Mshambuliaji wa TP Mazembe, Mbwana Samata.

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samata alifunga bao pekee na kuiongoza TP Mazembe ya DR Congo kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, huku mabingwa watetezi Al Ahly wakiaga mashindano kwa kuchapwa 3-2 nyumbani na Al Ahly Benghazi ya Libya.

Samata aliingia akitokea benchi na kufunga bao hilo dakika ya 68 na kuipa ushindi wa 1-0 dhidi ya Sewe Sport ya Ivory Coast na kusonga mbele kwa sheria ya bao la ugenini baada ya matokeo ya jumla kuwa 2-2 baada ya awali Mazembe kutunguliwa mabao 2-1 jijini Abidjan.

Samata ndiye aliyefunga bao la kufutia machozi Abidjan wiki moja iliyopita pamoja na bao pekee la Jumamosi jijini Lumbumbashi. Sasa Mazembe itasubiri kujua wapinzani wake katika droo itakayopangwa Aprili 29 mjini Cairo.

Nao mabingwa watetezi Al Ahly ya Misri wameaga mashindano hayo baada ya kuchapwa mabao 3-2 nyumbani na Al Ahly Benghazi katika pambano la marudiano lililopigwa mwishoni mwa wiki jijini Alexandria.

Kipigo hicho kinaifanya Al Ahly iondolewe mashindano hayo kwa jumla ya mabao 4-2, baada ya mechi ya kwanza iliyopigwa jijini Tunis, Tunisia ambako Benghazi wanatumia kama uwanja wa nyumbani kutokana na machafuko kushinda 1-0.

Kutoka: Mwananchi.
Axact

Post A Comment: