Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akioneshwa kufurahishwa jambo na Wajumbe wa TFDA.
 
Wajumbe wa Bodi ya TFDA walipotembelea Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
Mkuu wa Mkoa amewomba TFDA kuona umhimu wa kujenga kiwanda cha dawa katika Mkoa wa mwanza kutokana na ukuwaji wa Mkoa huo, na ambao unachangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza uchumi wa nchi.
Ndikilo aliyasema alipo tembelewa na wajumbe wa Bodi ya mamlaka ya chakula na dawa nchini wakati walipofika kwa ajili ya uona mchango wa Mkoa wa Mwanza katika jitihada za pamoja za masuala ya TFDA.
"kujengwa kwa kituo cha Biashara cha Jiji la mwanza ambapo milango ya biashara nyingi itakuwa wazi hususan bidhaa zinazodhibitiwa na TFDA".
"kwakuwa mamlaka ya chakula na dawa ndiyo yenye dhamana ya kuangalia afya ya mlaji, hivyo ni vema wakawashawishi  wafanya biashara wakubwa kuona umuhimu wa kujenga viwanda vya dawa katika mkoa huo".
Bodi ya  Ushauri ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kupitia kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MAB) ilikutana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Injinia Evalist Ndikilo kwa lengo la kutambua mchango wa mkoa na ushirikiano unaotolewa kwa TFDA katika masuala ya Udhibiti wa Bidhaa za Chakula, Dawa, Vipodozi  na Vifaa tiba.

Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekiti wa MAB, Balozi Dkt. Ben Moses, amepongeza ushirikiano uliopo baina ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na TFDA kanda ya Ziwa na kutoa wito wa kudumisha ushirikiano uliopo kwa  kuwa lengo la udhibiti litafanikiwa ikiwa ushirikiano uliopo utadumishwa.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amesifu kazi kubwa inayofanywa na TFDA katika kulinda afya ya wananchi kwani afya za wananchi zikiimarika basi uchumi wa unchi nao utaimarika. Vilevile,  katika kueleza changamoto ambazo mkoa unakabiliana nazo katika masuala ya udhibiti wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba,  Injinia Ndikilo alieleza kuwa  usafi katika machinjio ni changamoto kubwa na kwamba anatarajia kulipatia ufumbuzi hivi karibuni baada ya kuitisha kikao cha wadau wa Machinjio ya Mkoa huo wa Mwanza.

Axact

Post A Comment: