Ikiwa leoni tarehe 21 Mei 2017, wananchi katika mkoa wa Mwanza wakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, wameendele kuwalilia na kuwakumbuka watu waliozama na Meli Mv. Bukoba, huku simanzi na majonzi vikishindwa kufutika katika fikra na mawazo ya  watanzania.

Eneo la Makaburi ya Mv. Bukoba Jijini Mwanza katika Wilaya Nyamagana eneo la Igoma


Akizungumza katika kumbukumbu hiyo, Mkuu wa mkoa wa Mwanza, amewataka watanzania kila mmoja kwa imani yake kuendelea kuwaombea marehemu wote waliotangulia mbele ya haki huku akiwataka wamili wa vyombo vya usafiri wa majini kuwa makini na kuhakikisha vyombo vyao vinakaguliwa kabla yakuanza safari.

“Napenda kuchukua fursa hii pia kutoa wito kwa wasafirishaji na wasafiri kuzingatia usalama ili kukabiliana na ajali zinazoweza kuzuilika”, amesema Mongella  na kuongeza kuwa  kusaidia kutoa taarifa katika vyombo husika pale mnapoona kuna dalili za uzembe wa kutozingatia usalama ili hatua zichukuliwa mapema kabla ya ajali kutokea”.

Aidha, amewaomba wananchi  wasikubali kupanda vyombo vya usafiri vilivyojaa kupita kiasi na vile vyombo visivyo imara.      

amewataka wananchi wote kushirikiana na Serikali katika kuhifadhi kumbukumbu hizi muhimu kwa ajili ya ndugu waliotangulia mbele ya haki.

Kumbukumbu hiyo ilifanyika katika eneo la Makaburi ya Mv. Bukoba Eneo la Igoma Mwanza na kuhudhuriwa na wananchi pamoja na Viongozi wa dini na serikali waliokusanyika kwaajili yakuwaombea marehemu hao, kwa sala na Duwa zilizo ongozwa na viongozi wa dini.

Mmoja ya Manusura wa ajali hiyo Charles Limbu,  amesema, suala la elimu wakati wa kusafiri ni muhimu sana kwani mbali yakutokujua kwake kuogelea lakini, alimu aliyoipata wakati wa kuanza safari katika bandari ya Kemondo mkoani kagera ndiyo ilikuwa pona pona yake. “Mimi nilipoona chombo kinazidi kupoteza muelekeo niliamua kukimbilia kuchukua boya na ndilo lililo nisaidia” alisema Limbu.

Mv. Bukoba ilizama 21 Mei, 1996 na kuuwa watanzania kwa mamia waliokuwa wakisafiri kwa meli hiyo kutokea mkoani Kagera kuelekea Mwanza na kisha kuzama umbali mfupi kabla yakutia nanga katika Bandari ya Mwanza.

 
Axact

Post A Comment: