Na Afisa habari RS-  Mwanza

MKUU WA WILAYA YA SENGEREMA MH. ZAINAB  TERACK,  AKIHUTUBIA KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAJI  KIMKOA KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA MWANZA WILAYANI SENGEREMA.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo amewataka wahandisi wa miradi ya Maji katika  Mkoa na wale wa  Halmashauri na miji midogo mkoani hapa kusimamia vizuri miradi ya maji na kwamba fedha zitakazotumika kwenye miradi hiyo zitumike vizuri ilikusaidia kukamilika  katika  viwango vinavyotakiwa.

Akizungumza kwa kwenye kilele cha maji  mkoani hapa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Magesa Mulongo, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Zaibabu Terack kwenye  sherehe za kilele cha maji zilizofanyika Wilaya ya Sengerema, Mulongo alisema kuwa miradi ya maji Mwanza inaweza kukamilika kwa wakati kama fedha za miradi hiyo zitatumika vizuri.

Alisema kazi ya kusimamia miradi hiyo inapaswa kufanywa na wakandarasi wa Halmashauri na miji midogo ambayo inapitiwa na miradi hiyo na kwamba kama fedha za miradi zitatumika kinyume Mwanza itaendelea kuwa na tatizo la maji.

Katibu Tawala msaidizi maji, Wariba Sanya
akitoa taarifa ya hali ya maji na miradi itakayo
Tekelezwa Mkoani Mwanza.
“Naomba niwaombe Wakandarasi wa maji kutoka Halmashauri zote za Mwanza pamoja na miji midogo ambayo inapitiwa na miradi ya maji isimamie vizuri miradi hiyo.Nataka kuona fedha za miradi zinatumika vizuri na miradi yote inatekelezwa kwa wakati,”alisema Mulongo na kuongeza:

“Kama tutakwenda kinyume na matumizi ya fedha za miradi ya maji tutaendelea kuwa na tatizo la maji na kero za maji ambazo zinawakabili wananchi zitaendelea, hivyo sitakubali kuona wananchi wanateseka kwa kukosa maji wakati Serikali yao inawajali kwa kuwaletea miradi ya maji.”

Akisoma taarifa ya miradi ya maji, Katibu tawala msaidizi maji Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Warioba Sanya, alisema Serikali imewekeza Sh.84.46 bilioni  kwa ajili ya miradi ya Maji  ya mkoa wa Mwanza  kupitia mapango wa maji wa (WSDP).

“Mwanza tunaishukuru Serikali, kwani licha ya kutupa miradi mbalimbali ya maji Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maji vijijini 217 kati ya hiyo miradi 140 imekamilika sawa na asilimia 65 na kwamba miradi iliyobaki itakamilika ifikapo mwezi juni mwaka huu,”alisema Sanya.

Mkoa wa mwanza kwa hivi sasa unawapatia maji wananchi kwa asilimia 61.

 
Axact

Post A Comment: