MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO AKITOA MAELEKEZO KWA WATENDAJI.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mgesa Mulongo, amewaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha Ujenzi wa  vyumba vya Maabara unakamilika ifikapo Novemba 30 na kinyume na hapo basi itabidi kila mmoja awajibike.

Mulongo ameyasema hayo katika siku yake ya kwanza kikazi mkoani humo alipo wasili kwa ajili ya  kuripoti tangu alipoteuliwa na Rais kushika wadhifa huo Novemba 5 mwaka huu.

Amesema kwakuwa wenyeviti wa mabaraza ya madiwani wote walisha onesha nia kwa kusukuma na kuhimiza ujenzi huo wa maabara na tayari kamati za fedha zilikwisha idhinisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara lililopo kwa sasa ni kuhakikisha mamlaka zinazo takiwa kupeleka fedha kwa ajili ya ujenzi  zitekeleze majukumu yake huku akiwakazia sauti wakurugenzi wa halmashauri.

Amesema amekuja kuwaomba licha ya kwamba ni mgeni katika mkoa huo, huku akimuagiza Katibu Tawala Mkoa kuhakikisha kuwa kila siku taarifa ya ujenzi wa maabara zinawasilishwa mezani kwake na hatua zilizo fikiwa “Nimekuja kuwaomba na nazidi kuwaomba nazidi kuwaomba tena leo natumia nafasi hii na ugeni wangu huu kamalizeni maabara,  alisema na kuongeza kuwa ataendelea kulifatilia suala hilo kwa kufanya Monitoring yeye mwenyewe.

Aidha amehimiza kuwa wakurugenzi wahakikishe taarifa hizo zinasainiwa na wakurugenzi wenyewe na sio watumishi wengine wanao kaimu ofisi za wakurugenzi.
Ameawaambia wakuu wa Wilaya ikifika tarehe 30 Novemba, kama hakuna maabara hajui ni hatua zipi zitakazo fuata kwakuwa  wakati maelekezo yanatolewa na Rais wakuu hao wawilaya walikuwepo na kila mmoja alisaini moyoni mwake kuhusiana na ujenzi wa maabara hizo.
Mkuu huyo wa Mkoa alikuwa katika siku yake ya kwanza mkoani humo
Axact

Post A Comment: