KITANZI TAYARI KWA KUNYONGA.
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Tanzania imesema hadi kufikia Februari mwaka huu watanzania 177 wamefungwa katika magereza nchini China, huku miongoni mwao 15 wakiwa wamehukumiwa kunyongwa kutokana na makosa ya dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya hiyo, John Haule alisema watanzania hao bado hawajanyongwa kutokana na serikali ya China kuthamini ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na China na huenda wakabadilishiwa kifungo na kufungwa kifungo cha maisha jela badala ya Kunyongwa.

Haule amesema serikali ya Tanzania itahakikisha inadumisha ushirikiano na China kwa lengo la kupatikana kwa fursa za kiuchumi na kwamba tayari serikali ya China imetoa vifaa kwa Tanzania kwa ajili ya kugundua watu wanaosafirisha dawa za kulevya katika viwanja vya ndege.

Axact

Post A Comment: