashindano hayo na lengo la tuzo hiyo ni kuenzi amani na kuona hakuna matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu ambayo yanatokea wakati wa vita ,hivyo sheria  hiyo  inapaswa  kuendelea  kutolewa hata kwa Tanzania pia

Kwa  upande wake makamu Mkuu  wa  chuo   kikuu  cha Tumaini Iringa, Prof Nicholaus Bangu alisema  kuwa chuo  hicho  kitaendelea  kufanya  vema si katika mashindano pekee  bali katika mambo mbali mbali yakiwemo ya  kitaalum .

Kwani  alisema  kuwa moja kati  ya mambo  yanayozingatiwa katika  ufundishaji chuoni hapo ni pamoja na kuwafundisha  wanafunzi katika maadili na nidham na ndio mafanikio ya wanafunzi kufanya vema.

Tuzo  hiyo  ambayo  inatolewa kama  njia ya kumuenzi aliyekuwa mwanzilishi wa msalaba mwekundi  ilianzishwa  mwaka 2010 na  kuanza  kushindaniwa  mwaka 2011 ambapo ilichukuliwa na nchi  ya  Ephiopia  ilinyakuwa kwa mara ya kwanza na mwaka 2012 ilichukuliwa na Kenya na  mwaka huu Tanzania i meweza  kuzishinda nchi   hizo sita  ambazo ni South Afrika, Uganda,Kenya, Rwanda, Ethiopia na Zimbabwe

 
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Kufuatia  kuzingirwa na wanamgambo wenye silaha wako kwenye hatari ya kupata maradhi yatokanayo na maji machafu ikiwa hawatapata msaada wa haraka wa kibinadamu, lilionya Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya (KRCS) siku ya Jumanne (tarehe 26 Novemba).

Wanajeshi wakijiandaa kwenda kuwaokoa watu walio zingirwa.
"Hali ya kiafya inaweza ikawa mbaya zaidi kutokana na uwezekano mdogo wa kupata maji, huduma ya matibabu na chakula," alisema meneja wa KRCS kwa eneo la North Rift, Patrick Nyongesa, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya. "Wahanga hao, hasa watoto na wazee wasiojiweza, wana hatari ya kupatwa na homa ya mapafu na maradhi yatokanayo na maji kama vile kipindupindu kwa sababu ya uchafu."

Shirika la KRCS limesambaza msaada wa chakula na mengine iliyochangwa na serikali ya Kaunti ya Turkana kwa familia zilizookolewa.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa huko, Lucas Ngasike, hali ya utulivu imerejea kwenye eneo hilo lakini licha ya kuwepo kwa jeshi, kuna wasiwasi sana.

Aliiambia Sabahi kwamba kulikuwa na hofu kwamba watu wa jamii ya Pokot nchini Uganda walikuwa wanapanga kuivamia jamii ya Turkana na kuwatoa kwenye eneo hilo, na matokeo yake jamii ya Turkana wanajihami kwa silaha.

Lakini msemaji wa polisi ya Kenya, Zipporah Gatiria Mboroki, alisema mzingiro wa kijiji hicho ulimalizika pale wazee wa huko walipoingilia kati na kuwashawishi wanamgambo kujiondoa.

"Utulivu umerejea na barabara imefunguliwa na hakuna mtu aliyejeruhiwa," alisema na kuongeza kwamba polisi bado walikuwa wanaondosha miti iliyowekwa njiani kuzuia kijiji hicho kufikika.

Shirika la KRCS limeitolea wito serikali ya Kenya kuunga mkono suluhisho endelevu kwa mzozo huo kati ya jamii hizo mbili, ikiashiria kwamba mgogoro huo si jambo jipya, kiliripoti kituo cha Capital FM cha Kenya.

 
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeilaumu Uganda kwa kushindwa kufikiwa makubaliano katika mazungumzo kati yake na waasi wa Machi 23.

Lambert   Mende  Msemaji wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
Lambert Mende msemaji wa serikali ya Kongo amesema kuwa Uganda inajifanya kama sehemu ya mgogoro wa Kongo na kwamba hakuna nchi yoyote katika historia iliyosaini makubaliano na kundi lolote lililojitangazia kuvunjika.

 Kwa upande wake Luteni Kanali Paddy Ankunda msemaji wa timu ya usuluhishi ya Uganda ametetea nafasi ya Kampala katika mazungumzo kati ya serikali ya Kinshasa na waasi wa harakati ya M23 na kueleza kuwa Uganda inasalia kuwa mshiriki pekee wa kutumainiwa wa Kongo. Amesema kile kinachoidhuru Kongo kinaiathiri pia Uganda.

 Mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Kinshasa na waasi wa Machi 23 yaliakhirishwa hapo jana baada ya ujumbe wa serikali kutofika mahala palipopangwa kutekelezwa utiaji saini wa makubaliano kati ya pande mbili hizo. Serikali ya Kongo imetangaza kuwa, kunahitajika muda zaidi kwa ajili ya kuweka wazi baadhi ya vipengee vya makubaliano hayo.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
DR. MVUNGI.
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini amefariki dunia.

 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid jana jioni (Jumanne, Novemba 12, 2013), Dkt. Sendongo Mvungi alifariki majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.

 

“Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini amefariki dunia jana (Jumanne, Novemba 12, 2013) saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini,” amesema Bw. Rashid katika taarifa yake fupi ya awali na kuongeza:

 

“Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa leo (Jumatano, Novemba 13, 2013),” aliongeza.

 

Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.

 

Katika taarifa yake, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dkt. Mvungi katika kuomboleza msiba huo.

 
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
By . SABAHI.

At least 100 people are feared dead after a tropical cyclone hit Somalia's north-eastern Puntland region at the weekend, bringing strong winds, heavy rains and flash floods to the coastal towns of Eyl and Bandar Beyla, Dangorayo and Hafun.

"Information collected from coastal areas via irregular telephone contact over the past 48 hours indicates that up to 100 persons might have been killed, while hundreds of other people remain unaccounted for," a statement from Puntland administration said Monday (November 11th).

The cyclone struck the coast Saturday morning and is expected to continue inland through Wednesday, according to weather forecasts.

"Preliminary information also indicates that homes, buildings, boats and entire villages have been destroyed and over 100,000 livestock lost, endangering the livelihoods of tens of thousands of local people," the local administration said.

The storm has left many of the roads to affected areas inaccessible, but the Puntland administration said it is organising relief efforts and has appealed for international help.

 
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.






















Imeelezwa kuwa, Sekta ya Uvuvi ni miongoni mwa sekta zinazo ajiri watu wengi nchini kwani kwa mwaka huajiri watu Laki mbili, hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati akifungua Semina ya wataalamu wa Uvuvi kutoka nchi sita za Burundi, Kenya, Rwanda, Uganda, Senegali na Tanzania ambayo ni Mwenyeji.

 Ndikilo amesema, kwa wastani samaki wapatao tani 360,00 huvuliwa kila mwaka kwa kutumia zana mbali mbali za uvuvi ikiwapo, Nyavu pamoja na utumiaji wa boti.

Amesema katika dunia ya sasa ni yenye changamoto nyingi ni vema kila mara wataalam wakakutana ilikubuni mbinu mpya za uvuvi, kwani katika hata soko la Dunia ushindani ni mkubwa sana kutokana na kukuwa kwa Teknolojia hivyo ni wajibu wa kila nchi kuona inafanya bidii ilikuondoka na adha ya kutegemea mataifa makubwa.

Katika hatua nyingine  Ndikilo amesema, suala la uvuvi wa dagaa nalo limekuwa na shida hasa kipindi cha mvua na kipindi cha kiangazi kikali hasa kwenye Mbaramwezi hivyo ni lazima zipatikane mbinu mbadala katika kukabiliana na hali hiyo " kwenye ziwa Viktoria pekee hupoteza asilimia 10% hadi 20% kutokana na sababu hizo.

Nchi ya Senegali ni nchi mojawapo barani Afrika iliyofanikwa kwa masuala ya uvuvi, kwani  Tanzania mwanzoni mwa miaka ya 1990's ilikopa teknolojia kutoka Taifa hilo la Magharibi mwa bara la Afrika
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Al Bashir na Kiir wajadili kadhia ya Abyei na mipaka



Rais Omar Hassan al Bashir wa Sudan na mwenzake wa Sudan Kusini Salva Kiir wamekutana leo na kufanya mazungumzo mjini Juba katika safari yake ya pili huko Sudan Kusini baada ya nchi hiyo kujitenga.
Pande hizo mbili zimeafikiana juu ya kufunguliwa tena mipaka ya nchi mbili. Vilevile viongozi hao wamejadili suala la kuanzishwa idara ya pamoja ya eneo la Abyei linalogombaniwa ambao limesababisha mapigano ya hapa na pale kati ya majeshi ya Sudan na Sudan Kusini.
Mgogoro wa eneo la Abyei unatishia makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwaka 2005 na kukomesha vita vya ndani vya Sudan vilivyoendelea kwa kipindi cha zaidi ya miongo miwili.
Al Bashir na Kiir pia wamejadili na kuchunguza maamuzi ya Umoja wa Afrika kuhusu mgogoro wa pande hizo mbili na vilevile suala la kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
RENAMO washambulia polisi Msumbiji.
Alphonso wa Msumbiji

Ripoti kutoka Musumbiji zinaarifu kuwa wanaharakati waliojihami kutoka kundi la upinzani la Renamo,wameshambulia kituo kimoja cha polisi katika mji wa kati wa Maringue.
Kisa hicho kinajiri siku moja baada ya Renamo kusema kuwa inajiondoa katika mazungumzo ya amani ya mwaka 1992 yaliosababisha kusitishwa kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Renamo ilikaidi makubaliano hayo baada ya vikosi vya serikali kushambulia kambi iliokuwa na kiongozi wake Afonso Dhlakana na kumlazimu kutoroka.
Hali ya wasiwasi kati ya serikali na Renamo imeongezeka katika siku za hivi karibuni huku mapigano yakiripotiwa katika maeneo mbalimbali.
Inakadiriwa kwamba zaidi ya watu milioni moja waliuawa katika vita hivyo vya miaka 16 vilivyosababisha mazungumzo ya amani huku Renamo ikibadilika kutoka kundi la wanamgambo hadi chama cha kisiasa.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.


Rais Joyce Banda wa Malawi atishiwa kuuawa
  .Ni kutokana na kuwabana Mafisadi


Rais Joyce Banda wa Malawi ametishiwa kuuawa, baada ya kutekeleza mikakati yake ya kufichua na kupambana na ufisadi uliokithiri nchini humo. Brown Mpinganjira, Waziri wa Habari wa Malawi amethibitisha habari hizo na kusema kuwa, mafisadi wameanza kutishia maisha ya kiongozi huyo wa Malawi kutokana na msimamo wake wa kuvunja baraza la mawaziri na kufichua ufisadi mkubwa wa kifedha uliofanywa na viongozi waandamizi nchini humo. Mpinganjira amesema kuwa, baadhi ya vitisho hivyo vimetolewa toka nje ya nchi hiyo na jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi na hatimaye kubaini wahusika wa njama hizo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, tarehe 10 Oktoba mwaka huu, Rais Joyce Banda aliamua kulivunja baraza la mawaziri baada ya kufichuliwa kashfa ya ufisadi wa dola milioni tatu uliofanywa na viongozi wa ngazi za juu wa serikali ya Malawi. Joyce Banda anayehesabiwa kuwa rais wa kwanza mwanamke nchini humo, aliingia madarakani mwaka 2012 baada ya kufariki dunia Bingu wa Mutharika rais wa zamani nchini humo.