MAKAAZI YA RAIS ZUMA NDIO HAYA.



















Rais Jacob Zuma anatarajiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge la A-Kusini kujieleza kuhusu kashfa ya kufuja pesa za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake ya kifahari.

Ukarabati huo uligharimu dola million 23 na Bw Zuma ameamrishwa na mkaguzi au mlinzi wa mali ya umma nchini humo alipe baadhi ya pesa hizo .

Zuma alisema Jumatatu kuwa sio sawa kwake kutakiwa alipe sehemu ya pesa zilizotumiwa kwa ukarabati wa nyumba yake kwani sio yeye aliayeamuru ukarabati huo.

Alisema kuwa maafisa wa serikali ndio walioagiza ukarabati huo bila ya kumshauri.

Zuma alizungumza kwa mara ya kwanza Jumatatu tangu kashfa hiyo kujulikana akisema kuwa halipi chochote kwani hakuomba ukarabatai kufanywa.
Axact

Post A Comment: