December 2012
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Barack Obama

Bunge la Marekani linakutana tena leo kujaribu kutafuta suluhisho la mgogoro wa bajeti unaotishia kuitumbukiza nchi hiyo katika mdororo wa uchumi. Jee kuna matumaini yoyote?
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
 Mkoa wa Mwanza unatarajia kufanya uzinduzi wa Chanjo ya  Kimkoa kuhusu Nimonia pamoja na Kuzuia kuhara kwa watototo wenye umri wa wiki sita hadi  Mwaka mmoja.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

MABINGWA wa soka Bara, Simba jana waliogelea kipigo cha mabao 3-0 kutoka Tusker ya Kenya katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa, huku ujio wa kocha wao, Patrick Liewig kutoka Ufaransa ukizidi kutia shaka.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mkutano wa CHADEMA-Karatu

CHAMA  cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza kuwa Katibu Mkuu wake, Dk Willbrod Slaa atapewa fursa ya kuwania nafasi ya Urais kwenye uchaguzi mkuu ujao, mwaka 2015.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mhe. Zitto Kabwe-Mbunge na Waziri kivuli wa fedha

Maandamano ya amani yaliyofanyika mjini Mtwara siku ya alhamis wiki hii yameibua hoja mbali mbali kutoka kwa viongozi, wananchi, vyombo vya habari na mjadala wa siku nzima kwenye mitandao ya kijamii hasa facebook, twitter na JamiiForums.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Raia wa Uswisi Magd Najjar (kulia) akifikishwa mahakamani mjini Nairobi kushitakiwa rasmi kwa kuwa na mafungamano na al-Shabaab. Najjar ni mmoja wa washukiwa wengi wa al-Shabaab wenye utaifa wa nchi mbalimbali wanaodhaniwa wapo Kenya. [Simon Maina/AFP]


Jamii ya Kisomali nchini Kenya imelaumiwa sana kwa mashambulizi ya al-Shabaab, lakini wachambuzi wa masuala ya usalama wanaonya kwamba kuwasingizia Wasomali kunaongeza hatari ya mashambulizi ya baadaye kwani wanamgambo wa jamii nyingine wanaweza kufanya shughuli zao za kigaidi bila kufahamika.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Theo Walcott aliibuka kinara kwa kupachika mabao 3 kati ya 7 ya Arsenal walioifunga NewCastle United uwanja wa Emirates 29-Desemba-2012
Arsenal imeiangushia kipigo kikali New Castle kwa kuicharaza magoli 7-3 katika mchezo wa ligi kuu ya England uliofanyika Jumamosi kwenye uwanja wa Emirates.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Somalia
Ujumbe wa juu kutoka serikali ya Somalia ulikutana na kiongozi wa wapiganaji wa Ras Kamboni Sheikh Ahmed Mohamed Islam huko Kismayu Alhamisi (tarehe 27 Disemba), Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa iliripoti.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Faith Kabura Makena alivunja kikwazo cha kijinsia kwa madereva wa kike wa bodaboda mjini Garissa. [Bosire Boniface/Sabahi]
 Picha ya teksi ya pikipiki ya Faith Kabura Makena kwenye barabara za Garissa nchini Kenya inatoa taswira ya nadra sana.

Makena, mwenye umri wa miaka 30, alisema anajua kwamba kuchagua kwake biashara hii kumesababisha utata na mara kadhaa huwashangaza wakaazi wa huko anapowapita.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Robin Van Persie mfungaji wa bao la pili la Man U dhidi ya West Brom
Manchester United leo imeilaza West Brom magoli 2-0 na kujihakikishia nafasi ya kwanza kwenye msururu wa ligi kuu ya Premier ya England, mwanzo wa mwaka ujao wa 2013.
Gareth McAuley alijifunga mwenye na kuipa Manchester United, bao lao la kwanza kabla ya Robin Van Persie kufunga bao la pili.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Familia zilizoathiriwa kwa mujibu wa Gazeti la Standard Nchini Kenya wakipekuwa mali yao baada ya maporomoko hayo ya Ardhi
Watu wanane wamekufa baada ya nyumba kadha kufukiwa na maporomoko ya ardhi katika eneo la bonde la Kerio, magharibi mwa Kenya, jana usiku.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
An exterior shot of the new Concourse A. The facility has been built specifically to accommodate Emirates' A380 aircraft.

The new facility at Terminal 3 of Dubai’s International Airport is scheduled to receive its first flight in January 2013.
Dubai’s ruler Sheikh Mohammed Bin Rashid Al Maktoum inspected the newly-constructed Emirates’ Airbus A380 Concourse at the Dubai International Airport ahead of its official opening, official news agency WAM reported.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Eng. Evarist Ndikilo alipokuwa akiwasilisha ripoti ya utendaji wa Serikali kwa kipindi cha mwaka 2005/2012
Taarifa ya Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Eng. Evarist Ndikilo Aliyo itoa tarehe 29/12/2012. Alipokuwa akielezea utendaji wa Shughuli za Serikali kwa kipindi cha Mwaka 2005/2012.
Kama ilivyo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Kutoka kwa Mr. Atley Kuni- Afisa Habari wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
SUALA LAKUWAWEZESHA WAJASIRIA MALI NI JAMBO AMBALO MKUU WA MKOA ALILITOLEA MAELEZO, NA JINSI MKOA ULIVYOPIGA HATUA.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewaambia waandishi wa habari jijini hapa, kuwa kama tunafanya vizuri katika maendeleo, basi tusibeze jitihada za serikali, kwani kufanya hivyo nikuwapotosha wananchi.
Aliyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi mbalimbali wa vyombo vya habari jini hapa siku ya tarehe 29.12.2012.
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kocha wa Manchester Sir Alex Ferguson amemshutumu kocha wa Newcastle Allan Pardew na kumtaja kuwa mfarisayo na mnafiki.
Pardew alimshutumu Ferguson kwa utovu wa nidhamu baada ya mechi yao siku ya jumatano.
Pardew amesema shirikisho la mchezo wa soka nchini England, FA lingemuadhibu Ferguson kwa kukabiliana na maafisa waliokuwa wakisimamia mechi hiyo ambayo Manchester United ilishinda kwa magoli 4-3, katika uwanja wa Old Trafford.
'' Allan Pardew ndiye kocha ambaye mara nyingi huwazomema marefa kwa takriban karibu mechi zote'' alisema Ferguson.
Pardew alipigwa marufuku ya kutohudhuria mecho mbili baada ya kupatikana na hatia ya kumsukuma mmoja wa wasimamizi wa mechi yao mwezi Agosti.
Ferguson alimzomea refa wa mechi hiyo Mike Dean, naibu wake Jake Collin na Neil Swarbrick, mwanzo wa kipindi cha pili ya mechi yao ya ligi kuu ya Premier kupinga goli la pili la Newcastle.
Dean aliidhinisha kuwa Papiss Cisse, hakuwa ameotea wakati Jonny Evans alipojifunga kunako dakika 28.
Pardew hakufurahiswa na uamuzi wa FA wa kutomuadhibu kocha huyo wa Manchester United mwenye umri wa miaka sabini.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kocha wa Manchester Sir Alex Ferguson amemshutumu kocha wa Newcastle Allan Pardew na kumtaja kuwa mfarisayo na mnafiki
 

Pardew alimshutumu Ferguson kwa utovu wa nidhamu baada ya mechi yao siku ya jumatano.
Pardew amesema shirikisho la mchezo wa soka nchini England, FA lingemuadhibu Ferguson kwa kukabiliana na maafisa waliokuwa wakisimamia mechi hiyo ambayo Manchester United ilishinda kwa magoli 4-3, katika uwanja wa Old Trafford.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

THE Ilemela District commissioner Amina Masenza has promised to support engagement Strategy between Ilemela Civil Societies Network and Ilemela Municipal Council aiming at enhancing dialogue.
In her closing remark during the climate change adaption and mitigation dialogue yesterday at Buswelu ward in Mwanza City, DC Masenza said that having developed the strategy would be very much important to curb pollution in Ilemela district and entire Mwanza city.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Tanzania's Constitutional Ammendment Commettee Chairperson-Hon Judge Joseph Sinde Warioba
By Moses Matthew  in Mwanza
THE Actions for Democracy and Local Governance in collaboration with Forum Syd have advised the constitutional Review Commission (CRC)  to work in hand with Civil Societies Organizations and community Radios in the coming phase in order to be proficiency .
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mama yake Brayant Sixbert akiwa anampa kampani mwanae katika kutayarisha keki.
Ni tarehe 26/12/2012: Siku ambayo Mtoto Brayant Sixbert Makelele alipoweka historia Nyingine katika maisha yake mara baada ya wazazi wake Kumpeleka kanisani na kubatizwa rasmi katika Kigango cha Nyasaka. Parokia ya Buzuluga Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, na baadaye kufuatiwa na Bonge la Party lililofanyika huko Nyumbani kwao Nyasaka Picha na habari  vyote na  Atley Kuni.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mr Nelson Tugume, the chief executive officer of Inspire Africa, and his wife Atukunda, admire their new born baby girl at Nakasero

hospital on Christmas Day. PHOTO BY STEPHEN OTAGE.
By Frederic Musisi, Abdu Kiyaga, Farahani Mukisa, Abubaker Kirunda, Martin Okudi & Geoffrey Mutegeki
Kampala
Hospitals in Kampala District have registered the largest number of babies born on Christmas
Day, according to a mini-survey done by this newspaper. Out of the 175 babies recorded
countrywide, Kampala hospitals had 119 babies. Out of these, 58 were girls and 61 boys.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Bilawal Bhutto Zardari-Mtoto wa Benazir Bhutto
MWANAWE waziri mkuu wa Pakistan aliyeuawa, Benazir Bhutto, amezindua kuingia
kwake kwenye siasa hii leo ikiwa ni maadhimisho ya mwaka wa tano tangu mamake
kuuawa.
Bilawal Bhutto Zardari anatarajiwa kutangaza malengo yake kwa mara ya kwanza mbele ya maelfu
ya wafuasi nyumbani mwao katika jimbo la Sindh.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Nelson Mandela
Aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela
Aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela, ameruhusiwa kwenda
nyumbani kutoka hospitali moja mjini Pretoria.
Ikulu ya rais nchini humo imesema rais huyo wa zamani wa Afrika kusini, anaendelea kupata nafuu
nyumbani mwake.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza. Eng. Evarist Ndikilo anatarajiwa kukutana na kuzungumza na waandishi wa habari wote mkoani Mwanza tarehe 29-Desemba-2012 kuelezea juu ya taarifa ya mkoa kuhusu maendeleo na changamoto mbalimbali.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Elias Mangu Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Mwanza.
      POLISI mkoani Mwanza imesema iko tayari kuwadhibiti wahalifu watakaojihusisha na vitendo vya uporaji wa mali za wakazi wa jiji la Mwanza wakati wa sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, Eliasi Mangu aliyasema hayo jana jijini Mwanza alipokuwa anaelezea mikakati ya jeshi hilo katika kupambana na uhalifu wakati wa maadhimisho ya sikuukuu hizo.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Krimas 2012

Kiongozi wa waumini wa kikatoliki duniani Papa Benect XVI ameitumia nafasi ya kutoa ujumbe wa Christmas kushambulia ndoa za jinsia moja, na kuwatuhumu mashoga kuwa ni watu ambao wanaubadilisha uhalisia wao ili waweze kuendana na jinsia ambayo ni chaguo lao.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Shinzo Abe
Nchini Japan chama cha kihafidhina cha Liberal Democratic, LDP, kinaelekea kushinda kwa viti vingi katika uchaguzi mkuu.

Taarifa Zinahohusiana!
Vituo vya kupiga kura baada ya kufungwa, matokeo ya awali yalionesha kuwa LDP itapata zaidi ya viti 300
katika bunge la viti 480.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng. Evarist Ndikilo alipokuwa akifungua Mkutano wa RCC tarehe 14 Dec. 2012 Kwenye Ukumbiwa Chuo cha Ben
Na: Atleya Kuni- Mwanza.
Kikao cha kamati cha Ushauri cha Mkoa wa Mwanza (RCC),  mwishoni mwa juma hili wamekutana katika Ukumbiwa Chuo cha Benki jiji Mwanza nakujadili mambo kadha wa kadha yahusuyo maendeleo ya Mkoa Mwanza, Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mokoa wa Mwanza Eng. Evaristi Ndikilo, Alisema lengo la kikao hicho ilikuwa kutahmini ni kwa jinsi gani wameweza kutekeleza yale yote walio azimia katika kikao  kilichopita cha tarehe 03 June 2012.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Ilikuwa siku ya Tarehe 14 Dec. 2012 Wakati Mkurugenzi wa Vijana Nchini Prof. Elisante Ole Gabriel, alipo Hitimu kwa Mara Nyingine PhD ya Pili.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Nelson Mandela
Rais Mstaafu wa Afrika Kusini-Mzee Nelson Mandela
Ikulu ya rais wa Afrika Kusini inasema kuwa Nelson Mandela amefanyiwa uperesheni mjini Pretoria, kutolewa mawe ndani ya kibofu nyongo na anasemekana anaendelea vizuri.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Rais Obama akifuta machozi baada ya taarifa za mauji ya watoto wadogo
Rais wa Marekani-Barack Obama
Kufuatia ya moja kati ya mauaji makubwa kutokea katika historia ya Marekani, wanasiasa akiwemo Rais Barack Obama, wametaka sheria kuhusu umiliki wa bunduki nchini Marekani zibadilishwe, ili kuepusha maafa kama hayo siku za usoni.
Akizungumza baada ya mauaji ya watoto na watu wazima 26 katika shule moja ya msingi katika jimbo la Connecticut Ijumaa, Rais Obama aliyeonekana kujawa na huzuni, alitoa wito kuchukuliwe hatua ya maana kuzuwia mauaji kwa kutumia bunduki.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Hii ni sehemu mojawapo hapa jijini Mwanza ambapo blog hii ilimkuta msukuma mkokoteni huyu akiwajibika.
Kazi hii imewezesha kuwapatia kipato baadhi  ya wakazi wa mkoa huu!
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA



 
    
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 14/12/2012

            KWA NINI LAMBALAMBA WANAPIGWA VITA DODOMA
Kwanza ni lazima tufahamu Lambalamba ni nini?
Hili ni kundi la watu ambalo wameliunda kwa lengo la kujihusisha na vitendo vya kitapeli na ulaghai kwa wananchi hususani wa vijijini, ili kujipatia mali zikiwemo fedha na mifugo ya aina mbalimbali toka kwa wanavijiji katika mkoa wetu wa Dodoma.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mike "Iron" Tyson-Bingwa wa zamani wa uzito wa juu katika masumbwi

Bingwa wa zamani wa ngumi asiyepigika wa uzito wa juu Mike Tyson amesema anajisikia furaha baada ya kufanya upasuaji uliofanikiwa wa kubadilisha jinsia.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

WATU HAWATAKI KUFANYA KAZI WAMEBAKIA KUPIGA SOGA ASUBUHI YA SAA 2,00 HADI JUA LINWAKA UTWAKUTA TU . HAPO KEMONDO, STORI ZAO ZOTE NIKUISEMA SERIKALI KWA NAMNA HII KWELI TUTAFIKA?
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
JOHN MNYIKA-Mbunge wa Jimbo la Ubungo
ORODHA YA UFISADI NA UZEMBE TANESCO AWAMU YA KWANZA NA MWITO WA KUTOA MAONI KUHUSU KUSUDIO LA KUPANDISHA BEI YA UMEME KWA MARA NYINGINE
Shirika la Umeme (TANESCO) linakabiliwa na ufisadi na uzembe unaoongeza gharama za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme kwa upande mmoja na uendeshaji wa shirika kwa upande mwingine.  Ufisadi na uzembe huo unapunguza uwezo wa TANESCO kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika na unaongeza gharama na bei ya upatikanaji wa umeme hali inayoathiri uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa kuchangia katika mfumuko wa bei na ongezeko la gharama za maisha.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mzee Nelson Mandela-Rais Mstaaf wa Afrika Kusini
Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amelezwa hospitali kwa siku ya pili mjini Pretoria ambako alipelekwa Jumamosi.
Maafisa wamesema kwamba amekuwa akifanyiwa uchunguzi, ingawaje haijajulikana kwamba ni uchunguzi wa aina gani.
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Watangazi wawili wa Australia waliopiga simu ghushi hospitalini alipokuwa amelazwa mkewe Prince William, ambaye ni mjamzito wamesema wamehuzunishwa sana na kifo cha muuguzi aliyepokea simu hiyo.
Jacintha Saldanha alikutwa kafariki siku tatu baada ya kupokea simu iliyokuwa inaulizia kuhusu hali ya Duchess wa Cambridge, aliyekuwa hospitalini akiuguzwa ugonjwa unaohusika na mimba yake.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Wanafunzi wa shule wa elimu maalum Kakola wilayani Kwimba katika maadhimisho ya miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Imeelelezwa kwamba pamoja na Tanzania kuadhimisha miaka hamsini na moja ya Uhuru bado pato la mwana Mwanza lipo chini ya kiwango cha kawaida ukilinganisha na rasilimali ziliopo mkoani humo.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evaristi Ndikilo wakatiwa maadhimisho ya miaka hasini na moja ya uhuru wa Tanzaniabara yaliofanyika kimkoa katika Wilaya ya Kwimba.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Hivi ndivyo Mwandishi wa Blog hii alipo mkuta bibi Thabitha Ngalaba, Eneo la Station ya Mwanza akiosha kioski chake cha kuuzia Samaki. sikumoja kabla ya treni kuingia Mkoani Mwanza. Eneo la station lilikuwa Maarufu na Wajasiriamali wadogo katika kujipatia kipato.



Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Mhe. Zitto Kabwe-Waziri Kivuli wa Uchumi (MB-Kigoma Kaskazini)

Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini ndugu Zitto Zuberi Kabwe ameanza ziara ya kikazi nchini Ujerumani ambapo atahudhuria na kuhutubia Mkutano mkubwa wa masuala ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya Ujerumani na Africa. Mkutano huo “Economic Conference: Commitment to Africa Initiative” utafanyika Jijini Berlin kuanzia tarehe 9 – 11 Desemba 2012 na umeandaliwa na Wizara ya Ushirikiano wa Kimaendeleo ya Serikali ya Ujerumani.

no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Rais Morsi anapingwa kwa kujiongeza mamlaka
Upinzani nchini Misri umebatili kauli yao ya awali ambapo walisema wako tayari kukutana hii leo kujadili wito wa Rais Mohammed Morsi, wa kutaka maauzngumzo kati ya serikali na makundi ya upinzani.
Sasa wanasema hawako tayari kwa mazungumzo hayo huku nchi hiyo ikijiandaa kwa siku nyingine ya maandamano kupinga hatua ya Rais Morsi kujilimbikizia mamlaka.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Katibu Tawala Msaidiz Mipango na Uratibu Mkoa wa Mwanza Bibi Issabela Marick.

KIKAO cha kamati ya ushauri cha Mkoa wa Mwanza (RCC ) kinatarajia kufanya mkutano wake tarehe 14/12/2012, katika Ukumbi wa Chuo cha Benki jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mratibu wa kikao hicho, Katibu Tawala msaidizi wa Seksheni ya mipango na uratibu Bibi Issabela Marick, amesema katika kikao hicho mambo kadhaa ya Maendeleo yatajadiliwa na kutolea tathmini ya mambo ambao yalikuwa yamejadiliwa katika vikao vilivyopita.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Sherehe za miaka hamasini na moja ya Uhuru wa Tanzania Bara zina tarajia kufanyika tarehe 09/Dec.2012.
Sherehe hizo katika mkoa wa Mwanza zitafanyika katika, Kimkoa katika Wilaya ya Kwimba, na Mgeni Rasmi anategemewa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng. Evarist Ndikilo, Pamoja na mambo mengine Mkuu huyo wa Mkoa Atazungumzia hali ya Kimaendeleo ya Mkoa huo, ikiwa ni pamoj na kuhimiza suala la Amani na Utulivu.
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Wanuswa kwapa kama mahojiano
Hata ujuzi pia hauna maana.
Huko ni China.
Shirika maarufu la Uchina, HAINAN AIRLINE limeweka masharti kwamba mbali na elimu na uzoefu
lazima usinuke. Ukiwa mwili wako una harufu mbaya basi kazi huna. Ni China huko.
Kwa mujibu wa gazeti la SZ News shirika hilo katika kuajiri marubaNi wapya lazima mtu ananuswa
makwapa.
no image
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Wanajeshi nchini Misri wameanza kuwafukuza waandamanaji, ikiwa ni pamoja na waandishi wa mashirika mbalimbali ya habari, waliokusanyika nje ya kasri ya rais mjini Cairo.
Hatua hiyo ni kufuatia ghasia za usiku kucha kati ya waandamanaji wanaomuunga mkono Rais Mohammed Morsi, na wale wanaompinga.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
SIDO Mwanza
Maonesho ya Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO)  yanayo fanyika jiji Mwanza katika Viwanja vya Nyamagana, yameonekana kuwa kivutia kikubwa kwa wakaazi wa Jiji hilo, Mwandishi wa Blog hii alivyofika alishuhudia bidhaa mbalimbali zilizo tengenezwa na Wazalendo wa nchi hii zikwa zimepedeza, nakufanya kununuliwa na wadau Mbalimbali waliofika kujionea Maonesho hayo.