Watumishi mkoa wa Mwanza kuwezesha kituo cha damu salama kanda ziwa kuwa na damu yakutosha ili kuweza kukidhi mahitaji halisi yanayo fikia chupa za ujazo 78,000 kwa mwaka.

MKUU WA MKOA WA MWANZA AKIZUNGUMZA KATIKA MOJA YA VIKAO VYAKE MKOANI HUMO.
Hayo yamesemwa na wakuu wa taasisi za umma waliopo Mkoani Mwanza wakati wa kikao cha pamoja na mkuu wa mkoa wa Mwanza kama sehemu yakujitambulisha kwa mkuu huyo wa mkoa, lakini pia kuelezea shughuli zao wanazo zifanya katika mkoa huo.
Akizungumza kwa niaba ya wakuu wengine wa taasisi hizo mkurugenzi wa maji safi na maji taka jiji Mwanza Mhandisi Antony Sanga, amesema wao kama Mamlaka ya maji safi na maji taka Jijini Mwanza wapo tayari kutoa elimu kwa watumishi walioko chini yao juu ya umuhimu wa kuchangia damu kwenye kituo cha damu salama huku akiahidi kutoa ushirikiano wa kutosha wakati wa zoezi hilo “Katibu Tawala naomba niwahakikishie kuwa sisi kama mamlaka tunao watumishi wengi ambao ninaimani tukiwaeleimisha vizuri watachangia damu bila matatizo kwa kuwa suala la damu ni suala mtambuka linalo mgusa kila mmoja wetu leo unaweza usione umuhimu wa kuchangia lakini tatizo likikutokea kwako mwenyewe au ndugu yako ndio utaona umhimu wake” alisema Sanga.
Kwa Upande wake mkurugenzi wa hospitali ya Rufaa Bugando alisema ni kweli kituo cha damu salama kimekuwa na changamoto ya uwepo wa damu salama hivyo ni vema kama taasisi za umma wakubaliane juu ya mpango huo.
Akiwasilisha ombi hilo kwa wakuu hao wa taasisi Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Faisal Issa, amesema ni jambo lisilo kubalika katika karne hii kupoteza maisha ya watu kwa ajili ya kukosa damu salama “ karne hii hatutakiwi kupoteza watu kwa ajili yakukosa damu alisema Issa na kuongeza tumsaidie ndugu yetu wa damu salama ili aweze kuwa na damu yakutosha katika benki ya damu”
Awali akijitambulisha mbele ya mkuu wa mkoa Meneja wa kituo cha damu salama kanda ya ziwa Fedrick Venance alielezea changamoto zinazo kikumba kituo kwa sasa kuwa ni pamoja na upungufu wa damu, alisema kwa hivi sasa kituo cha damu salama hadi kufikia tarehe 18.12.2014 kilikuwa na damu salama chupa 300 pekee huku kikiwa na upungufu wa chupa 77700 ambazo ndio hitaji kamili la wananchi wa kanda ya ziwa “Mhe mkuu wa mkoa zipo changamoto kadhaa ikiwapo ya uhaba wa damu salama kwa kiwango kinachotakiwa, kwakuwa wengi tunao wategemea katika suala la uchangiaji damu ni wanafunzi ambao kwa hivi sasa wapo likizo hivyo kufanya kituo kupungukiwa na damu. Alisema menejaVenance.
Majibu hayo yalifuatia swali aliloliuza mkuu wa mkoa akitaka kujua hali ya ukusanyaji damu ilivyo kwa sasa kwa kanda ya ziwa.
Mikoa ya kanda ya ziwa inayoundwa na Mwanza, Shinyanga, Mara, Kagera, Simiyu, na Geita ndio kwa kiasi kikubwa hutegemea kituo hicho japo wapo wananchi wengine ambao hufika kwa ajili yakupata damu salama kutoka maeneo mengine ya nchi.
Kukosekana kwa damu inaelezwa kuwa ni tatizo kubwa kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano, wakina mama wajawazito wakati wa kujifungua, wazee na watu wengine ambao hupata ajali na kutokwa na damu nyingi mwilini.
Kwa upande mwingine Venance amesema, zipo jitihada zinazo endelea kuchukuliwa kwa ajili kuboresha hali ya damu salama kwa mikoa ya kanda ya ziwa ikiwapo, kuanzishwa kwa kituo cha kukusanyia damu salama kwa mkoa wa Mara kuanzia mwezi  Januari na Mkoa wa Simiyu kuanzia mwezi Februari mwakani.
Hata hivyo wakati wakikao hicho mkuu wa mkoa aliwaambia watendaji hao kwamba, kila mmoja aliyewekwa katika eneo hili anatosha na ndio maana yupo hapo alipo, na kuwaonya kuacha kutegemea kila kitu makao makuu ya taasisi husika “najua tumefanya vizuri kwenye baadhi ya sekta lakini jambo hapa sio kufanya vizuri  suala nikwa jinsi tunaweza kuya maintain, sasa nimekuja kuwakumbusha kwamba tunatakiwa kuyasimamia vizuri maeneo yetu ili tusidondoke” alisema Mulongo.
Huu ni muendelezo wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika kufahamiana na wadau mbali mbali wa maendeleo katika mkoa wa Mwanza ambapo zamu hii ilikuwa kwa ajili yakukutana na taasisi za umma zilizopo mkoani humo.
Axact

Post A Comment: