June 2014
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Kama nisingekuwa Mwanahabari nisingepata cha kuandika siku ya leo, au kama ndoto zangu hizi nilizo ziamini toka nasoma shule ya msingi Pale Mkalama Mkoani kilimnjaro katika Wilaya ya Hai leo hii ningepata shida sana kuandika chochote.
Nkwabi Ng'wanakilala Umeondoka wakati nchi yetu na Taifa kwa ujumla sisi tulipitia chini ya darasa lako tulitamani sana tuendelee kuchota hekima Busara na maarifa Chanya Ulokuwa nayo, Mzee ambaye hukuwa kukasirika hata siku moja na hata kama ulikasirika ilikubidi uwe mtu makini sana kuitambua hasira ya Mzee huyu.
Nikiwa pale Chuoni siku moja mtu mmoja aliniuliza hivi nina nani aliyekuvutia hata kukufanya leo hii kuwepo ndani ya darasa la habri jibu lililotoka hakika bila unafiki, nilimjibu ni Ngw'anakilala, akaniuliza tena kwa nini huyo, nikamwambia ni mtu aliyesukuma ndoto zangu nilimfahamu toka nikiwa kinda yeye na Charles Hilari wakati huo wakiwa RTD.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inawatangazia Watanzania  wenye sifa na uwezo kujaza jumla ya nafasi wazi za kazi 1,324 ambazo ni  kwa ajili ya waajiri mbalimbali Nchini.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Xavier Daudi amesema kuwa nafasi 1,334 zimeainishwa bayana kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ambayo ni www.ajira.go.tz  ili kuwawezesha wahitimu wote wenye sifa na uwezo kutuma maombi kwa ajili ya kujaza nafasi hizo ajira Serikalini.
"Nadhani ni vizuri zaidi kwa kila muhitimu anayetafuta kazi serikalini kufungua tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kuangalia nafasi za kazi zilizotangazwa na pale anapoiona kazi inayoendana na sifa alizonazo kutuma maombi yake ili kuweza kushindanishwa na wengine....maana ajira za Serikali hivi sasa ni za ushindani hivyo inampasa kila anayetaka kupata kazi serikalini kujiandaa vyema ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuajiriwa katika Utumishi wa Umma" alisema Daudi.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
It said to be the Smallest  National Park in Tanzania, but is the place were you can enjoy most rather than any tourism place when your in Mwanza Region. though Mwanza it has number of tourism attraction but Saanane it remain to be the number one.

Our Correspondent, hire he come with some Photos which was taken during the visits of  Lake zone Regionals Police Commander's after three days of Seminar which was arranged by Tanzania National Park Authorities (TANAPA).   















Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Li Yuanchao, wakati alipowasili Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo juni 23, 2014 akiongozana na Ujumbe wake kwa ajili ya mazungumzo.  Li Yuanchao, yupo nchini kwa ziara ya siku sita. Picha na OMR
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Li Yuanchao, wakati alipowasili Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 23, 2014 akiongozana na Ujumbe wake kwa ajili ya mazungumzo.  Li Yuanchao, yupo nchini kwa ziara ya siku sita.  Wa pili (Kulia) ni Balozi wa Tanzania, nchini China, Luteni General Abraham Shimbo. Picha na OMR
 

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika mazungumzo na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Li Yuanchao, wakati alipowasili Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo June 23, 2014. Li Yuanchao, yupo nchini kwa ziara ya siku sita. Picha na OMR
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa pili kulia) na baadhi ya Mawaziri wake, akiwa katika mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Li Yuanchao, aliyeongozana na ujumbe wake  wakati alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 23, 2014 kwa ajili ya mazungumzo.  Li Yuanchao, yupo nchini kwa ziara ya siku sita. Picha na OMR
 

Baadhi ya Mawaziri waliofika katika mazungumzo hayo Ikulu jijini Dar es Salaam, na baadhi kusaini mikataba na watu wa China.
 

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara (kulia) akisainiana mkataba na Naibu Waziri wa Wizara ya Biashara ya Wau wa China, Li Jinzao, wa Makabidhiano ya gari la matangazo la Shirika la Utangazaji la TBC, yaliyofanyika mapema mwaka huu. Shughuli hiyo ya kutiliana saini imefanyika leo Juni 23, 2014, Ikulu jijini Dar es Salaam, ikishuhudiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Li Yuanchao. Picha na OMR
 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dorothy Mwanyika, (kulia) akisainiana mikataba miwili na Naibu Waziri wa Wizara ya Biashara ya Wau wa China, Li Jinzao, ya makubaliano ya ushirikiano wa Kitaalamu utakaoiwezesha China kuwapa mafunzo Wanariadha wa Tanzania nchini China na wa makubaliano ya awamu ya tatu ya Ushirikiano wa kiufundi baada ya China kusaidia na kukamilisha Ujenzi wa Uwanja wa Taifa. Shughuli hiyo ya kutiliana saini imefanyika leo Juni 23, 2014, Ikulu jijini Dar es Salaam, ikishuhudiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Li Yuanchao. Picha na OMR

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
PICHA HII INA MAELEZO UKIWEZA KUANGALIA KWA JICHO LA TATU.

Lile sataka la kubaka linalomkabili mume wa mwanamuziki maafuru wa nyimbo za dini – Flora Mbasha limechukua sura mpya baada ya hapo jana mwigizaji na mwongozaji maarufu wa filamu nchini William Mtitu (Pichani) kuamua kufunguka haya juu ya mwanamziki huyu.
Hatutaki kukupotezea muda, jisomee mwenyewe hapo chini kIsha “utafakari”.

Huku akiwa ameweka picha hiyo hapo juu ya Flora Mbasha na mumewe Mtitu alinzanza kwa kuandika…

“Ukiiangalia vizuli hii picha utagundua kitu katika macho ya frola mbasha kuna kitu nakiona kinejificha lakini sasa hivi kimeshajitokeza tayali.....hicho kitu ndicho kilichompeleka jera mbasha na asipokuwa makini anaweza asiwe uraiani tena kama ulivyowatokea familia ya nguza .namaanisha mzee nguza na papii kocha wako wapi? Kiukweli frola una roho mbaya ya mwisho kabisa ilichanganyika na ukatili wa mwisho kabisa kiasi kwamba nashindwa kuelewa umeokoka nn ww ? Eti umemrudia YESU ?YESU yupi huyu nnaemwabudu mm au una YESU wako ww na HUYO GWAJIMA wako? Leo umemsahau Mbasha ww ? Wakati alikuokata umechakaa wakati mbasha dereva teksi leo wataka kumfunga ili iwe nn sasa mbasha akifungwa utapata faida gani ww? Huyo mtoto akija kukuuliza baba yuko wapi utamwambiaje? Fine unaweza kujikaza ukamwambia yuko jela je akikuuliza nani alimshitaki utajibu nn ? Pia waweza kujikaza ukawataja hao wasichana mliowapandikiza je akiuliza ww ulifanya jitihada gani baba asifungwe utasemaje? Hapo auna jibu Acha roho mbaya NENDA KAMTOE MARA MOJA NA MWENDE NYUMBANI MKAONGEE KAMA FAMILIA TWAJUA UWEZO HUO UNAO ILI NA YEYE ATAFUTE HAMSINI ZAKE KAMA WW ULIVYOAMUA KUJISALIMISHA KWA GWAJIMA. USIJE UKASHANGAA WATU WAKASUSIA KAZI ZAKO ZOTE. GDAY.”
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kulia Naibu Waziri wa Tamisemi Kasimu Majaliwa akitoa taarifa ya kuteuliwa kwa wanafunzi wa kidato cha tano kushoto ni Benard Makali Mkurugenzi anayeshuhulikia Elimu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi.
 
 Jumla ya wanafunzi wapatao 235,227 wa kidato cha nne mwaka 2013 sawa na asilimia 58.21 ya watahiniwa wote wamefaulu kujiunga na kidato cha tano pamoja na vyuo mbalimbali vya serikali, matokeo hayo yanaonesha kiwango cha ufaulu kimepanda kwa asilimia 15.13.
Naibu Waziri wa Tamisemi Kasim Majaliwa alisema kuwa, takwimu zinaonesha kuwa kumekuwa na ongezeko la ufaulu kwa wahitimu wa kijitegemea kutoka 26,193 sawa na asilimia 43.07 mwaka 2012 hadi kufikia watahiniwa 34,075 sawa na asilimia 66.21 kwa mwaka 2013 kwa kulinganisha na mwaka 2012 lipo ongezeko la asilimia 30.09.
Majaliwa alifafanua kuwa ufaulu kwa mwaka 2013 katika daraja kwanza hadi la tatu umefikia watahiniwa 71,527 sawa na asilimia 20.28 ya watahiniwa waliofanya mtihani Tanzania Bara, hivyo kuna ongezeko la ufaulu wa asilimia 106.73 ikilinganishwa na matokeo ya ufaulu mwaka 2012.
Uteuzi huo wa ufaulu wa wanafunzi wa kujiunga kidato cha tano umefanyika kwa kutumia kompyuta kwa kuzingatia machaguo ya wanafunzi pamoja na ufaulu, hivyo hapatakuwa na mabadiliko, pia wanafunzi wote wametakiwa kuripoti shuleni tarehe 10 Juni mwaka huu.
Wanafunzi ambao watashindwa kuripoti shuleni hadi tarehe 30 Juni mwaka huu nafasi zao zitajazwa na wanafunzi ambao wamekosa nafasi.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

 


RAIS WA KENYA UHURU MWIGAE KINYATTA
Mauaji ya Mpeketoni yemesababisha vifo vya watu zaidi ya hamsini
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa mauaji yaliyofanywa katika mji wa Mpeketoni, Pwani ya Kenya hayakufanywa na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab.
Kauli ya Rais Kenyatta inakuja kupitia kwa televisheni siku moja baada ya kundi hilo kukiri kufanya mauaji yaliyotokea Mpeketoni Jumapili usiku.
Kenyatta emesema kuwa kuna ushahidi kuonyesha kuwa shambulizi hilo lilipangwa vyema na kwamba wanasiasa walihusika nao.
Al Shabaab lilikiri katika taarifa kwa vyombo vya habari kuwa ndilo lilifanya mauaji hayo Jumatatu jioni.
Alisema kuwa ujasusi ulitolewa kuwa mashambulizi hayo yangefanyika lakini hawakuchukua hatua zozote kuzuia mashambulizi hayo.
Rais amesema kuwa maafisa waliohusika tayari wameachishwa kazi na kwamba watashitakiwa. Amesema kuwa kwa sasa wanachunguza wanasiasa waliohusika na mauaji hayo ili sharia iweze kuchukua mkondo wake.
Mauaji zaidi yalifanyika usiku wa kuamkia leo licha ya taarifa ya Al Shabaab kusema kuwa washambuliaji walioshambulia Mpeketo walikuwa wamerejea salama nchini Somalia.
Uharibifu mkubwa ulishuhudiwa katika mji huo huku washambuliaji wakichoma hoteli na kituo cha polisi pamoja na kuteketeza magari waliyoyatumia kwa usafiri wao.
Kenyatta amesema kuwa kuna baadhi ya wanasiasa wanaochochea uhasama miongoni mwa jamii.
 
Hata hivyo Kenya katika siku za hivi karibuni imekuwa katika hali tete ya mashambulio ya kigaidi likiwepo shambulio kubwa lililowahi kutokea katika Jengo kubwa la Westgate la Jiji Nairobi na kusababisha vifo vya watu kadhaa na mamia wengi kujeruhiwa.
 
Hata hivyo wachambuzi wa mambo wanasema kipigo wanachokipata nchi hiyo ni kutokana na kupeleka wanajeshi wake Nchini Somalia kwa ajili ya kukabiliana na makundi ya kigaidi