Serikali mkoani Mwanza imeitaka jamii kote nchini kuwapeleka watoto wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) shule, badala ya kuwanyanyapaa na baadhi kuwaficha ndani na kisha kufifisha ndoto zao za maisha.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Leonard Subi, akifungua kambi Siku tano Jiji Mwanza, kushoto kwake Mkurugeni wa (AGPAHI) Dkt. Sekela Mwakyusa.
Akizungumza katika kambi ya siku tano mjini hapa, mganga mkuu wa mkoa wa Mwanza Dk Leonard Subi kwenye ufunguzi wa kambi hiyo iliyotayarishwa  na taasisi isokuwa ya serikali ya ‘Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) na kuwakutanisha watoto wanaoishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka mikoa ya Tanga, Simiyu na Mara, Dkt. Subi amehimiza umuhimu wa malezi kwa watoto
“Naamini kila mtoto ana ndoto zake  katika maisha lakini zaidi sana katika kusoma na vipaji vingine endapo tu akisaidiwa kwa kujengewa mazingira rafiki ya kumwezesha kupata elimu bila bugudha, alisema Dkt..Subi na kuongeza “Kila mtoto ana haki ya kuishi, apate afya bora”.
Ukumbi ulivyokuwa umepambwa na Wanasemina wakifatilia kwa umakini mkubwa wakati wa Ufunguzi wa kambi hiyo ya siku tano Jijini Mwanza.
Naye , Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo ya AGPAHI, Dr. Sekela Mwakyusa, alisema jukumu la taasisi hiyo zaidi ni kutoa usaidizi kwa vituo vya afya vilivyopo katika serikali kuu pamoja na serikali za mitaa kwenye huduma za afya hususan katika maswala ya VVU na UKIMWI, sambamba na huduma za afya ya uzazi kwa mama na  mtoto.
Mwakyusa alifafanua kuwa tangu taasisi hiyo ilipoanzishwa mwaka 2011, imekuwa ikifanya kazi katika mikoa miwili ya Shinyanga na Simiyu. Lakini toka mwezi Oktoba mwaka 2016 2017 taasisi imekuwa na kutoa huduma katika mikoa sita ikiwemo Mwanza, Mara, Geita na Tanga.
Amefafanua kwamba hadi kufikia mwezi Machi 2017 walikuwa wamewafikia watu wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi wapatao 189,000 na kati ya hao 8,620 ni watoto wadogo ambao ndio nguvu kazi ya taifa lijalo.
“Kwetu kama Taasisi ni kutoa huduma shirikishi zaidi na kuhakikisha kwamba tunaondoa maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa watoto na pia tunabaki na kizazi ambacho hakina UKIMWI.” Alisema
Ameongeza kwamba tayari wamefikia asilimia tano ya watu wote ambao wanawahudumia wakiwa ni watoto ingawaje lengo ni kufikia angalau asilimia kumi ya watoto na hivyo wanafanya jitihada zote kuweza kuwapata wale watoto kwenye vituo vya afya na pia kwenye jamii.
Hata hivyo, AGPAHI inajukumu la kuwafuatilia afya za akina mama wakiwa bado na uja uzito hadi wanapozaliwa kuhakikisha kwamba wanapata huduma zote zinazostahili toka tu pale mama anapo pata ujauzito.
“Wapo wale watoto ambao kwa bahati mbaya mama hakuweza kutabulika kwamba ana matatizo na tunawakuta mara nyingi tukiwa tumeenda kufanya kampeni za upimaji au kwenye vituo vya afya wanakuja na tunawatambua.” alisema Mwakyusa.
Aidha alitoa wito kwa jamii kuwa na ushirikiano kwani asilimia kubwa ya jamii  hasa akina mama hawana nafasi ya kufanya maamuzi kama vile kwenda kupata huduma za afya kwa wakati, huku wakiahidi kuweka kambi ingine katika mkoa wa Kagera itakayohusisha mikoa ya Mwanza, Geita na Shinyanga kwa lengo lakuzidisha uelewa kwa jamii juu ya masuala ya afya katika miezi ijayo
 
 

Picha ya Pamoja ni muhimu kwaajili yakuweka kumbukumbu, pichani Dkt. katikati, waliokaa akiwa katika picha ya pamoja mara baada yakufungua na kujionea maendeleo ya kambi
Axact

Post A Comment: