October 2016
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Bw John Mongella (kulia) akipokea cheti cha kutambua jitihada zake katika kufanikisha Rock City Marathon kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mbio hizo Bw Zenno Ngowi. Mbio hizo zilizofanyika Septemba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
 
Na Mwandishi wetu,
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Bw John Mongella amesema mkoa wake umejipanga kutumia michezo kama nyenzo muhimu katika kutangaza fursa na vivutio vya utalii vilivyopo mkoani humo.