JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO






(TAARIFA KWA UMMA)

WITO WA KUWASILISHA MUHTASARI WA MADA (ABSTRACT) KWA AJILI YA KONGAMANO LA KITAIFA LA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LITAKALOFANYIKA MOROGORO 6/03/2015
Tarehe 8 Machi, 2015 Tanzania itaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambayo itaadhimishwa kitaifa mkoa wa Morogoro. Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake mwaka 2015 ni “Usawa kwa Wanawake ni Maendeleo ya Haraka kwa Wote”.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, itaadhimisha siku hiyo kwa kuandaa kongamano la kitaifa litakalofanyika tarehe 6/03/2015 mkoani Morogoro sanjari na wiki ya maonesho ya wadau mbalimbali yatakayozinduliwa tarehe 03/03/2015 na kufikia kilele  chake tarehe 8/03/2015. Lengo kuu la kongamano ni kujenga jukwaa la majadiliano ya kina kuhusu masuala ya maendeleo ya wanawake na usawa wa kijinsia.

 Mada kuu nne zimependekezwa kuwasilishwa katika maeneo yafuatayo:
1.     Ukatili wa kijinsia (intimate partner violence- Ukatili katika mahusiano)
2.     Haki za wanawake/binadamu na mchango wa wanaume katika utetetezi wa haki za wanawake (Kwa mfano, ubakaji, ukatili kwa watoto/ wasichana)
3.     Hali ya Mtoto wa Kike (mf. Ndoa za utotoni)
4.     Ajira salama na haki katika ajira,
5.     Tathimini ya sheria na sera (dawati la jisia na polisi) na
6.     Majadiliano ( panel discussion) kuhusu uwezeshaji wa wanawake kiuchumi.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto inakaribisha mwanajamii yeyote aliyetayari kuandaa mada katika maeneo yaliyotajwa hapo juu, awasilishe muhtasari wa mada yake (ikisiri, abstract) yenye maneno kati ya 300 na 500 kwa ajili ya maandalizi ya kongamano hili muhimu. Siku ya mwisho ya kuwasilisha maelezo hayo (abstract) ni tarehe 20/01/2015.

Waandishi ambao muhtasari wa mada zao utakubaliwa watafahamishwa tarehe 20/01/2015 na watashirikishwa katika maandalizi ya mada kamili tarehe 31/01/2015.

Maelezo ya mada (abstract) yatumwe kwa:

(i)  Elizabeth Makawa: e_palelamakawa@yahoo.com – Simu No. 0655 975478

(ii) Dinah Enock: edinnah@yahoo.com – Simu No. 0766 070376

(iii) Judy Kizenga: kizengajudy@yahoo.com  - Simu No. 0754 564414


Tangazo hili limetolewa na
Anna T. Maembe
Katibu Mkuu
05/01/2015
Axact

Post A Comment: