July 2015
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
ASKARI JESHI KWENYE SIKU YA MASHUJAA JIJI MWANZA, HAPA WAKILIPUA RISASI HEWANI KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOLEA KWA NCHI YAO KATIKA VITA YA PILI YA DUNIA 1939-1945.
Serikali Mkoani Mwanza Imekeme tabia ya watu wanaohubiri mambo ya ukabila katika karne ya sasa wakati mkoa huo ukiwa kwenye maadhimisho ya siku ya mashujaa yaliyofanyika kwenye mviringo wa makutano ya barabara ya Nyerere, Kenyatta na makongoro jijini Mwanza.
Akihutubia Mamia ya wananchi hao, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magessa Mulongo, amesema ameshangazwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa kuhubiri habari ya ukabila kwenye karne ya sasa hasa kipindi hiki tunacho elekea kwenye uchaguzi mkuu.
MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO
AKITOA HOTUBA FUPI.
”Nimeshangazwa na ndugu zetu wa Chadema, juzi wamekuja hapa eti wamekuja kuwaambia wanamwanza, kuwa Magufuli sio msukuma” alisema Muolongo na kuhoji yaani kweli hiyo ndio meseji mtu aliyo kuja nayo? Amakweli duniani hapa kuna watu wana akili isiyo nzuri alisisitiza Mulongo, na kuuliza hiyo kwa watu wa Mwanza inamaana gani? “ Unapokuja na gari la udini unataka kuwaambia nini, na kusema, Ezekiel Wenje, alichaguliwa na wanamwanza lakini sio msukuma yeye ni Mshashi wa Mara lakini pia Highness alichaguliwa na kuongoza Ilemela lakini yeye ni Mchaga wa Kilimanjaro. Nilazima wakati mwingine na nyie wananchi muwe mnapima watu kwa hoja zao, sio mtu anakuja hapa mkutano mzima yeye ni kutukana tuu na kusema mambo ya hovyo mwanzo hadi mwisho.
BASE KAMANDA CANAL KIVAMBA AKIPOKEA SIME
TAYARI KWA KUWEKA KWENYA MNARA WA MASHUJAA.
Katika hatua nyingine, amekemea tabia ya baadhi ya vijana wanaopita mitaani  mara baada yakumaliza mikutano ya siasa na kuanza kubugudhi watu wenye biashara zao, ”Umemaliza kusikiliza mkutano wa siasa nenda nyumbani kwako  kimya kimya” tabia yakupita mitaani na kuanza kuwakera watu wengine wenye biashara zao sio kitendo kinacho vumilika hata kidogo na niwaombe tu vijana wenzagu, kwamba kwa atakaye thubutu kufanya hivyo tena sinto mvumilia” kwa mara ya kwanza niliwazuia askari kuwachukulia hatua lakini niseme, kwa atakaye kiuka utaratibu huo sinto muonea haya wala aibu eti kwakuwa tu kuchukua hatua utalalamikiwa, haiwezekani mtu yeye avunje sheria halafu aangaliwe na hakuna mtu aliye juu ya sheria aliongeza Mulongo.
Hata hivyo ameviagiza vyombo vya ulizi na usalama kuhakikisha vinasimamia kikamilifu ulinzi na usalama na kuhakikisha kila mchakato unapita salama katika kipindi hiki na maisha mengine yanaendelea kama kawaida.
Awali kabla ya kutoa maonyo hayo, Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza juu ya uzalendo wa mtu mmoja mmoja na umuhimu wa kutunza amani” Ndugu zangu yamkini kama tungempa nafasi mzee wetu Sadalla aeleze kile walichokutana nacho miaka hiyo hangetamani kirudie tena, lakini hata wenyewe mmeshuhudia hiki walichokuwa wakifanya askari wetu hapa na hii ilikuwa ni maonesho tu ,sitaki kusema mengi tuitunze amani kwakuwa hakuna mbadala wa amani, badala ya Amani ni Vita.
MZEE IBRAHIMU SADALA ASKARI MSTAAFU WA KAR
AKIFANYA MAHOJIANO NA AFISA HABARI WA MWANZA.
Naye kwa upande wake Mzee Ibrahimu Saddala aliyepigana vita vya pili vya Dunia(KAR) mwenye umri wa miaka 90 kwa hivi sasa, alisema kila anapokumbuka hali ilivyokuwa hatamani kusikia habari ya vita huku akiwataka watanzania kuilinda amani kama mboni ya jicho. ”Mimi niliingia jeshi wakati ule nikiwa na miaka kumi na tisa na ndio kwanza nilikuwa nimemaliza shule, tukaja tukachukuliwa  na kwenda kujiunga jeshi tukaenda hadi Bama wakati huo tukiongozwa na wazungu” anasema Mzee Saddala na kuongeza kuwa “pamoja na kwamba vita ile iliniwezesha kupata pesa yakununua nyumba kwa shilingi miasaba (700) hapa Mwanza lakini kitu ambacho sitaki kukumbuka ni hali ilivyo kuwa pamoja na umri wangu huu”.
Mzee Saddala mwenye umri wa miaka tisini kwa sasa, ni miongoni mwa  watu  wachache waliosalia kati ya walipigana vita kuu ya pili ya Dunia kati ya Mwaka 1939-1945 na kwa sasa anaishi jijini Mwanza lakini pia ni mwenye nguvu na kuweza kutembea yeye mwenyewe kwa kutumia fimbo ndogo aina ya mkongojo inayo msaidia.
Imeandaliwa na Afisa habari Mwanza zaidi na picha isome kupitia


ASKARI JESHI WAKITOA HESHMA ZAO WAKATI WA MAADHIMISHO HAYO YALIYOFANYIKA LEO.

HAPA ASKARI WA GWARIDE WAKIPOKEA MAELEKEZO KUTOKA KWA MMOJA YA VIONGOZI WAO NAMNA YAKUKABIDHI ZANA HIZO KWA VIONGOZI WATAKAO WEKA KUMBU KUMBU.

HAPA VIONGOZI WA DINI WAKIA WANASIKILIZA KWA MAKINI MAZOEZI YA GWARIDE LA MASHUJAA.


MPIGANAJI WA KAR KITENGO CHA SIGNO, IBRAHIMU SADALLA, AKIWA AMEMALIZA KUWEKA SHOKA KATIKA MNARA WA KUWAENZI MASHUJAA WA VITA YA PILI YA DUNIA.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo akiongea na waandishi wa habari juu ya kulaani vitendo vya  mauwaji kwa kujichukulia sharia mikononi kwa baadhi ya watu.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari.


Hapa Mkuu wa Mkoa alikuwa akikemea juu ya tabia ya waandishi wa habari kununuliwa na nakuanza kuandika watu vibaya.


Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, pichani ni Mwandishi wa Mtanzania Benjamini Masese wakwaza kushoto.

Na: Afisa habari- Mwanza.

Serikali mkoani Mwanza imelaani mauwaji yaliyofanywa na mfanyabiashara maarufu jijini humo Jumanne Mahende(J4) hivi karibuni katika eneo la Nyakato Sokoni katika Wilaya ya Ilemela mkoani humo.

Tamko hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake mapema hivi leo, akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari, Mkuu wa mkoa wa Mwanza  amesema sio kitendo kinacho kubalika wala kuhalalishwa na mtu yeyote mwenye roho ya binadamu.

Mulongo amesema, hata wavumilia wala kuwachekea watu wanao thubutu kutoa uhai wa mtu kwa kisingizio cha madeni, “nataka wananchi wafahamu hakuna mbadala wa uhai wa mtu, kama Serikali ya mkoa, wataiomba mahakama iweze kutenda haki pale ambapo ushahidi utakapojitosheleza ili haki ipatikane.

Aidha, amesema hakuna mtu aliye juu ya sheria na kuamua kutoa uhai wa mtu mwingine. ”Ndugu zangu nataka kila mmoja wetu afahamu hakuna mbadala wa maisha au uhai wa mtu, haiwezekani mtu afanye mauwaji halafu aachwe aendelee kutamba kwa kusema yupo karibu na vyombo vya usalama, mimi kama mkuu wa mkoa nataka umma ufahamu kuwa tunataka kuongoza watu kwa amani na utulivu na ikitokea mmoja hataki kufuata utaratibu lazima sheria ifuate mkondo wake.
Waandishi wa wakimsikiliza Mulongo.

Alisema  “ kuondoa haki ya mtu kuishi na kufanya wategemezi wa familia kuwa wategemezi kwa watu wengine kitu ambacho kina dumaza uchumi wa mtu mmoja mmoja, jamii lakini uchumi wa mkoa na nchi kwa ujumla.

Wakati huohuo ameiomba jamii ya wanamwanza kutoa ushirikiano wa dhati kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pindi wanapo ona kuna viashiria vya uvunjifu wa amani huku akiahidi kusimama kidete na kuona haki inatendeka kikamilifu.

Mbali ya kutoa karipio hilo, mkuu huyo wa mkoa ametumia wasaa huo kutoa taarifa ya uandikishaji wapigakura kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa BVR katika mkoa huo na kusema mkoa umevuka lengo kwa kufikisha asilimia 103, ambayo ni mafanikio makubwa kutokana na malengo waliyo jiwekea hapo awali.

Alisema  hapo awali mkoa ulijiwekea malengo ya kuandikisha watu 1,403,743 lakini kutokana na maandalizi na mipango mizuri ya mkoa wamefanikiwa kuandikisha watu 1,442,391 sawa na asilimia 103.

Akitoa mchanganuo huo kwa kila jimbo alisema Jimbo la Nyamagana wameandikisha watu (273,636). Ilemela (234,879), na Sengerema (153,054), majimbo mengine ni Buchosa (158,510), Misungwi (149,535), Magu (147,155),Kwimba (86,273), Sumve (76,466) na Ukerewe (162,883).

Mkoa wa Mwanza kwa mujibu wa Sensa ya watu wa makaazi ya Mwaka 2012 ulikuwa na watu wapatao Mil.2.7.

Mwisho.