December 2015
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

 

OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA

 

 
TAARIFA KWA UMMA.


YAH: MLIPUKO WA UGONJWA WA HOMA YA NGURUWE

 

Kumetokea mlipuko wa ugonjwa wa Homa ya Nguruwe (African Swine Fever) Wilaya ya Nyamagana, Kata za Mabatini, Mirongo kishiri na Buhongwa na Igoma. Mlipuko huu umedhibitishwa kwa uchunguzi uliofanyawa na Maabara ya Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA)

 

Ugonjwa wa Homa ya Nguruwe unasababishwa na Virusi (African Swine fever virus). Madhara yake ni makubwa kwa wafugaji na kiuchumi kwani husababisha vifo asilimia 100 (100%) kwa Nguruwe wote walioambukizwa.

Ugonjwa wa Homa ya Nguruwe hauna chanjo wala tiba na hauambukizi Binadamu. Njia pekee ya kudhibiti ugonjwa huu ni kuzuia kueneoa kwa maambuzi toka eneo lenye maambukizi kwenda eneo lisiloambukizwa.

HATUA  ZA TAHADHARI KUZUIA KUENEA KWA UGONJWA WA HOMA YA NGURUWE

 

·         Wafugaji waepuke kununua Nguruwe kutoka kwenye Maeneo/Mashamba yenye ugonjwa

·         Nguruwe wafugwe kwenye Mabanda imara na waepuke kutembea ovyo

·         Nguruwe wasilishwe mizoga au masalio ya chakula kutoka vyanzo visivyojulikana

·         Teketeza Mizoga iliyokufa kwa ugonjwa na ufanye usafi kwa kuzingatia maelekezo ya watalaam na kwa kutumia dawa za kuua vimelea vya magonjwa (disinfectants)

·         Wakulima watoe taarifa ya uwepo wa ugojwa haraka kwa mtalaa wa Mifugo aliye karibu

·         Wananchi wazingatie maelekzo yote yanaotolewa pindi watalaam wa Mifugo wanapoweka Tangazo la Karantini (QUARANTINE) la kuzuka kwa   ugonjwa wa Homa ya Nguruwe

·          

IMETOLEWA LEO 11. DESEMBA, 2015.


Dkt Yohana D. Sagenge

Kny: KATIBU TAWALA (M)

MWANZA
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGULI ALIPOKUWA AKITANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI KUSHOTO NI MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU NA KULIA NIA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA.
Magufuli: Kumekuwa na speculation nyingi na watanzania wamekuwa na hamu kubwa ya kujua baraza la mawaziri, baada ya kusubira kwa muda mrefu, baada ya kuapa tulitakiwa angalau tarehe kumi tuwe tumetangaza baraza.

Tuliona angalau tujiridhishe kwanza, baraza lililopita lilikuwa na mawaziri na manaibu zaidi ya 59, tukaona tuwe na baraza dogo. Hatuwezi kukaa bila baraza, katika baraza hili, wizara nyingi tumeziunganisha na kutakuwa na wizara 18 na tutakuwa na mawaziri 19 tu, kuna baadhi ya wizara zitakuwa na mawaziri na hazitakuwa na manaibu waziri.

Lengo ni kutimiza ahadi yetu ya kuwa na baraza dogo kupunguza gharama na effective kwa kufanya kazi. Zilitengwa bilioni 2, mawaziri watakapoteuliwa waende semina elezi, baraza nitakaloliteua halitakuwa na semina elekezi na fedha tutaelekeza sehemu nyingine kama ni madawati au kwenye elimu bure. Watafanya semina elekezi wenyewe ndani kwa ndani.

WIZARA
Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora: Mawaziri ni George Boniface Taguluvala Simbachawene na Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, Naibu waziri Selemani Saidi Jafo.

Ofisi ya makamu wa Rais, muungano na mazingira: Waziri ni January Yusuf Makamba, naibu Luhaga Mpina

Ajira, walemavu: Jenista Joakim Mhagama, Naibu nimemtua mbunge, Abdallah Possi. M ambae ni mhadhiri Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu: Waziri ni Jenista Muhagama, manaibu Anthony Mavunde, Possy Abdallah.

Kilimo, mifugo na uvuvi: Waziri ni Mwigulu Lameck Nchemba, naibu William Ole Nasha

Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano: Waziri bado sijamtafuta, naendelea kumfikiria, Naibu waziri mhandisi Edwin Ngonyani.

Fedha na mipango: Waziri bado tunamtafuta, naibu waziri ni Ashantu Kizachi

Nishati na madini: Waziri ni Professa Sospeter M. Muhongo, Naibu waziri ni Medalled Karemaligo

Katiba na sheria: Waziri Harrison George Mwakyembe

Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa: Waziri ni Augustine Philip Mahiga ambae nimemteua kuwa mbunge na kisha waziri, Naibu ni Dr Suzan Kolimba.

Ulinzi na kujenga taifa: Waziri ni Dr. Hussein Ali Mwinyi

Mambo ya ndani: Charles Muhangwa Kitwanga

Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi: Waziri ni William Vangimembe Lukuvi, Naibu Angelina Mabula

Maliasili na Utalii: Waziri bado, naibu ni Ramo Makala

Viwanda, biashara na uwekezaji: Waziri Charles John Poul Mwijage

Elimu,Sayansi Teknolojia na Ufundi: Waziri bado hajapatikana, Naibu ni Stella Manyanya

Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto: Waziri Ummy Ally Mwalimu, Naibu ni Hamisi Andrea Kigwangalla

Habari, utamaduni, wasanii na michezo: Waziri Nape Nnauye, naibu Anastazia Wambura

Wizara ya maji na umwagiliaji: Waziri Makame Mnyaa Mbarawa ambae nilimteua kuwa mbunge, Naibu ni Isack Kamwela

=====================

Swali: Kuna baadhi hukutaja, tatizo ni nini hasa kwa wizara ambazo hujateua? Wabunge wa chama chako hawana sifa? Usimamizi wa baraza unatarajia zitafanya kazi zake Dodoma ukiondoa TAMISEMI?

Magufuli: Nilitegemea ungeniuliza kwanini sikuteua siko niliyoteuliwa, subira yavuta heri, hawa wameanza na wengine watafata. Usiwe na haraka. Kuhusu Dodoma tutatekeleza yaliyoko kwenye ilani ya chama cha mapinduzi.

Swali: Umesema hakutakuwa na semina elekezi, utafanya nini waweze kwenda na kasi ya hapa kazi?

Magufuli: Niliyowachagua wote wana CCM na wengi wao ni wabunge, walinadi ya sera hapa kazi na ndio maana haja ya semina elekezi, spidi ni hiyo hiyo ndio maana hatutatumia semina elekezi ya bilioni mbili.

Manyerere Jackton: Kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri na kwa kulinganisha na tulipotoka, serikali itakuwa imepunguza kiasi gani?

Magufuli: Wewe ndie utapiga hesabu, kwa vile ni mmiliki wa gazeti huwa unapiga hesabu huwa unapata kiasi gani. Utanisaidia katika kupunguza baraza tutakuwa tumesevu kiasi gani na zile tulizosevu za gharama elekezi, kuchelewa kutangaza baraza na wale ambao sijawataja na bahati nzuri nyie waandishi mnaweza kupiga hesabu vizuri. Zipo nchi zina mawaziri wengi mpaka kufikia hata 70, wizara 44, manaibu na mawaziri. Tutakapomaliza tutakuwa na baraza la watu 34 tu.

Wakienda kule mawaziri wakafanye kazi kweli ndio maana sisi tulipochaguliwa tulifanya kazie kweli na hatukwenda kwenye semina elekezi na tulijielekeza, wakajieleze kwenye maeneo yao.

Wasihangaike kufanya sherehe kwa sababu ni kazi ngumu na kama wapo wanaopenda kufanya sherehe wajiandae kufanya sherehe siku wakifukuzwa, contract ni miaka mitano. Wakawafanyie kazi watanzania bila kuwabagua, Baraza hili la wizara 15 tumejiridhisha linaweza kufanya kazi tunayowatarajia kuifanya effectivly. Ngoja tukimaliza uteuzi wote tutajua tumesave kiasi gani ili ziweze kwenda kwa wananchi.

Raymond(Uhai Production): Siku saba zimetimia, wafanyabiashara wamesharesha zile hela?

Magufuli: Swali hilo kamuulize kamshna wa kodi TRA.

SWALI: Kuna wizara ina mawaziri wawili, huko kazi ngumu?

Magufuli: Kafanye utafiti hio wizara imeunganisha wizara ngapi, utapata majibu.

Swali: Katika baraza, kuna mawaziri wa baraza lililopita, ulizangatia nini wakati wa uteuzi?

Magufuli: Umekosea hata kupiga hesabu, Kafanye hesabu vizuri, waliorudi ni saba na sio kumi? Ukipiga utaelewa ni vigezo gani nilivyotumia.

Asanteni sana na ninawashukuru