Na Atley Kuni. Mwanza.

HILI NDILO KOMBE LINALO INGIA MWANZA.



 

KIKAO NA WAANDISHI WA HABARI MWANZA.

Kwa mara ya kwanza Kombe la Dunia litapokelewa Mkoani Mwanza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uwanja wa CCM Kirumba.
 



 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo, mbele ya waandishi wa habari na kamati ya maandalizi ya ujio huo katika ukumbi wa Mwanza Hotel hivi leo.
 
Ndikilo amesema hii ni mara ya kwanza kwa kombe hilo kupokelewa katika Mkoa huo na akawataka wanachi kujitokeza kwa wingi ili kuweza kulipokea,amesema na kuongeza kuwa "Mhe shimiwa Rais ambaye yupo ziarani katika Mkoa wa Simiyu amekubali kulilaki kombe hilo katika mkoa wetu wa Mwanza hii ni heshima kubwa kama wananchi wa Mkoa huu na wapenda michezo kwa ujumla.
 
Amesema kombe hilo litawasili katika uwanja wa ndege wa mwanza majira ya saa tatu asubuhi na badae kupelekwa katika uwanja wa CCM Kirumba, ambapo pamoja na mambo mengine baadhi ya wananchi watapata fursa ya kupiga picha na kombe hilo.
 
Kwa upande wake Mwakilishi wa Coca Cola Nchini bw. Eyebolt Gretchen, amesema ujio wa Kombe hilo kwa mara ya tatu katika nchi ya Tanzania nia pamoja na amani ya nchi iliyopo na ukarimu wa watu wake, Miongoni mwa nchi za Afrika ambazo zimekuwa na utulivu hata kufanya kutembelewa na kombe la Dunia ni Tanzania, amesema na kuongeza kwamba, kama Coca cola wamekuwa mstari wa mbele kwenye jitihada za kukuza soka nchini ikiwapo mashindano ya Kopa Coca cola.
 
Kwa upande wake kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ernest Mangu amewahakikishia wanachi wote wa Mkoa wa Mwanza amani na utulivu, aidha amewaomba wananchi kutokuja wanjani hapo wakiwa na watoto wadogo ili kuepusha adha wanayoweza kupata watoto hao" Labda niombe ndugu zangu kwa wale watoto wadogo ni vema wakaachwa nyumbani kuepuka usumbufu". alisema na kuongeza kuwa watu hawataruhusiwa kusogea karibu na eneo la Pitch ya uwanja huo.
 
Hii ni mara ya tatu kombe hilo linakuja hapa nchini ambapo mara zote limekuwa likipokelewa na kulakiwa na wananchi waishio katika Mkoa wa Dar es Salaam. 
 
Wadadisi wa mambo wanasema kwamba, ujio wa kombe hilo si tu kwamba linakuja kutazamwa na wanachi wa Mwanza bali pia ni frsa nzuri kwa mkoa huo kujitangaza kimataifa lakini pia kutangaza rasilimali zinazo patikana katika Mkoa huo alkini pia iwe chachu kwa vingozi kuona kuna umuhimu wa kuipa kipaumbele michezo yote, anasema Mashaka Baltazari mwandishi mwandamizi wa Jambo Leo na Mwakilishi Mkoani Mwanza.
 
Axact

Post A Comment: