> Nibaada yakushindwa Marshrti.
Moja ya Mashine katika kiwanda hicho ambayo baadhi ya vifaa vyake vimenyofolewa.

Mtambo huu unatajwa ndio kwanza Tekinolojia yake inaingia Afrika lakini hapa kwetu ulifungwa miaka mingi iliyopita.


Mkuu wa mkoa wa Mwanza akiwa ameambatana na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama hapa wakifanya ukaguzi wa ndani ya Kiwanda hicho.

 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, ameamuru kufungwa kwa kiwanda cha Ngozi cha Mwanza ambacho kilibinafsishwa wakati wa zoezi la ubinafsishaji mwanzoni mwa miaka ya tisini  kufuatia utata uliogubika  umiliki halali  wa kiwanda hicho.
Hatua ya mkuu wa Mkoa inafuatia ziara yake aliyoifanya kiwandani hapo tarehe 10 Julai, 2017 na kuwaamuru wahusika kuwa na mpango kazi ambao ungeonesha kwa namna gani wataanza kazi ifikapo Januari, 2018, huku akiwataka wahusika wote ambao wanamaslahi na kiwanda hicho kuwepo kiwandani hapo ifikapo 20 Julai, 2017.
Kinyume na matarajio ya Mkuu wa Mkoa, alipowasili kiwandani akiwa ameambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo, majira ya saa 5.43 za asubuhi siku ya tarehe 20 Julai, 2017, alikuta hakuna maendeleo yoyote juu ya hatma ya kiwanda hicho na hata mpango kazi aliokuwa ameagiza hakuuona.
Kwaundani isome kupitia    www.mwanza.go.tz
Axact

Post A Comment: