Pichani Eng. Mussa Iyombe Katibu Mkuu OR- TAMISEMI  (kutoka Maktaba).
 
Serikali imeonya na kusema, walimu 381 na mafundi sanifu wa maabara 137 ambao mara baada ya maombi yao kupitishwa na kupangiwa kazi wanapaswa kuripoti katika vituo hivyo vya kazi walivyo pangiwa na  watakaochukua fedha na kisha kutoweka kwenye vituo vya kazi watachukuliwa hatua kali za kishesheria ikiwapo kufikishwa mahakamani.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhandisi Mussa E. Iyombe na kusambazwa kwenye vyombo vya habari na tovuti hii kufanikiwa kupata nakala yake imesema, wale wote waliopangiwa vituo hivyo vya kazi watatakiwa kuripoti katika vituo vyao kati ya tarehe 17 na 21 Julai, 2017.
Soma habari yote kupitia na majina ya wahusika  www.mwanza.go.tz

 
Axact

Post A Comment: