Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amezindua Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekouture inayoundwa na wajumbe wapatao 15, huku akiibebesha jukumu lakuhakikisha hospitali hiyo inachana na mfumo wa ukusanyaji mapato wa kawaida na badala yake watumie mfumo wa kieletroniki
 
 
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella, akimkabidhi mmoja  ya wajumbe wa Bodi Ndungu Christopher Mwita Gachuma Miongozo ya namna yakuendesha Hospitali za Rufaa
Mkuu huyo wa mkoa amesema pamoja na Hospitali hiyo kuongeza mapato yake lakini bado kiasi hicho kinacho kusanywa hakingani na hadhi ya hospitali hiyo, kwani kwa mujibu wa takwimu za makadirio ya watu huo unakadiriwa kuwa na watu wapatao Mil.3.5 kwa sasa.

 
“Ni kweli kuwa tumeongeza makusanyo yetu kutoka Mil. 500 hadi kufikia Bil. 1 kwa mwaka, lakini kwa idadi yetu ya watu tulipaswa kufikia Bil.2.5 hadi Bil. 3 kwa mwaka”, alisema Mongella na kuendelea kuitaka bodi hiyo isimame imara kuhakikisha malengo hayo ya makusanyo yanafikiwa.

Mongella pia katika hotuba yake, amesema mpango uliopo kwa sasa nikujenga jengo la Ghorofa ili kuimarisha na kuongeza shughuli zautoaji huduma za afya katika hosptali hiyo inayotegemewa hata na baadhi ya mikoa ya kanda ya ziwa, huku akiahidi kuomba kubadilishiwa matumizi   kiasi cha fedha Mil. 460 zilizokuwa zimetolewa na hazina kuelekezwa katika ujenzi wa jengo la Ghorofa tatu linalo tarajia kujengwa katika Hospitali hiyo.

Awali Mganga mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Leonard Subi, akimkaribisha  mkuu wa mkoa kuzindua bodi hiyo, alisema mahitaji halisi ya watumishi wa Idara afya katika mkoa huo ni watumishi 7,582 lakini watumishi waliokuwepo kabla ya zoezi la uhakiki ilikuwa ni watumishi 3,552 sawa na asilimia 48 ya mahitaji yote ya watumishi, aidha Subi amesema kuwa mkoa wa Mwanza kwa hivi sasa hauna tishio lolote lile la Magonjwa ya Mlipuko.

 

Akitoa taarifa ya Hospitali hiyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Onesmo Rwakyendera, amesema hospitali hiyo kwa sasa imeendelea kutekeleza azma ya Serikali ya awamu ya tano ambayo imelenga kuwahudumia watanzania wote katika kuboresha maisha yao ikiwa ni pamoja na huduma za afya.

Wajumbe wa Bodi na baadhi ya Waalikwa wakimsikiliza kwa Makini Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, John Mongella, wakati wa Uzinduzi wa Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekouture
 
“Kupitia juhudi hizo hospitali imeweza kuwa na mafanikio mbalimbali kama vile uwepo wa dawa muhimu kwa asilimia 80” amesema Rwakyendera, aidha  amesema katika kufikia mafanikio chanya kwa kipindi cha miaka mitatu Hospitali iliwahudumia Jumla ya wagonjwa wa nje wapatao 512,548.

Picha ya Pamoja kati ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongella na Wajumbe wapya wa Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekouture.
Wajumbe watakao simamia hospitali hiyo iliyo anza mwaka 1994 ni pamoja na Mganga Mkuu wa Mkoa Mwanza Dkt. Leonard Subi, Mganga Mfawidhi wa Hospitali Dkt. Onesmo Rwakyendera, Bwana Christopher Mwita Gachuma, Bibi. Asia Kapande na Shekh Hassan Kabeke, wengine ni Bwana Joseph Kahungwa, Bibi Elicia Yinza, Bwana Kaviti Mushi, Dr. Richard Mbwambo, Bibi,  Victoria Ndalahwa, Mhe. Serapian Matiku, Dr. Agnes Mwita, Bwana Charles Misango, Bwana . H.V Shah, Mganga Mkuu Halmashauri Ya, Manispaa Ilemela
Axact

Post A Comment: