Articles by "afya"
Showing posts with label afya. Show all posts
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Seleman Jafo, akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa kuhusu ukarabati wa vituo 172 vya Afya nchini kote.
 
Serikali imepanga kukarabati vituo vya afya 172 kutokana na fedha kutoka Benki ya Dunia na Ubalozi wa Canada ambapo wametoa jumla ya Dolla za Kimarekani Mil 88 sambamba na Bil.12 fedha za kitanzania zilizovuka katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Watumishi mkoa wa Mwanza kuwezesha kituo cha damu salama kanda ziwa kuwa na damu yakutosha ili kuweza kukidhi mahitaji halisi yanayo fikia chupa za ujazo 78,000 kwa mwaka.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kuongeza kiwango cha wajawazito kujifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya  kutoka 68%-80% ifikapo desemba 2015, kuongeza  kiwango cha huduma baada ya kujifungua ndani ya siku 7 kutoka 21% mpaka 62% ifikapo  Decemba  2015, kuongeza kiwango cha watoto wanaozaliwa na kina mama wenye maambukizi ya VVU kutumia  ARV (prophylaxis) kutoka 45% to 65% ifikapo Decemba 2015 kuongeza namba ya vituo vinavyotoaa huduma ya IMCI kutoka 69%-80% ifikapo Desemba 2015, mbali ya mikakati hiyo vilevile mkoa umedhamiria Kuboresha utoaji wa taarifa kwa wakati kutoka 66%-100% ifikapo Decemba 2015.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Aagiza Shughuli za usafi zifanywe na Vikundi vidogo vidogo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo amekerwa na hali ya uchafu iliyopo katika mitaa ya Jiji la Mwanza na kuwaagiza  watendaji wa halmashauri hiyo  kuacha  kukaa ofisini na badala yake watoke na kwenda kuwasikiliza watu katika maeneo yao ya kibiashara. 
Mulongo ametoa kauli hiyo jijini Mwanza, mara baada yakufanya ziara yakutembelea maeneo yaliyotengwa  maalumu kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo Jijini humo na kukuta hali ya mazingira kiafya ikiwa hairidhishi.
 
Mkuu huyo wa mkoa akiwa ameambatana na kamati ya Ulinzi na usalama ya Mkoa alitembelea maeneo ya Makoroboi, Soko kuu, Sahara na Standi ya Nyegezi.




MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO AKISHANGAA UCHAFU ENEO LA SOKO KUU.
AKIWA KATIKA ENEO LA MAKOROBOI, HAPA VIJANA WA SHULE WAKICHAGUA NGUO ZA MTUMBA




"HAIKUBALIKI KATIKATI YA JIJI PAWE NA HALI YA UCHAFU KIASI HIKI"- MULONGO




UKARABATI WA VIBANDA KATIKA ENEO AMBALO LIMEZUIWA KUFANYA BIASHARA NDOGO NDOGO

ZAWADI NAZO HAZIKUKOSEKANA (PICHA ZOTE NA OFISI YA MKUU WA MKOA)

MKUU WA WILAYA YA NYAMAGANA BARAKA KONISAGA AKITOA MAELEZO MBELE YA MKUU WA MKOA WAKATI WA ZIARA HIYO


ENEO LILILOKUWA NYUMBA YA NHC AMBAPO MKUU HUYO WA MKOA AMETOA SIKU HADI KUFIKIA TAREHE 30 DESEMBA LIWE LIMEENDELEZWA.


KWA MBALI MKUU WA MKOA AKITAZAMA JENGO LA MSIKITI WA JAMII YA WAHINDU AMBAPO WAFANYABIASHARA WAMEKUWA AKIFANYA BAISHARA BILA YA IDHINI YA SERIKALI.


HUU NDIO UCHAFU UNAO NYOOSHEWA KIDOLE NA MKUU WA MKOA WA MWANZA KATIKA ENEO LA STANDI YA TAX JIJINI HUMO.

KAZI NI UHAI KWA KILA BINADAMU, ASIYEFANYA KAZI NA ASILE(PICHA NA OFISI YA RC MWANZA.)

TUPO KAZINI WAJASIRIAMALI KATIKA ENEO LA MTAA WA SOKONI WAKIUZA SAMAKI AINA YA NEMBE.

MKUU WA MKOA ALIYE NYANYUA MWAMVULI KUMSIKILIZA BIBI ASIA RASHIDI ENEO LA SOKO KUU WAKATI WA ZIARA HIYO.(PICHA NA OFISI YA RC MWANZA)

MKUU WA MKOA AKISHUHUDIA WAKINA MAMA WAUZA SAMAKI KATIKA MTAA WA SOKONI.

 Aidha katika hatua nyingine ameuagiza uongozi wa jiji hilo kuhakikisha wana viainisha vikundi vidogo vidogo vinavyo undwa na vijana pamoja na kina mama ili viweze kukabidhiwa jukumu la kutunza mazingira badala ya kazi hiyo kuachiwa mawakala wa usafi ambao kwa namna moja au nyingine wameonekana kulemewa na jukumu hilo .

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
 Taasisi ya Benjamin W. Mkapa HIV/AIDS (BMAF) iliyoanzishwa mwaka 2006 na Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Benjamin W. Mkapa, imekuwa mstari wa mbele kuchangia juhudi za Serikali kupitia miradi mbalimbali inayolenga kuimarisha huduma za afya, hususan katika maeneo ya vijijini na yenye mazingira magumu. Mradi mmojawapo unaotekelezwa na Taasisi ni wa “Mkapa Fellows” wa miaka mitano (2013- 2017) ambao unafikia Halmashauri 15 zilizopo katika mikoa ya Shinyanga, Kagera, Simiyu, Rukwa na Zanzibar.

Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.


HUU NDIO MNARA ULIOZINDULIWA HUKO SENGEREMA MKOANI MWANZA KWA MADHUMUNI
YAKUPINGA NA KUTOKOMEZA KABISA MAUWAJI YA ALBINO HAPA NCHINI.

Mnara huu wa kwanza wa kihistoria dunia umesimikwa katika kipita shoto kikuu kinachounganisha barabara zinazoelekea mkoa wa Geita, Kahama, Bukoba mkoani Kagera na Kamanga mkoani Mwanza, ukiwa umeorodheshwa majina takribani 72 ya watu wenye albinism waliouawa.
Kabla ya uzinduzi huo maandamano yalifanyika yakihusisha wageni pamoja na wananchi wa wilaya ya Sengerema walio hamasika na mpango huo ulionuia kutokomeza kabisa mauaji hayo ya kinyama. 
Viongozi wa kada mbalimbali wilayani Sengerema wakiwa na Rais wa Under the Same Sun Bw. Peter Ash wakisoma majina ya watu wenye albinism waliouawa kwa matukio ya ushirikina.
Mnara uliozinduliwa unamwonyesha baba asiye na ulemavu wa ngozi akiwa amembeba mabegani mtoto wake mwenye albinism huku mama ambaye pia hana ulemavu wa ngozi akisaidia kumvika kofia mwanaye. Kumbe sasa hata baba na mama wasio na albinism katika mwonekano wa ngozi ya kawaida wanaweza kuzaa mtotomwenye albinism.
Pia Shirika hilo la Kimataifa la kutetea haki za watu wenye ulemavu wa ngoziduniani kupitia Taasisi yake ya Under the Same Sun limetoa tuzo ya kwanza duniani kwa vyombo vya habari 127 hapa nchini ikiwemo kampuni ya IPP MEDIA ambayo imejinyakulia ushindi mkubwa wa tuzo 5. Pichani Mwakilishi wa ITV Cosmas Makongo akitoka kupokea moja kati ya tuzo.

Ni tuzo ya kwanza duniani kwa vyombo habari na waandishi wake ambao wameibuka washindi kwa kuhamasika kufuatilia kwa ukaribu matukio mbalimbali yaliyojitokeza na kuyawasilisha kwa jamii.





Mwakilishi wa ITV Cosmas Makongo akipata mkono wa pongezi kutoka kwa Katibu Tawala wilaya ya Sengerema Alfred Kapole mara baada ya kupokea Tuzo kwa Kampuni yake ya IPP kupitia ITV kwa kutangaza bure habari na vipindi vilivyokuwa vikihamasisha kupungua kwa mauaji ya kinyama dhidi ya albinism hapa nchini.

Rais wa Under the Same Sun Peter Ash akitoa hotuba yake kwa jamii iliyofurika katika viwanja vya Telecenter mjini Sengerema. Huku akiwa na baadhi ya watu walioathirika  na matukio ya kinyama walio nusurika kuuawa wakipoteza baadhi ya viungo vyao. Kutoka kushoto ni Bi. Mariam ambaye alipoteza mikono yake kwa kukatwa mapanga na watu waliokuwa wakihitaji viungo vya albino kwaajili ya masuala ya ushirikina, mtoto Festo aliyekatwa kiganja cha mkono wa kulia na kukatwa kabisa mkono wake wa kushoto huku aking'olewa meno pamoja na Said Abdalah mkulima mkata mkaa aliyekatwa mkono wake wa kushoto kwa imani hizo hizo. Inasikitisha.

Wadau wa Taasisi ya Under the Same Sun Vick Ntetema (L) na Gamariel mboya (R).
Nao wazazi wenye watoto wenye albinism walifika eneo la tukio kupata elimu. Kutoka kushoto ni Daudi Nzila akiwa na mwanae Elikana na Mathayo Felician akiwa amempakata mwanae Faustin.
Mahudhurio yalikuwa makubwa huku huzuni ikitawala.
Wanahabari mstari wa mbele kunasa matukio.
Eneo lilifurika watu kiasi cha wengine kujikita pembezoni mwa barabara.
Mwanadada Mariam aliyekatwa mikono yake yote na wavamizi, aliwatoa machozi wengi kwa simulizi ya mkasa wake.

Mwalimu Peter akisoma risala ya Kikundi cha albinism Sengerema kwa mgeni rasmi.
Wananchi wakigawiwa vipeperushi na majarida ya Taasisi inayopambana na ukatili dhidi ya watu wenye albinism ya Under the Same Sun.
Elimu toka kwa majarida.
Wageni wadau wa Taasisi ya Under the Same Sun, ambapo kulia ni Bi. Maphordens Soto ambaye ni Mfamasia Bingwa wa kutengeneza losheni za kuwakinga albinism dhidi ya miale mikali ya mwanga wa jua inayo athiri ngozi zao.
Blogger G. Sengo.
Mnara huu wa kwanza wa kihistoria dunia umesimikwa katika kipita shoto kikuu kinachounganisha barabara zinazoelekea mkoa wa Geita, Kahama, Bukoba mkoani Kagera na Kamanga mkoani Mwanza, ukiwa umeorodheshwa majina takribani 72 ya watu wenye albinism waliouawa.
Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Katibu Mkuu wa TUCTA Nicolous Mugaya akizungumza na waandishi wa habari nje Ukumbi mara
baada yakufungua Semina hiyo.
Mamlaka ya Mifuko ya hifadhi ya Jamii na udhibiti SSRA, wameendelea na utoaji wa Semina kwa makundi tofauti tofauti safari hii wakitoa semina hiyo kwa Viongozi wa Vyma vya wafanyakazi katika Mkoa wa Mwanza.

Akifungua mkutano huo hii leo Katibu Mkuu wa TUCTA Taifa Nicolous Mugaya amesema lengo kuu la vyama vyama vya wafanyakazi ni kuhakikisha mfanyakazi anaboreshewa maisha kwa kumpatia mafao mazuri lakini pia mazingira mazuri yakufanyia kazi.

 Mugaya amesema, wao kama vyama vya wafanyakazi lazima wafute na kuiga kwenye nchi ambazo zimekuwa na mifuko michache na hivyo kufanya mafao kuwa bora huku akitolea mfano wa nchi ya Kenya na Zambia. akaongeza kwamba Utaratibu wa kukokotoa mafao hivi sasa upo katika hatua za awali za mchakato na itafika wakati mafao yatakuwa yana kokotolewa kwa fomula moja.

Akizungumza katika semina hiyo mgaya amesema " Tunataka siku moja mifuko ya hifadhi ya Jamii inabaki kuwa miwili ambayo itakuwa na ushindani wa dhati na hivyo kufanya maslahi ya Mtumishi kuwa bora na kuleta tija" amesema na kuongeza kuwa,  kwa hivi sasa ni mifuko michache ndio  ambayo kwa kiasi Fulani imekuwa hailalamikiwi, hivyo kama vyama vya wafanyakazi wanajukumu la kuhakikisha maslahi yanaboreshwa.

Fatilia habari kwa Picha kwa zaidi na zaidi.......!!!!

Wafanyakazi wakiimba wimbo wa Mshikamano kabla yakuanza kwa Semina hiyo.

Nasaha za Mugaya wakati wa kufungua Semina hiyo ya Siku moja.

Hapa wakiwa katika picha ya Pamoja mara baada yakufungua Semina hiyo, iliyo fanyika katika Ukumbi wa CWT Mkoa wa Mwanza.


Darasa linaendelea na Umakini ni suala la Muhimu sana Bibi Sarah Kibonde Msika akitoa somo.

Tunanukuu yale ya Muhimu unayo tufundisha.

Lazima tuelewe manufaa ya hii mifuko inawigo mpana sana, kuna kitu kina itwa Multiply effects
 kutokana na uwekezaji.

Mshikamano sio kwa wanachama pekee bali pia viongozi wao.

Tunakupenda sana sana tuachie maoni yako basi ndugu.!!!




Kuni News Blog. Habari, matukio na uchambuzi wa makala.
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (wa nne kulia) akiwa na  Jenerali wa Magereza Tanzania John Minja (katikati)  wakimsiliza kwa makini Mnadhimu wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mmeta Manyara akijitambulisha. Kamishna Chato  ametembelea Makao Makuu ya Magereza ikiwa kni ziara ya siku sita nchini Tanzania.Wa tatu kulia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza John Yumbe, wa pili kulia ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Tebuho Nyambe na wa kwanza ni Mrakibu Msaidizi wa Magereza James Nkoloma wote kutoka Makao Makuu ya Magereza nchini Zambia.


Kamishna wa Magereza nchini Zambia yuko katika ziara ya siku sita nchini kufuatia mwaliko uliotolewa kwake na Kamishna Jenerali wa Magereza wa Tanzania John Minja mwezi Septemba mwaka, 2013 alipotembelea Magereza nchini Zambia. Ziara ya Kamishna Percy pamoja na maafisa wengine watatu ni kudumisha ushirikiano uliopo kwa muda mrefu baina ya nchi hizi mbili na magereza kwa ujumla. Akiwa nchini Tanzania Kamishna Percy atatembelea baadhi ya Magereza na Vyuo vya Mkoa wa Dare es salaam, Kilimanjaro na Arusha ili kujionea shughuli za urekebishaji wa wafungwa zinavyofanywa kwa vitendo na kuona maeneo ambayo taasisi hizi mbili zinaweza kubadilishana uzoefu.
 
Askari wa Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani (KMKGM) cha Ukonga jijini Dar es salaam wakionesha aina mbalimbali za mzoezi ya kujihami na kuanguka bila kuumia katika kukabiliana na hatari yoyote, mblele ya Kamishna wa Magereza nchini Zambia Percy Chato (hayupo pichani)

Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (mwenye suti) akikagua paredi maalum lililoandaliwa kwa heshima yake katika Chuo cha Maafisa wa Magereza Ukonga, Dar es salaam.
 
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (mwenye suti) akipokea salaam ya heshima kutoka kwa Paredi maalum (halipo pichani) lililoandaliwa maalum kwa jairi yake katika uwanja wa paredi wa Chuo Cha Maafisa wa Magereza Ukonga.Nyuma yake ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Dkt Juma Ali Malewa na mwenye nguo za kijani ni Kaimu Mkuu wa Chuo  Kamishna Msaidizi wa Magereza Erasmus Kundi
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato wa (pili kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa mmoja wa mafundi katika Karakana ya magari ya Magereza iliyoko Ukonga Dar es salaam, wa kwanza kulia ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Dkt Juma Ali Malewa.
: Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato (katikati) akifurahia kukaa katika moja ya samani zinazotengenezwa kiwandani Ukonga, kushoto ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza Tanzania, Dkt Juma Ali Malewa na kulia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza wa Zambia John Yumbe.
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato ( wa nne kushoto), akipokea taarifa fupi kutoka kwa mmoja wa maofisa  kiwandani Ukonga. Kamishna Percy alitembelea Kiwanda cha Magereza Ukonga, Dar es salaam kuona shughuliza za urekebishaji wa wafungwa zinavyofanyika.
Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato akisaini kitabu cha wageni Kiwandani Ukonga, wa pili kushoto ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Tanzania Dkt Juma Ali Malewa
 Kamishna wa Magereza nchini Zambia  Percy Chato ( wa nne kushoto), akipokea taarifa fupi kutoka kwa mmoja wa maofisa  kiwandani Ukonga. Kamishna Percy alitembelea Kiwanda cha Magereza Ukonga, Dar es salaam kuona shughuliza za urekebishaji wa wafungwa zinavyofanyika.
 
PICHA NA HABARI KNY. YA JESHI LA MAGEREZA KITENGO CHA HABARI.