Wasimamizi waaswa kuzingatia Sheria, kanuni na taratibu
Imefahamika kwamba maandalizi muhimu ya uchaguzi mkuu kwa mikoa ya kanda ya ziwa yanaendelea vizuri huku, waratibu wa uchaguzi, wasimamizi na maafisa uchaguzi kutoka mikoa ya Mwanza na Mara wakiaswa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu wakati wa zoezi la mchakato kuelekea Octoba 25 mwaka huu ili kuepusha malalamiko yanayoweza kujitokeza mara baada ya uchaguzi kumalizika. endelea baada ya picha.......


Mwanasheria wa tume ya uchaguzi Bw.Mtibora Seleman akifafanua jambo wakati wa semina hiyo.

Wanasemina wakifatilia kwa karibu mafunzo hayo yanayofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Wanasemina ya masuala ya Uchaguzi kanda ya ziwa wakiwa darasani.

Msisitizo kutoka kwa mwanasheria.

Bi. Jescar Mongi kutoka tume ya uchaguzi hapa akionesha mfano wa utaratibu wa upigaji kura utakavyokuwa.

Imefahamika kwamba maandalizi muhimu ya uchaguzi mkuu kwa mikoa ya kanda ya ziwa yanaendelea vizuri huku, waratibu wa uchaguzi, wasimamizi na maafisa uchaguzi kutoka mikoa ya Mwanza na Mara wakiaswa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu wakati wa zoezi la mchakato kuelekea Octoba 25 mwaka huu ili kuepusha malalamiko yanayoweza kujitokeza mara baada ya uchaguzi kumalizika.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku mbili iliyo andaliwa na Tume ya taifa ya uchaguzi na kuhusisha Waratibu wa uchaguzi wa mikoa, wasimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wasaidizi, na maafisa uchaguzi kutoka katika mikoa ya Mwanza na Mara Kaimu mkuu wa mkoa wa Mwanza Manju Msambya, amesema watumishi hao wanayo dhima ya kuhakikisha zoezi la uchaguzi linakwenda vizuri kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Msambya amesema nilazima dhamana waliopewa watumishi hao watambue  ni muhimu kwakua inakwenda kutoa mustakabali wa taifa letu na wapi tunako taka kuelekea kwa kuchagua viongozi kwa nafasi za udiwani, ubunge na urais. “Ndugu wanasemina tambueni kwamba, madhumuni ya semina hii nikuwajenge uwezo katika mchakato mzima wa uteuzi wa wagombea, upigaji kura, kuhesabu, kujumlisha pamoja na kutangaza matokeo ya uchaguzi” hivyo suala la umakini ni muhimu sana.

Msambya amesema, kwakutumia uzoefu walionao watumishi hao katika mazoezi mbali mbali ya kitaifa wataweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa hasa ikizingatiwa kwamba wengi wao walishiriki katika zoezi kama hilo kwa mwaka 2010.

Awali akimkaribisha kufungua semina hiyo Mratibu wa uchaguzi wa kanda ya ziwa Deogratius Nsanzugwanko alisema tayari maandalizi kadhaa kuhusiana na uchaguzi yamekwisha kamilika ikiwapo madaftari ya mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na vifaa vyote muhimu kuwa tayari vimekwisha anza kusafirishwa kwenda kwenye mikoa husika.

Kanda ya ziwa inayoundwa na mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Kagera, Simiyu na Mara, ambapo kwa mkoa wa Mwanza pekee inakadiriwa kuwa na wapiga kura 1,442,391 sawa na asilimia 103% ya lengo lililokuwa limewekwa hapo awali na bodi ya takwimu ya mkoa wa Mwanza ya kuandikisha wapiga kura 1,403,763.

 Imeandaliwa  Na: Atley Kuni- The Power of Media grew.

 

MWISHO.   
Axact

Post A Comment: