Kufuatia  kuzingirwa na wanamgambo wenye silaha wako kwenye hatari ya kupata maradhi yatokanayo na maji machafu ikiwa hawatapata msaada wa haraka wa kibinadamu, lilionya Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya (KRCS) siku ya Jumanne (tarehe 26 Novemba).

Wanajeshi wakijiandaa kwenda kuwaokoa watu walio zingirwa.
"Hali ya kiafya inaweza ikawa mbaya zaidi kutokana na uwezekano mdogo wa kupata maji, huduma ya matibabu na chakula," alisema meneja wa KRCS kwa eneo la North Rift, Patrick Nyongesa, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya. "Wahanga hao, hasa watoto na wazee wasiojiweza, wana hatari ya kupatwa na homa ya mapafu na maradhi yatokanayo na maji kama vile kipindupindu kwa sababu ya uchafu."

Shirika la KRCS limesambaza msaada wa chakula na mengine iliyochangwa na serikali ya Kaunti ya Turkana kwa familia zilizookolewa.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa huko, Lucas Ngasike, hali ya utulivu imerejea kwenye eneo hilo lakini licha ya kuwepo kwa jeshi, kuna wasiwasi sana.

Aliiambia Sabahi kwamba kulikuwa na hofu kwamba watu wa jamii ya Pokot nchini Uganda walikuwa wanapanga kuivamia jamii ya Turkana na kuwatoa kwenye eneo hilo, na matokeo yake jamii ya Turkana wanajihami kwa silaha.

Lakini msemaji wa polisi ya Kenya, Zipporah Gatiria Mboroki, alisema mzingiro wa kijiji hicho ulimalizika pale wazee wa huko walipoingilia kati na kuwashawishi wanamgambo kujiondoa.

"Utulivu umerejea na barabara imefunguliwa na hakuna mtu aliyejeruhiwa," alisema na kuongeza kwamba polisi bado walikuwa wanaondosha miti iliyowekwa njiani kuzuia kijiji hicho kufikika.

Shirika la KRCS limeitolea wito serikali ya Kenya kuunga mkono suluhisho endelevu kwa mzozo huo kati ya jamii hizo mbili, ikiashiria kwamba mgogoro huo si jambo jipya, kiliripoti kituo cha Capital FM cha Kenya.

 
Axact

Post A Comment: