Bibi Leah Mwainyekule, akitoa ufafanuzi kuhusu Semina hiyo juu ya utunzaji fedha katika Vituo vya Afya na Shule Jiji Mwanza
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Wakili Msomi Kiomoni Kiburwa Kibamba, amewagiza wataalam kutoka ngazi ya Kata za Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela kuzitumia ipasavyo tovuti za Halmashauri na mikoa katika kuweka mapato na matumizi ili kuongeza uwazi kwa wananchi.
Kaimu Mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Omary Kamatta akifungua Semina hiyo ya siku mbili inayo washirikisha, Waratibu Elimu kata wa Jiji na Manispaa ya Ilemela katika ukumbi wa mkuu wa Mkoa wa Mwanza.


Akisoma hotuba kwa niaba ya Mkurugezi wa Jiji la Mwanza, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo, Omary Kamatta, amesema ili wananchi wawe na imani na serikali yao, suala la uwazi lazima litiliwe maanani “nielekeze matumizi ya tovuti za Mikoa na Halmashauri katika kuweka taarifa zote za mapato na matumizi ya fedha za umma” alisema Kamatta na kuongeza kuwa   suala hilo ni maelekezo ya Serikali, na kila mmoja analijua na anapaswa kutekeleza.
Bwanakher Mmmoja ya Wakufunzi wakati wa Semina hiyo kwa Waratibu Elimu Kata na wasimamizi wa Vituo vya Afya.

Kamatta amesema, Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma ujulikanao kwa Kiingereza kama Public Sector Systems Strengthening, (PS3), uliowezesha mafunzo hayo ya Mfumo wa Uhasibu na Utoaji Taarifa za Fedha kwa ngazi ya Kituo cha Kutolea Huduma [Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)], una lengo la kuongeza ufanisi, hususan katika masuala mazima ya mapato, na ndio utakuwa mtatuzi wa malalamiko ya wananchi.

Ameongeza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma, na kusaidia upatikanaji wa taarifa sahihi katika mahesabu ya mapato na matumizi katika halmashauri kote nchini.Mafunzo haya yanafanyika sambamba katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, ili kuhakikisha kwamba nyote mnakuwa katika nafasi ya kwenda kuwafundisha watoa huduma mbalimbali katika Vituo vyote vya kutolea Huduma Tanzania Bara, yaani (Service providers or Facilities), ambavyo vinajumuisha Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali, Shule za Sekondari na za Msingi” alisema Kamatta.
Mkurugenzi wa Manispaa ya ilemea John Wanga, akisema maneno yakuwaasa washiriki wa Semina hiyo juu yakuzingatia yote watakayo fundishwa.

Akitoa maelezo ya awali, msimamizi mafunzo hayo katika Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela, Mkuu wa Mawasiliano wa PS3, Bibi Leah Mwainyekule, amesema kuanzia mwaka ujao wa fedha, yaani Julai 1, 2017, Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania itaanza kupeleka rasilimali fedha moja kwa moja kwenye vituo vya afya kwa ngazi za vituo vya kutolea huduma ambavyo vitapokea fedha hizo vinavyojumuisha Zahanati, Vituo vya Afya, na Hospitali za Wilaya.  Aidha zoezi hilo litakwenda sambamba na inavyotekelezwa kwenye sekta za elimu, Serikali za Vijiji na Ofisi za Kata.

Bibi Mwainyekule amesema, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), wametoa mafunzo ya kina kwa wakufunzi  490 katika ngazi ya taifa na halmashauri nchini kote.  Mafunzo hayo yalifanyika katika mikoa ya Dodoma, Mbeya, Mtwara, na Shinyanga, ambao nao sasa wanajukumu kuwawezesha watumishi katika vituo vya Sekta ya Afya na Elimu kupata ujuzi wa namna ya kutumia mfumo mpya wa FFARS.

 

Mwainyekule  amesema, wakufunzi hao kwa sasa ndio wanaotoa elimu hiyo kwa watumiaji wa mwisho wa mfumo wa FFARS kwa ngazi ya Vituo vya Afya 550, Zahanati 6800, Hospitali za Wilaya 135, na takribani Shule za Msingi na Sekondari 20,000 katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara, vikiwemo vituo vya kutolea huduma kutoka Mikoa 13 na Halmashauri 93 zinazotekeleza Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3).

Mafunzo hayo yatahakikisha kuwa watoa huduma katika vituo wana ujuzi unaohitajika katika usimamizi wa fedha na kutoa huduma bora kwa wananchi wote Tanzania na kwa jamii zenye uhitaji.

Mfumo wa FFARS unatekelezwa kwa ushirikiano baina ya Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI); Wizara ya Fedha na Mipango; Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi; na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na USAID
Axact

Post A Comment: