Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo anatazamiwa kufanya ziara ya kikazi katika Wilaya za Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kuhimiza shughuli mbali mbali za maendeleo kwenye wilaya hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika moja ya Majukumu hapa alikuwa akitoa cheti.  
  
Kwa mujibu wa ratiba ambayo mtandao huu imeupata inaonesha kuwa, ziara hiyo ya kikazi itaanzia katika wilaya ya Sengerema siku ya tarehe 02.12.2013.

Katika ziara hiyo Mkuu huyo wa Mkoa atapata fursa ya kujionea shughuli mbali mbali za maendeleo zinazotekelezwa kwenye wilaya hizo, kukagua pamoja na kuhutubia wananchi kwenye mikutano ya hadhara.

Mkoa wa Mwanza unaundwa na Wilaya za Sengerema, Ukerewe, Ilemela, Nyamagana, Magu, Misungwi na Kwimba na kwa mujibu wa sensa ya watu ma makaazi ya mwaka 2012 mkoa huo unajumla ya wakaazi  2,772,509 , huku  shughuli kuu za uzalishaji mali ikiwa ni Kilimo, Madini, Mifugo Viwanda pamoja na Biashara.

Axact

Post A Comment: