Pichani ni Bibi Sarah Kibonde Msika, aktika Semina iliyofanyika katika chuo cha Fedha TIA tawi la Mwanza
kwa ajili ya Semina ya Ufahamu juu ya SSRA.
JESHI la POlisi mkoa wa Mwanza wamelalamikia kuhamishwa hamishwa kwenye mifuko ya hifadhi za jamii na kufanya michango yao mingine  kutoonekana katika kuchangia kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.
Malalamiko hayo yalitolewa jana na baadhi polisi walioshiriki katik semin ya siku moja iliyoandaliwa na Mamlaka ya usimamizi na Udhibiti wa Mifuko y Hifadhi za Jamii (SSRA) iliyohusu umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi za jamii.
Akiongea  kwa jazba katika semina, Martin Nkinga alisema wamekuwa wakihamishwa kutoka PSPF kwenda NSSF huku michango yao ikikwama njiani bila kufikishwa kwenye mfuko husika na hivyo kuwasabishia kero ya kufuatilia kila wakati bila mafanikio.
Wakati hayo yakijiri, Mfuko wa hifadhi ya Jamii wa (NSSF) na ule wa Bima ya Afya (NHIF) umezidi kuonyooshewa vidole na wadau wao mbele ya Mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya hifadhi ya jamii katika semina za wadau zinazoendelea jijini humo
Askari wakifatilia kwa makini Semina hiyo.
Wakiongea kwa uchungu askari Polisi hao Mwanza mbele ya Maafisa wa SSRA hapo jana wamesema,”’ ‘ NSSF imekuwa kero kubwa kwa wateja wake ikilinganishwa na mifuko mingine ya hifadhi ya jamii kwani mfuko huo mbali ya kuwa na Vitega uchumi vingi bado wanachama wao wameendelea kuwa wa hadhi ya chini zaidi”,alisena na kuongeza.
“Inashangaza kuona mtu umechangia sawa sawa na mwingine katika muda unaolingana kazini lakini mwisho wa kustaafu unakuta sisi wa NSSF tunapata mafao kiduuuchu sana ikilinganishwa na mwalimu au mtumishi mwingine aliyekuwa akichangia katika mifuko mingine” alisema mmoja wa polisi hao.
Huku Mkaguzi msaidizi wa Polisi Msangi yeye kiliochake aki kipeleka kwenye mfuku wa bima ya afya, (NHIF), kwamba hivi sasa wamekuwa na masharti magumu kwa wanachama kana kwamba matibabu wanayo yapata niya bure kumbe wanachangia mishahara yao, “Haiwezekani mtegemezi mtu amemuandika katika orodha ya wategemezi lakini inapofika wakati mtu huyo ameugua eti hatambuliki kwakuwa tuu jina lililokuwa kwenye kitambulisho na lile la muajiriwa havirandani wakati mimi nakatwa mshahara wangu tena bila yakuulizwa, huu ni unyanyasaji wa hali ya juu sana”.
Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa SSRA, bibi Sarah Kibonde Msika akitoa majibu kwa wadau hao alisema, “ Ni dhahiri kwamba zipo changa moto kadha wa kadha kwenye mifuko hii na sio rahisi kuzimaliza kwa wakati mmoja lililopo ni kwenda nazo taratibu na muda utafika, kama sio kuzimaliza basi tutazipunguza kwa kiwango kitakacho leta tija kwa wanachama.
Awali akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa watu kujiunga na Mifuko ya hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Jeshi la Polisi katika mkoa wa Mwanza alisema, kujinga na mfuko wa hifadhi ya jamii sio kujitabiria mabaya bali kujiweka tayari kwa wakati wa badae “ Kwa hivi sasa wengi wetu tunajiona tunanguvu nyingi za kutuwezesha kukimbia huku na huko kwa ajili yakujitafutia riziki ni vema, tukatumia kama wakati wa kujiwekea akiba ya badae” alisema Kibonde na kuongeza.. “ Mimi hapa kama mfano wa kuigwa nimejiunga na mifuko miwili mmoja ukiwa ni wa lazima na mwingine wa hiayari ambayo siku moja itanisaidia hata kusomesha watoto wangu alisema Bibi Kibonde.
SSRA walio anzishwa kwa Mujibu wa Sheria namba 8 ya Mwaka 2008hivi sasa wanaendelea na kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii katika mkoa wa Mwanza ambapo hapo kesho viongozi wa shirikisho la wafanyakazi katika Mkoa wa Mwanza watapatiwa elimu hiyo kwenye ukumbi wa Walimu uliopo kirumba.
Kwa mujibu wa SSRA hadi hivi sasa ni watanzania wapatao Mil.1.8 tu ndio walio jiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii, wakati nguvu kazi yenye uwezo wa kuzalisha ni mil.22, suala ambalo linawalazimu SSRA kujizatiti na kutoa Elimu kwa umma hivi sasa, ambapo hapo jana walitoa elimu kwa Watumishi wa Serikali ya Mkoa na hivi leo wametoa elimu hiyo kwa Askari Polisi pamoja na wanafunzi wa Chuo usimamizi wa Fedha nchini TIA.
Koplo Kelema akitoa kilio chake mbele ya Maafisa wa SSRA.

Liberatus Chonya, Afisa Uhusiano wa SSRA akinukuu mambo muhimu katika Semina hiyo.

Mmoja ya walimu wa TIA Tawi la Mwanza akitoa maelekezo kwa washiriki kabla ya Semina kuanza.

Maafisa wa Polisiwakisikiliza kwa makini Semina hiyo kutoka SSRA.

Hapa darasa linaendelea kwa wanasemina kumsikiliza mtoa mada kwa umakini wa hali ya Juu.


Tungependa kufahamu upi ni Mfuko bora wa Hifadhi ya Jamii kuliko mwingine, Ni baaadhi ya maswali yaliyo ibuka


Semina hiyo iliwahusisha askari wa Jinsia zote. Pichani ni Msaisizi wa Polisi Msangi  mkuu wa kituo cha Polisi akitoa ushauri katika semina hiyo.
 
 
Axact

Post A Comment: