Kulia Naibu Waziri wa Tamisemi Kasimu Majaliwa akitoa taarifa ya kuteuliwa kwa wanafunzi wa kidato cha tano kushoto ni Benard Makali Mkurugenzi anayeshuhulikia Elimu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi.
 
 Jumla ya wanafunzi wapatao 235,227 wa kidato cha nne mwaka 2013 sawa na asilimia 58.21 ya watahiniwa wote wamefaulu kujiunga na kidato cha tano pamoja na vyuo mbalimbali vya serikali, matokeo hayo yanaonesha kiwango cha ufaulu kimepanda kwa asilimia 15.13.
Naibu Waziri wa Tamisemi Kasim Majaliwa alisema kuwa, takwimu zinaonesha kuwa kumekuwa na ongezeko la ufaulu kwa wahitimu wa kijitegemea kutoka 26,193 sawa na asilimia 43.07 mwaka 2012 hadi kufikia watahiniwa 34,075 sawa na asilimia 66.21 kwa mwaka 2013 kwa kulinganisha na mwaka 2012 lipo ongezeko la asilimia 30.09.
Majaliwa alifafanua kuwa ufaulu kwa mwaka 2013 katika daraja kwanza hadi la tatu umefikia watahiniwa 71,527 sawa na asilimia 20.28 ya watahiniwa waliofanya mtihani Tanzania Bara, hivyo kuna ongezeko la ufaulu wa asilimia 106.73 ikilinganishwa na matokeo ya ufaulu mwaka 2012.
Uteuzi huo wa ufaulu wa wanafunzi wa kujiunga kidato cha tano umefanyika kwa kutumia kompyuta kwa kuzingatia machaguo ya wanafunzi pamoja na ufaulu, hivyo hapatakuwa na mabadiliko, pia wanafunzi wote wametakiwa kuripoti shuleni tarehe 10 Juni mwaka huu.
Wanafunzi ambao watashindwa kuripoti shuleni hadi tarehe 30 Juni mwaka huu nafasi zao zitajazwa na wanafunzi ambao wamekosa nafasi.
Axact

Post A Comment: