TUPO TAYARI KUJA KUWEKEZA KATIKA NCHI YA TANZANIA NA HUSUSAN KATIKA MKOA WA MWANZA, NDIVYO ANAVYO ONEKANA KUSEMA SON YOUNG SOO, KIONGOZI WA MSAFARA KWA MKUU WA MKOA WA MWANZA.

 FURSA NI JAMBO MOJA UTAYARI WA WANANCHI WETU NI JAMBO JINGINE, NIWAOMBE WANANCHI KWA UJUMLA WAO WAWE TAYARI KUSHIKIANA NA WAWEKEZAJI. NAIBU WAZIRI WA ARDHI NA MBUNGE WA ILEMELA, DKT. ANGELINA MABULA.
 MKUU WA MKOA WA MWANZA JOHN MONGELLA AKIMUELEKEZA JAMBO MKURUGENZI WA MANISPAA YA ILEMELA JUU UJUMBE KUTOKA KOREA KUSINI.
 MKUU WA MKOA WA MWANZA JOHN MONGELLA  MARA BAADA YAKUFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE KUTOKA NCHINI KOREA KUSINI.



 TUNAPOSEMA, MWANZA KAZI NA MAENDELEO NDIO HII TAFSIRI YAKE, KOREA KUSINI WAMEKUJA, KWASABABU YA AMANI NA UTULIVU WA NCHI YETU, RC MONGELLA
(PICHA ZOTE NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA  MWANZA),

·        Awaahidi ushirikiano nao..

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amepokea ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini Korea Kusini, wenye niya yakuwekeza katika mkoa wa Mwanza ukiwa na ujumbe wa watu kumi na watano nakufanya nao mazungumzo mapema katika Ofisi yake kabla yakuendelea na ziara yao katika Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.

Katika mazungumzo yao yaliyodumu saa 1:33, Mkuu wa Mkoa amewahakikishia utayari wa mkoa wa Mwanza kuwapokea wawekezaji kutoka nchini humo lakini pia kuwabainishia maeneo mbali mbali katika sekta ya uchumi ambayo watu wa Korea kusini  wanaweza kuwekeza.

Alianza kwakuwashukuru sana kwakutambua urafiki wa nchi hizi mbili ambao umeanza miaka ya 1960’s, na kuwaambia  kuwa Mwanza ni mkoa ambao una fursa nyingi za uwekezaji katika Nyanja mbali mbali ikiwapo: Viwanda, Biashara, Kilimo, uvuvi,  Mifugo,  kwakutaja baadhi.

Mkuu huyo wa mkoa ameuwambia ujumbe huo wa  watu wa jamhuri ya Korea kusini, uliokuwa unaomngozwa na Bw. Son Yang Soo, kuwa Mwanza ndio sehemu pekeee katika nchi za eneo la  maziwa makuu inayo liunganisha soko la Afrika Mashariki kwa nchi za South Sudan, Rwanda, Burudi, Jamhuri ya Congo na hata Kenya na Uganda

Mkuu wa mkoa amesema kutoka na uchumi wa Mkoa wa Mwanza kufikia Tril. 8.45 kwa mwaka katika uzalishaji lakini pia Mwanza ndio mkoa unaochangia pato la Taifa ukishika nafasi ya pili ambapo mchango wake ni asilimia 9.4 katika pato la taifa ukitanguliwa na Dar es Salaam unaochangia kwa asilimia 17 kwa mwaka, hivyo kwa watu wanaotaka kuwekeza Mwanza wamewaza vyema kama jinsi ujumbe huu wa Korea Kusini ulivyo fanya.

Naye kiongozi wa msafara huo, Song Young Soo, alianza kwakuwapa Watanzania pole kufuatia tetemeko la Ardhi lililotokea tarehe 10, Septemba na kuathiri zaidi Mkoa wa Kagera na mara baada ya hapo, akasema wamefurahishwa na jitihada zinazo chukuliwa na mamlaka ya serikali katika kuahakikisha wawekezaji wanapata fursa yakuwekeza, Song amesema katika Nchi ya Korea Kusini uwekezaji umejikita katika nyanja za Teknolojia ya habari na mawasiliano, Afya na Viwanda kwa ujumla, aidha amesema kufuatia ziara iliyofanywa na mbunge wa Ilemela na Ujumbe wake mapema Mwaka huu, hiyo sasa imeibua chachu na muendelezo wa ushirikiano wanachi wan chi hizi mbili ambazo zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu sasa.

Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makaazi Dkt. Angeline Mabula (MB), amewataka wana watanzania na wana Mwanza  kwa ujumla wao , kuonesha utayari na kuwapokea wageni wanao kuja kwa nia njema yakuwekeza katika Mkoa wa Mwanza “ Niwa ombe tuu wananchi wa Tanzania, kuonesha utayari wakupokea wawekezaji, tunaimba viwanda, viwanda vikiwapo watakao ajiriwa ni watanzania wenye sifa husika, hivyo nilazima tunapopata wawekezaji tuwe na utayari na ukarimu kwa wageni wetu hasa  wawekezaji wema na kuwapa ushirikiano kwenye maeneo yetu,” alisema Mabula.

Ujumbe huo wa Korea Kusini ulikuwa ukiongozwa na Song Yaung Soo, wajumbe wengine ni Shing Jong Sam, Cho Yoop Gon, Kim Gi Geob, Doewak Kim, KTM Kyu il, wengine ni Rark in Nwan,  Kim Il Hyun, Kim Ji Mi, Lee Suk Hoom, Kim Chan Kyu, Byun Kyumg Ho, Lee Joom Hwa na Kim Lim Gon na Mkalimani wao aliyekuwa anaitwa Alex Gang.

Ujumbe huo wa Korea pamoja na mambo mengine utatembelea eneo la Nyamongholo kisha utapata fursa yakujionea Matayarisho ya Mpango Kamambe ya urasimishaji wa Makaazi ya Jiji la Mwanza na mpangilio wake.

Imeandaliwa na Afisa habari na Uhusiano Mwanza

 
Axact

Post A Comment: