|
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGULI ALIPOKUWA AKITANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI KUSHOTO NI MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU NA KULIA NIA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA. |
Magufuli:
Kumekuwa na speculation nyingi na watanzania wamekuwa na hamu kubwa ya kujua
baraza la mawaziri, baada ya kusubira kwa muda mrefu, baada ya kuapa tulitakiwa
angalau tarehe kumi tuwe tumetangaza baraza.
Tuliona angalau tujiridhishe kwanza, baraza lililopita lilikuwa na mawaziri na
manaibu zaidi ya 59, tukaona tuwe na baraza dogo. Hatuwezi kukaa bila baraza,
katika baraza hili, wizara nyingi tumeziunganisha na kutakuwa na wizara 18 na
tutakuwa na mawaziri 19 tu, kuna baadhi ya wizara zitakuwa na mawaziri na
hazitakuwa na manaibu waziri.
Lengo ni kutimiza ahadi yetu ya kuwa na baraza dogo kupunguza gharama na
effective kwa kufanya kazi. Zilitengwa bilioni 2, mawaziri watakapoteuliwa
waende semina elezi, baraza nitakaloliteua halitakuwa na semina elekezi na
fedha tutaelekeza sehemu nyingine kama ni madawati au kwenye elimu bure.
Watafanya semina elekezi wenyewe ndani kwa ndani.
WIZARA
Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora: Mawaziri ni George
Boniface Taguluvala Simbachawene na Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, Naibu
waziri Selemani Saidi Jafo.
Ofisi ya makamu wa Rais, muungano na mazingira: Waziri ni January Yusuf
Makamba, naibu Luhaga Mpina
Ajira, walemavu: Jenista Joakim Mhagama, Naibu nimemtua mbunge, Abdallah
Possi. M ambae ni mhadhiri Dodoma
Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu:
Waziri ni Jenista Muhagama, manaibu Anthony Mavunde, Possy Abdallah.
Kilimo, mifugo na uvuvi:
Waziri ni Mwigulu Lameck Nchemba, naibu William Ole Nasha
Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano: Waziri bado sijamtafuta, naendelea
kumfikiria, Naibu waziri mhandisi Edwin Ngonyani.
Fedha na mipango: Waziri bado tunamtafuta, naibu waziri ni Ashantu
Kizachi
Nishati na madini: Waziri ni Professa Sospeter M. Muhongo, Naibu waziri
ni Medalled Karemaligo
Katiba na sheria: Waziri Harrison George Mwakyembe
Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa:
Waziri ni Augustine Philip Mahiga ambae nimemteua kuwa mbunge na kisha
waziri, Naibu ni Dr Suzan Kolimba.
Ulinzi na kujenga taifa: Waziri ni Dr. Hussein Ali Mwinyi
Mambo ya ndani: Charles Muhangwa Kitwanga
Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi: Waziri ni William Vangimembe
Lukuvi, Naibu Angelina Mabula
Maliasili na Utalii: Waziri bado, naibu ni Ramo Makala
Viwanda, biashara na uwekezaji: Waziri Charles John Poul Mwijage
Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi: Waziri bado hajapatikana, Naibu ni
Stella Manyanya
Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto: Waziri Ummy Ally
Mwalimu, Naibu ni Hamisi Andrea Kigwangalla
Habari, utamaduni, wasanii na michezo: Waziri Nape Nnauye, naibu
Anastazia Wambura
Wizara ya maji na umwagiliaji: Waziri Makame Mnyaa Mbarawa ambae
nilimteua kuwa mbunge, Naibu ni Isack Kamwela
=====================
Swali: Kuna baadhi hukutaja, tatizo ni nini hasa kwa wizara ambazo
hujateua? Wabunge wa chama chako hawana sifa? Usimamizi wa baraza unatarajia
zitafanya kazi zake Dodoma ukiondoa TAMISEMI?
Magufuli: Nilitegemea ungeniuliza kwanini sikuteua siko niliyoteuliwa, subira
yavuta heri, hawa wameanza na wengine watafata. Usiwe na haraka. Kuhusu Dodoma
tutatekeleza yaliyoko kwenye ilani ya chama cha mapinduzi.
Swali: Umesema hakutakuwa na semina elekezi, utafanya nini waweze kwenda
na kasi ya hapa kazi?
Magufuli: Niliyowachagua wote wana CCM na wengi wao ni wabunge, walinadi
ya sera hapa kazi na ndio maana haja ya semina elekezi, spidi ni hiyo hiyo ndio
maana hatutatumia semina elekezi ya bilioni mbili.
Manyerere Jackton: Kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri na kwa
kulinganisha na tulipotoka, serikali itakuwa imepunguza kiasi gani?
Magufuli: Wewe ndie utapiga hesabu, kwa vile ni mmiliki wa gazeti huwa
unapiga hesabu huwa unapata kiasi gani. Utanisaidia katika kupunguza baraza
tutakuwa tumesevu kiasi gani na zile tulizosevu za gharama elekezi, kuchelewa
kutangaza baraza na wale ambao sijawataja na bahati nzuri nyie waandishi
mnaweza kupiga hesabu vizuri. Zipo nchi zina mawaziri wengi mpaka kufikia hata
70, wizara 44, manaibu na mawaziri. Tutakapomaliza tutakuwa na baraza la watu
34 tu.
Wakienda kule mawaziri wakafanye kazi kweli ndio maana sisi tulipochaguliwa
tulifanya kazie kweli na hatukwenda kwenye semina elekezi na tulijielekeza,
wakajieleze kwenye maeneo yao.
Wasihangaike kufanya sherehe kwa sababu ni kazi ngumu na kama wapo wanaopenda
kufanya sherehe wajiandae kufanya sherehe siku wakifukuzwa, contract ni miaka
mitano. Wakawafanyie kazi watanzania bila kuwabagua, Baraza hili la wizara 15
tumejiridhisha linaweza kufanya kazi tunayowatarajia kuifanya effectivly. Ngoja
tukimaliza uteuzi wote tutajua tumesave kiasi gani ili ziweze kwenda kwa
wananchi.
Raymond(Uhai Production): Siku saba zimetimia, wafanyabiashara
wamesharesha zile hela?
Magufuli: Swali hilo kamuulize kamshna wa kodi TRA.
SWALI: Kuna wizara ina mawaziri wawili, huko kazi ngumu?
Magufuli: Kafanye utafiti hio wizara imeunganisha wizara ngapi, utapata
majibu.
Swali: Katika baraza, kuna mawaziri wa baraza lililopita, ulizangatia
nini wakati wa uteuzi?
Magufuli: Umekosea hata kupiga hesabu, Kafanye hesabu vizuri, waliorudi
ni saba na sio kumi? Ukipiga utaelewa ni vigezo gani nilivyotumia.
Asanteni sana na ninawashukuru