Articles by "Maisha. Familia."
Showing posts with label Maisha. Familia.. Show all posts
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
/>
Mkurugenzi wa Miradi kutoka shirika la Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative (AGPAHI) Dk. Safila Telatela akizungumza wakati wa kufungua Ariel Camp (Kambi ya Ariel) ya siku tano kuanzia June 19,2017 - June 23,2017 iliyokutanisha watoto na vijana 50 kutoka mikoa ya Shinyanga,Mwanza na Geita jijini Mwanza.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amezindua Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekouture inayoundwa na wajumbe wapatao 15, huku akiibebesha jukumu lakuhakikisha hospitali hiyo inachana na mfumo wa ukusanyaji mapato wa kawaida na badala yake watumie mfumo wa kieletroniki
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGULI ALIPOKUWA AKITANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI KUSHOTO NI MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU NA KULIA NIA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA.
Magufuli: Kumekuwa na speculation nyingi na watanzania wamekuwa na hamu kubwa ya kujua baraza la mawaziri, baada ya kusubira kwa muda mrefu, baada ya kuapa tulitakiwa angalau tarehe kumi tuwe tumetangaza baraza.

Tuliona angalau tujiridhishe kwanza, baraza lililopita lilikuwa na mawaziri na manaibu zaidi ya 59, tukaona tuwe na baraza dogo. Hatuwezi kukaa bila baraza, katika baraza hili, wizara nyingi tumeziunganisha na kutakuwa na wizara 18 na tutakuwa na mawaziri 19 tu, kuna baadhi ya wizara zitakuwa na mawaziri na hazitakuwa na manaibu waziri.

Lengo ni kutimiza ahadi yetu ya kuwa na baraza dogo kupunguza gharama na effective kwa kufanya kazi. Zilitengwa bilioni 2, mawaziri watakapoteuliwa waende semina elezi, baraza nitakaloliteua halitakuwa na semina elekezi na fedha tutaelekeza sehemu nyingine kama ni madawati au kwenye elimu bure. Watafanya semina elekezi wenyewe ndani kwa ndani.

WIZARA
Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora: Mawaziri ni George Boniface Taguluvala Simbachawene na Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, Naibu waziri Selemani Saidi Jafo.

Ofisi ya makamu wa Rais, muungano na mazingira: Waziri ni January Yusuf Makamba, naibu Luhaga Mpina

Ajira, walemavu: Jenista Joakim Mhagama, Naibu nimemtua mbunge, Abdallah Possi. M ambae ni mhadhiri Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu: Waziri ni Jenista Muhagama, manaibu Anthony Mavunde, Possy Abdallah.

Kilimo, mifugo na uvuvi: Waziri ni Mwigulu Lameck Nchemba, naibu William Ole Nasha

Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano: Waziri bado sijamtafuta, naendelea kumfikiria, Naibu waziri mhandisi Edwin Ngonyani.

Fedha na mipango: Waziri bado tunamtafuta, naibu waziri ni Ashantu Kizachi

Nishati na madini: Waziri ni Professa Sospeter M. Muhongo, Naibu waziri ni Medalled Karemaligo

Katiba na sheria: Waziri Harrison George Mwakyembe

Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa: Waziri ni Augustine Philip Mahiga ambae nimemteua kuwa mbunge na kisha waziri, Naibu ni Dr Suzan Kolimba.

Ulinzi na kujenga taifa: Waziri ni Dr. Hussein Ali Mwinyi

Mambo ya ndani: Charles Muhangwa Kitwanga

Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi: Waziri ni William Vangimembe Lukuvi, Naibu Angelina Mabula

Maliasili na Utalii: Waziri bado, naibu ni Ramo Makala

Viwanda, biashara na uwekezaji: Waziri Charles John Poul Mwijage

Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi: Waziri bado hajapatikana, Naibu ni Stella Manyanya

Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto: Waziri Ummy Ally Mwalimu, Naibu ni Hamisi Andrea Kigwangalla

Habari, utamaduni, wasanii na michezo: Waziri Nape Nnauye, naibu Anastazia Wambura

Wizara ya maji na umwagiliaji: Waziri Makame Mnyaa Mbarawa ambae nilimteua kuwa mbunge, Naibu ni Isack Kamwela

=====================

Swali: Kuna baadhi hukutaja, tatizo ni nini hasa kwa wizara ambazo hujateua? Wabunge wa chama chako hawana sifa? Usimamizi wa baraza unatarajia zitafanya kazi zake Dodoma ukiondoa TAMISEMI?

Magufuli: Nilitegemea ungeniuliza kwanini sikuteua siko niliyoteuliwa, subira yavuta heri, hawa wameanza na wengine watafata. Usiwe na haraka. Kuhusu Dodoma tutatekeleza yaliyoko kwenye ilani ya chama cha mapinduzi.

Swali: Umesema hakutakuwa na semina elekezi, utafanya nini waweze kwenda na kasi ya hapa kazi?

Magufuli: Niliyowachagua wote wana CCM na wengi wao ni wabunge, walinadi ya sera hapa kazi na ndio maana haja ya semina elekezi, spidi ni hiyo hiyo ndio maana hatutatumia semina elekezi ya bilioni mbili.

Manyerere Jackton: Kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri na kwa kulinganisha na tulipotoka, serikali itakuwa imepunguza kiasi gani?

Magufuli: Wewe ndie utapiga hesabu, kwa vile ni mmiliki wa gazeti huwa unapiga hesabu huwa unapata kiasi gani. Utanisaidia katika kupunguza baraza tutakuwa tumesevu kiasi gani na zile tulizosevu za gharama elekezi, kuchelewa kutangaza baraza na wale ambao sijawataja na bahati nzuri nyie waandishi mnaweza kupiga hesabu vizuri. Zipo nchi zina mawaziri wengi mpaka kufikia hata 70, wizara 44, manaibu na mawaziri. Tutakapomaliza tutakuwa na baraza la watu 34 tu.

Wakienda kule mawaziri wakafanye kazi kweli ndio maana sisi tulipochaguliwa tulifanya kazie kweli na hatukwenda kwenye semina elekezi na tulijielekeza, wakajieleze kwenye maeneo yao.

Wasihangaike kufanya sherehe kwa sababu ni kazi ngumu na kama wapo wanaopenda kufanya sherehe wajiandae kufanya sherehe siku wakifukuzwa, contract ni miaka mitano. Wakawafanyie kazi watanzania bila kuwabagua, Baraza hili la wizara 15 tumejiridhisha linaweza kufanya kazi tunayowatarajia kuifanya effectivly. Ngoja tukimaliza uteuzi wote tutajua tumesave kiasi gani ili ziweze kwenda kwa wananchi.

Raymond(Uhai Production): Siku saba zimetimia, wafanyabiashara wamesharesha zile hela?

Magufuli: Swali hilo kamuulize kamshna wa kodi TRA.

SWALI: Kuna wizara ina mawaziri wawili, huko kazi ngumu?

Magufuli: Kafanye utafiti hio wizara imeunganisha wizara ngapi, utapata majibu.

Swali: Katika baraza, kuna mawaziri wa baraza lililopita, ulizangatia nini wakati wa uteuzi?

Magufuli: Umekosea hata kupiga hesabu, Kafanye hesabu vizuri, waliorudi ni saba na sio kumi? Ukipiga utaelewa ni vigezo gani nilivyotumia.

Asanteni sana na ninawashukuru
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
ASKARI JESHI KWENYE SIKU YA MASHUJAA JIJI MWANZA, HAPA WAKILIPUA RISASI HEWANI KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOLEA KWA NCHI YAO KATIKA VITA YA PILI YA DUNIA 1939-1945.
Serikali Mkoani Mwanza Imekeme tabia ya watu wanaohubiri mambo ya ukabila katika karne ya sasa wakati mkoa huo ukiwa kwenye maadhimisho ya siku ya mashujaa yaliyofanyika kwenye mviringo wa makutano ya barabara ya Nyerere, Kenyatta na makongoro jijini Mwanza.
Akihutubia Mamia ya wananchi hao, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magessa Mulongo, amesema ameshangazwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa kuhubiri habari ya ukabila kwenye karne ya sasa hasa kipindi hiki tunacho elekea kwenye uchaguzi mkuu.
MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO
AKITOA HOTUBA FUPI.
”Nimeshangazwa na ndugu zetu wa Chadema, juzi wamekuja hapa eti wamekuja kuwaambia wanamwanza, kuwa Magufuli sio msukuma” alisema Muolongo na kuhoji yaani kweli hiyo ndio meseji mtu aliyo kuja nayo? Amakweli duniani hapa kuna watu wana akili isiyo nzuri alisisitiza Mulongo, na kuuliza hiyo kwa watu wa Mwanza inamaana gani? “ Unapokuja na gari la udini unataka kuwaambia nini, na kusema, Ezekiel Wenje, alichaguliwa na wanamwanza lakini sio msukuma yeye ni Mshashi wa Mara lakini pia Highness alichaguliwa na kuongoza Ilemela lakini yeye ni Mchaga wa Kilimanjaro. Nilazima wakati mwingine na nyie wananchi muwe mnapima watu kwa hoja zao, sio mtu anakuja hapa mkutano mzima yeye ni kutukana tuu na kusema mambo ya hovyo mwanzo hadi mwisho.
BASE KAMANDA CANAL KIVAMBA AKIPOKEA SIME
TAYARI KWA KUWEKA KWENYA MNARA WA MASHUJAA.
Katika hatua nyingine, amekemea tabia ya baadhi ya vijana wanaopita mitaani  mara baada yakumaliza mikutano ya siasa na kuanza kubugudhi watu wenye biashara zao, ”Umemaliza kusikiliza mkutano wa siasa nenda nyumbani kwako  kimya kimya” tabia yakupita mitaani na kuanza kuwakera watu wengine wenye biashara zao sio kitendo kinacho vumilika hata kidogo na niwaombe tu vijana wenzagu, kwamba kwa atakaye thubutu kufanya hivyo tena sinto mvumilia” kwa mara ya kwanza niliwazuia askari kuwachukulia hatua lakini niseme, kwa atakaye kiuka utaratibu huo sinto muonea haya wala aibu eti kwakuwa tu kuchukua hatua utalalamikiwa, haiwezekani mtu yeye avunje sheria halafu aangaliwe na hakuna mtu aliye juu ya sheria aliongeza Mulongo.
Hata hivyo ameviagiza vyombo vya ulizi na usalama kuhakikisha vinasimamia kikamilifu ulinzi na usalama na kuhakikisha kila mchakato unapita salama katika kipindi hiki na maisha mengine yanaendelea kama kawaida.
Awali kabla ya kutoa maonyo hayo, Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza juu ya uzalendo wa mtu mmoja mmoja na umuhimu wa kutunza amani” Ndugu zangu yamkini kama tungempa nafasi mzee wetu Sadalla aeleze kile walichokutana nacho miaka hiyo hangetamani kirudie tena, lakini hata wenyewe mmeshuhudia hiki walichokuwa wakifanya askari wetu hapa na hii ilikuwa ni maonesho tu ,sitaki kusema mengi tuitunze amani kwakuwa hakuna mbadala wa amani, badala ya Amani ni Vita.
MZEE IBRAHIMU SADALA ASKARI MSTAAFU WA KAR
AKIFANYA MAHOJIANO NA AFISA HABARI WA MWANZA.
Naye kwa upande wake Mzee Ibrahimu Saddala aliyepigana vita vya pili vya Dunia(KAR) mwenye umri wa miaka 90 kwa hivi sasa, alisema kila anapokumbuka hali ilivyokuwa hatamani kusikia habari ya vita huku akiwataka watanzania kuilinda amani kama mboni ya jicho. ”Mimi niliingia jeshi wakati ule nikiwa na miaka kumi na tisa na ndio kwanza nilikuwa nimemaliza shule, tukaja tukachukuliwa  na kwenda kujiunga jeshi tukaenda hadi Bama wakati huo tukiongozwa na wazungu” anasema Mzee Saddala na kuongeza kuwa “pamoja na kwamba vita ile iliniwezesha kupata pesa yakununua nyumba kwa shilingi miasaba (700) hapa Mwanza lakini kitu ambacho sitaki kukumbuka ni hali ilivyo kuwa pamoja na umri wangu huu”.
Mzee Saddala mwenye umri wa miaka tisini kwa sasa, ni miongoni mwa  watu  wachache waliosalia kati ya walipigana vita kuu ya pili ya Dunia kati ya Mwaka 1939-1945 na kwa sasa anaishi jijini Mwanza lakini pia ni mwenye nguvu na kuweza kutembea yeye mwenyewe kwa kutumia fimbo ndogo aina ya mkongojo inayo msaidia.
Imeandaliwa na Afisa habari Mwanza zaidi na picha isome kupitia


ASKARI JESHI WAKITOA HESHMA ZAO WAKATI WA MAADHIMISHO HAYO YALIYOFANYIKA LEO.

HAPA ASKARI WA GWARIDE WAKIPOKEA MAELEKEZO KUTOKA KWA MMOJA YA VIONGOZI WAO NAMNA YAKUKABIDHI ZANA HIZO KWA VIONGOZI WATAKAO WEKA KUMBU KUMBU.

HAPA VIONGOZI WA DINI WAKIA WANASIKILIZA KWA MAKINI MAZOEZI YA GWARIDE LA MASHUJAA.


MPIGANAJI WA KAR KITENGO CHA SIGNO, IBRAHIMU SADALLA, AKIWA AMEMALIZA KUWEKA SHOKA KATIKA MNARA WA KUWAENZI MASHUJAA WA VITA YA PILI YA DUNIA.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akimwapisha George Mcheche, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, wakati wa hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo mchana. Picha na OMR


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akisaini nyaraka wakati wa hafla fupi ya kumwapisha, George Mcheche, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kwenye hafla hiyo iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo mchana. Picha na OMR
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akimkabidhi nyaraka za Serikali, George Mcheche, baada ya kumwapisha kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, wakati wa hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo mchana. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa kwanza kutoka kulia) Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Spika wa Bunge la Jamhuri, Anne Makindajaji Mkuu, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othuman, Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Mcheche, aliyeteuliwa, wakiwa katia ukumbi wakisubiri zoezi hilo la kuapishwa. Picha na OMR
Picha ya pamoja ya kumbukumbu na viongozi wa ngazi za juu.
Picha ya pamoja ya kumbukumbu na wakuu wa Ulinzi na usalama.
Picha ya pamoja ya kumbukumbu na wanafamilia wa Bw. George.
Picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya wafanyakazi wenzake.
Picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya wafanyakazi Tume ya Sheria.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyekuwa akisubiri kuapishwa, George Mcheche, akizungumza jambo na viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, wakati wa hafl hiyo.
Baadhi ya viongozi waliohudhuria hafla hiyo.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO






(TAARIFA KWA UMMA)

WITO WA KUWASILISHA MUHTASARI WA MADA (ABSTRACT) KWA AJILI YA KONGAMANO LA KITAIFA LA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LITAKALOFANYIKA MOROGORO 6/03/2015
Tarehe 8 Machi, 2015 Tanzania itaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambayo itaadhimishwa kitaifa mkoa wa Morogoro. Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake mwaka 2015 ni “Usawa kwa Wanawake ni Maendeleo ya Haraka kwa Wote”.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, itaadhimisha siku hiyo kwa kuandaa kongamano la kitaifa litakalofanyika tarehe 6/03/2015 mkoani Morogoro sanjari na wiki ya maonesho ya wadau mbalimbali yatakayozinduliwa tarehe 03/03/2015 na kufikia kilele  chake tarehe 8/03/2015. Lengo kuu la kongamano ni kujenga jukwaa la majadiliano ya kina kuhusu masuala ya maendeleo ya wanawake na usawa wa kijinsia.

 Mada kuu nne zimependekezwa kuwasilishwa katika maeneo yafuatayo:
1.     Ukatili wa kijinsia (intimate partner violence- Ukatili katika mahusiano)
2.     Haki za wanawake/binadamu na mchango wa wanaume katika utetetezi wa haki za wanawake (Kwa mfano, ubakaji, ukatili kwa watoto/ wasichana)
3.     Hali ya Mtoto wa Kike (mf. Ndoa za utotoni)
4.     Ajira salama na haki katika ajira,
5.     Tathimini ya sheria na sera (dawati la jisia na polisi) na
6.     Majadiliano ( panel discussion) kuhusu uwezeshaji wa wanawake kiuchumi.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto inakaribisha mwanajamii yeyote aliyetayari kuandaa mada katika maeneo yaliyotajwa hapo juu, awasilishe muhtasari wa mada yake (ikisiri, abstract) yenye maneno kati ya 300 na 500 kwa ajili ya maandalizi ya kongamano hili muhimu. Siku ya mwisho ya kuwasilisha maelezo hayo (abstract) ni tarehe 20/01/2015.

Waandishi ambao muhtasari wa mada zao utakubaliwa watafahamishwa tarehe 20/01/2015 na watashirikishwa katika maandalizi ya mada kamili tarehe 31/01/2015.

Maelezo ya mada (abstract) yatumwe kwa:

(i)  Elizabeth Makawa: e_palelamakawa@yahoo.com – Simu No. 0655 975478

(ii) Dinah Enock: edinnah@yahoo.com – Simu No. 0766 070376

(iii) Judy Kizenga: kizengajudy@yahoo.com  - Simu No. 0754 564414


Tangazo hili limetolewa na
Anna T. Maembe
Katibu Mkuu
05/01/2015
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kiongozi wa Albino asema hukumu ikishindikana Duniani, itatolewa Mbinguni.
Watu 15 Wanashikiliwa na Polisi, nayo pikipiki iliyotekeleza mpango yabambwa na polisi, uchunguzi unaendelea.

WANANCHI WA NDAMI TARAFA YA MWAMASHIMBA WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA WA MWANZA.
WAANDISHI WA HABARI SHEILA SEZI NA GRACE CHILONGOLA WAKIWA NA MAMA PENDO EMMANUEL, AMBAYE HIVI SASA ANA MAJONZI BAADA YA MTOTO WAKE KUTWALIWA NA WATU HAO.
Serikali mkoani Mwanza imesema hakuna kulala hadi mtoto Pendo Emmanuel  miaka 4(Albino) apatikane, kufatia tukio la kutekwa na watu wasio julikana toka tarehe 27, Desemba, 2014 katika kijiji cha Ndami, Tarafa ya Mwamashimba Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza na kisha kutoweka naye kwenda kusiko julikana hadi sasa.  
ALFREDY KAPOLE MWENYEKITI WA ALBINO MKOA WA MWANZA AKIONGEA KATIKA KIKAO HICHO



SUNGU SUNGU KWENYE KIKAO.
  
MWENYEKITI WA CHAWATA MKOA WA MWANZA NA MWENYEKITI WA ALBINO MKOA WA MWANZA WALIPOKUWA WAKIONGEA NA MAMA YAKE NA PENDO EMMENUEL.

 MKUU WA MKOA.

MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo, alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo na kuwahusisha wananchi wakijiji hicho pamoja na uongozi wa Wilaya na Mkoa huku akitaka kujua hatua iliyofikiwa na wana nchi hao katika kuwabaini walifanya unyama huo.
Mtoto Pendo alitekwa na watu wasiojulikana mnamo usiku wa tarehe 27.12.2014 majira ya saa nne usiku akiwa amelala na wazazi wake huko Nyumbani kwao na kisha watekaji kutoweka naye na kwenda kusiko julikana hadi sasa, huku taarifa za Polisi zikionesha jumla ya watu kumi na watano (15), wakiendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi.
Akihutubia wananchi wa kijiji hicho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, alisema ni tukio la kusikitisha kwani toka mwaka 2007 hakuna tukio la namna hiyo lililo wahi kutokea katika Wilaya hiyo na tukio la mwisho lililotokea lilimkumba mwananchi wa Wilaya hiyo aliyekuwa amesafiri kwenda Mkoani Shinyanga kwa shughuli zake.
Amesema kiburi walicho nacho watekaji hakiwezi kuwa nje ya mipaka ya kijiji hicho cha Ndami bali mpango mzima unajulikana kwa wenyeji na ndio maana ilikuwa rahisi kufanya unyama huo “Kiburi cha watekaji kimo humu humu haiwezekani mtu kutoka mbali aje atekeleze tukio hapa kijijini bila yakuwa na wenyeji lazima kuna mtu au watu walioshirikiana na wahalifu hao”, alisema Mulongo na kuongeza “ kwa mazingira ya Nyumba ya kina Pendo ilipo kule hakuna sehemu yakutokea na kama mliona pikipiki inaranda randa mchana,.. iweje mshindwe kuitilia shaka? Hapana,  hii haikubaliki! mimi nimekuja kuwaambia nataka Pendo apatikane na sio vinginevyo, nawapa siku tano ijumaa nitarudi hapa mniambie Pendo yuko wapi! Alisema mkuu huyo wa Mkoa akionesha kusononeshwa na tukio hilo.
“Mbona mifugo inapo ibwa inapatikana”? Aliwahoji viongozi wa sungu sungu na kusema haiingii akilini kusema wakati wa tukio la utekaji sungu sungu wote walikuwa wamekwenda kula chakula na ndipo kadhia hiyo ilipotokea, mkuu wa mkoa, alihoji kufatia kauli iliyotolewa na kiongozi wa sungu sungu kuwa wakati wa tukio askari wote wa sungu sungu walikuwa wamekwenda kula majira ya saa tatu na tukio kutokea saa nne.
MWENYEKITI WA ALBINO MWANZA.
Awali akielezea kusikitishwa kwake na tukio hilo, Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu wa Ngozi mkoani hapa Alfred Kapole, alisema inasikitisha kuona wanadamu wakiwauwa binadamu wenzao kama vile wanyama bila hata woga na vyombo vya maamuzi vikishindwa kutoa hukumu kwa wakati huku akielekeza lawama zake kwa mahakama na Mkemia Mkuu. “Mh. Mkuu wa mkoa inasikitisha kuona miongoni mwa kesi 72 zilizokuwa mahakamani, ni kesi 3 tu ndizo zilizokwisha kutolewa hukumu” alisema Kapole, na kuongeza ingekuwa ni kesi ya Wabunge wameshindana kwenye masuala ya uchaguzi ingekuwa imekwisha hukumiwa lakini kwakuwa ni mlemavu wa ngozi,   basi kupuuzia kumekuwa kwingi mno. Alisema kapole.
Akinukuu maneno kutoka katika kitabu cha Biblia, Kapole alisema hata kama hukumu zitashindwa kutolewa na wanadamu hapa Duniani, naamini Mungu wa Mbinguni kuna siku haki itatendeka kwa kuwa “Kitabu cha Mika 3.3-7 kinaeleza juu ya hukumu watakayo ipata watu walao nyama za watu bila woga. Kesi zinaendeshwa Polisi wanajitaihidi sana lakini mkemia watendaji wa ofisi ya mkemia mkuu wanatuhujumu kwa kuita nywele zetu albino ni za Midoli, aling’aka Kapole wakati akielezea kusikitishwa na ofisi ya Mkemia mkuu wa serikali pindi inapo pelekewa Nywele.
Mwenyekiti Kapole pia aliomba kwa yeyote aliye na Mtoto huyo kumrejesha na kama wamemdhuru basi warejeshe hata mwili wake ili matanga yaweze kufanyika, akatumia fursa hiyo kumomba Rais wale wote waliohukumiwa kunyongwa wanyongwe ili kuepusha kuendelea kula chakula cha serikali bure.
RC ITIKADI KATIKA KAZI.
Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa aliwataka wanachi kuweka mbali itikadi zao za namna yoyote na kufanya kila linalowezekana  ili kufanikisha zoezi zima la kuwasaka walio husika na utekaji wa mtoto Pendo Emmanuel, ambao unasimuliwa kuleta siamanzi kubwa ndani ya jamii ya wana Kwimba na watanzania  lakini pia kuchafua taswira ya nchi mbele ya mataifa mengine ya Dunia . Huku akiwaonya watu wa haki za binadamu kuacha kupaza sauti za kuwatetea wahalifu. Tanzania inatajwa kuwa kinara cha ukatili huo tangu mauwaji hayo yalipo zuka mwanzoni mwa miaka ya 2006/2007.
TAKWIMU ZA KIMATAIFA.
Kwa Mujibu wa takwimu za kimataifa zinaonesha ni asilimia 2% tu ya watu ambao huzaliwa na ulemavu wa ngozi ndio hufikia na kusherekea miaka 40 ya kuzaliwa kwao, huku pia takwimu zikionesha katika nchi za Afrika mtu mmoja (1) kati ya elfu mbili (2000) huzaliwa wakiwa na ulemavu wa ngozi wakati katika marekani ni mtu mmoja kati ya elfu kumi na saba ndio huishi na ulemavu wa ngozi.
Mauaji ya Albino katika Tanzania yanaonekana kushamiri katika Mikoa ya kanda ya ziwa, ambapo imani za kishirikina zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha mauwaji ya hayo lakini pia yale yalio wahusu vikongwe yanayo husishwa na  masuala ya kujipatia utajiri wa haraka suala ambalo sio la kweli, ambapo takwimu zinaonesha kuwa mauwaji yalianza  siku nyingi japo kuripotiwa katika mamlaka za serikali na vyombo vya habari ilianza  mwaka 2006/2007.
Hivi sasa zipo asasi za kiraia zinazo jihusisha na harakati za kupinga mauwaji hayo ikiwapo asasi ya Under The Same Sun ya Nchini Canada na kwa Tanzania imeshakuwa na tawi toka mwaka 2008.
KAMANDA WA POLISI.
Awali akitoa taarifa ya uchunguzi wa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mulowola alisema tayari watu 15 wanashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoani humo kwa mahojiano zaidi akiwapo baba mzazi wa Pendo, lakini pia jeshi hilo limefanikiwa kuipata piki piki iliyotumika kufanya unyama huo. “Hivi sasa tunawashikilia watu wapatao kumi na watano na wanaendelea kuhojiwa na Polisi” alisema Mlowola na kuongeza kuwa huo sio mwisho kwa kuwa jinai haina mwisho hata miaka ishirini tukio hili litaendelea kuchunguzwa”, na kusema hata kama yeye atahamishwa au kustaafu kijana atakayekuja ataendelea na kesi hiyo, hivyo wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa kile wanacho kifahamu, alisema Mlowola na kusema tayari Jeshi hilo mkoani hapa limetangaza kuto Milioni tatu 3 kwa atakayefanikisha kupatikana kwa mtoto  Pendo.
Mtoto Pendo alikuwa ni miongoni mwa alibino 74 waliopo katika wilaya ya Kwimba na alikuwa namba 9 katika suala la kupatiwa ulizi.
Imeandaliwa na Afisa habari Mwanza- Atley Kuni.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.














Mfuko wa Penshini wa LAPF kwa watumishi wa umma na wasio watumishi wa umma umetoa elimu kwa Waajiriwa waliopo katika Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza huku wakiwataka watumishi kujisikia fahari kujiunga na mfuko huo kwani ndio mfuko pekee nchini wenye kutoa mafao bora na kwa wakati.

Akitoa elimu kwa watumishi hao meneja wa LAPF kutoka makao makuu Abubakar Ndwata amesema kutokana na ubora wao, ndio maana watu wameendelea kuwaamini na katika mwaka wa 2013 walifanikisha kuwaunganisha wateja wapatao elfu kumi na moja(11,000) jambo ambalo wao wanalitaja kama ni mafanikio makubwa kuyafikia ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.

Katika hatua nyingine Ndwata amesema Tanzania ndio nchi pekee yenye sera ya mifuko ya hifadhi ya jamii katika nchi zilizopo Afrika mashariki na kati na hii inatokana na Tanzania kuridhia mikataba mbali mbali kama ule wa ILO  namba 102 sera ya hifadhi ya mifuko ya jamii ya mwaka 2003 pamoja na sheria zilizoanzisha mifuko ya hifadhi ya jamii ikiwapo ile iliyo anzisha LAPF ya mwaka 2006.

Awali akifungua mafunzo hayo Katibu tawala msaidizi wa seksheni ya Utawala na rasilimali watu, Bibi Crescencia Shayo, aliwataka watumishi kuwa huru kujiunga na mfuko wanao utaka bila ya kulazimishwa “ Kwa hivi sasa kwa mujibu wa sera ya mifuko ya hifadhi ya jamii kila mtu anaye ajiriwa anayo hiyari ya kujiunga na mfuko anaoutaka hivyo basi mtumishi awe huru kuchagua mwenyewe na wapi anataka kujiunga na ninyi wenye mifuko kila mmoja abakie kueleza uzuri au ubaya wa mfuko anaotoka” alisema na kuongeza haipendezi kuanza kunyang’anyana wateja kwa njia ambazo sio halali mathalani kutumia rushwa nk.”.

Mfuko wa LAPF ulioanza mwaka 1944 chini ya iliyokuwa serikali ya Kikoloni ya Tanganyika ilikuwa kwa ajili ya wafanyakazi wa chini maakida na makarani kwa lengo la kuwawezesha kujiwekea akiba ulibadilishwa na kuwa mfuko wa hifadhi ya jamii kwa sheria namba 9 ya 2006 kufuatia mabadiliko ya kanuni ya kukokotoa mafao ya uzeeni sawa na yale yanayotolewa kwa wafanyakazi wa Serikali kuu.