September 2017
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Seleman Jafo, akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa kuhusu ukarabati wa vituo 172 vya Afya nchini kote.
 
Serikali imepanga kukarabati vituo vya afya 172 kutokana na fedha kutoka Benki ya Dunia na Ubalozi wa Canada ambapo wametoa jumla ya Dolla za Kimarekani Mil 88 sambamba na Bil.12 fedha za kitanzania zilizovuka katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.


Nteghenjwa Hosseah, Tamisemi – Dodoma.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo akizungumza  katika hafla ya kufungua mafunzo ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi  katika Ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma Leo
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala  za Mikoa  na Serikali za Mitaa  Mhe. Selemani Jafo amewataka Wakuu wa Wilaya  na Wakurugenzi wote nchini kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi  ili kutimiza matarajio  ya watanzania  ambao wanaitegemea Wizara hii kama chachu ya  mabadiliko  katika utendaji kazi wa Serikali ya awamu ya Tano.