Na:  Atley  Kuni.
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania hivi leo imeadhimisha miaka kumi toka kuanzishwa kwake kwa mafanikio makubwa.
Katibu Tawala Msaidizi kwenye Sekretariti ya Mkoa wa Mwanza Bw. Wambura Sabora alipokuwa akifungua
Kongamano la Miaka kumi ya TCRA waliokutana Mkoani Mwanza katika Ukumbi wa Victoria Pales wa Jiji Mwanza.

Hayo yamesemwa na Meneja wa TCRA kanda ya ziwa bw.Lawi Odiero wakatia akitoa maelezo mafupi ya juu ya nini kimtendeka tangu kuanzishwa kwa mamlaka ya mawasiliano nchini miaka kumi iliyopita.

Amesema katika kipindi cha miaka kumi ilyopita shughuli za mawasiliano zimekuwa kwa kasi kubwa sambamba na kukua kwa TEHAMA katika kilimo, miofugo,ufugaji, madini pamoja na biashara mbali mbali.
Amesema katika kipindi hicho cha miaka kumi vile vile kumekuwepo na ongezeko la vyombo vya habari, ambapo ndani ya Miaka kumi ya Mamlaka ya mawsiliano vyombo vya habari na TV vimeongezeka kwa kasi ikiwapo kutoka TV Moja hadi 27 na Redio kutoka 1 hadi 84 hivi sasa.
Amesema lengo la kuanzishwa kwa mamlaka hiyo ilikuwa na kusudio la utekelezaji wa Dhima ya taifa Tanzania Vission 2025, sera ya Taifa ya Teknolojia ya habari na mawasiliano ya mwaka 2003 na Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003.
 
Ameongeza kuwa mamalaka ya mawasiliano kwa hivi sasa inatekeleza wajibu wa  kusuluhisha migogoro kadha wa kadha kutoka kwa watumiaji kwa maana ya watumiaji wa huduma za mawasiliano, kutunga sharia za mawasiliani lakini pia kushirikiana na mamlaka nyingine kutoka nchi tofauti tofauti ulimwenguni.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye alikuwa mgeni rasmi na kuwakilishwa na Katibu Tawala Msaidizi wa Seksheni ya miundo mbinu bwana Wambura Sabora, amesema kuwa kila Mdau anatakiwa kuiga mfano wa TCRA ambao kwa namna moja au nyingine wameonesha mafanikio makubwa, alisema kutokana na kukuwa kwa teknlojia ya Mawasiliano nchini kumesaidia kukuza Teknolojia, ushindani wa soko umekuwa,uwekezaji umeongezeka lakini pia umeongeza uhuru wa mlaji kuchagua huduma gani aweze kutumia katika kujipatia huduma ya mwsiliano.
 
Sabora amesema pia kuwa kila Jambo linafaida na hasara lakini kwa hili la TCRA yeye kama mdau wa mawasiliano anasikia fahari kuona masuala ya mawsiliano yamekuwa ukilinganisha na miaka kumi au hata hamsini iliyopita, "hivyo ndugu zangu tusibeze jitihada na juhudi ambazo serikali imekwisha zifanya katika suala Zima la mawasiliano nchini" alisema na kuongeza kuwa kwa mada hizo ambazo zilikuwa zinawasilishwa ni vema wanasemina wakazingatia na kutilia maanani mafunzo hayo.
 
katika hatua nyingine takwimu zinaonesha kuwa kuanzia mwaka 2005 Mamlaka imeongeza idadi ya watoa huduma za leseni za mawasiliano imeongezeka kutoka wanne(4) hadi kufikia wanane(8) sawa na ongezeko la asilimia mia(100)., huku idadi ya watumiaji wa wavuti kwa hivi sasa ikifikia Milioni 7.5 na idadi hiyo inazidi kuongezeka siku hadi siku.
 

Kwa hivi sas mamlaka ya mawasiliano inatoa leseni za Miundombinu ya mawasiliano, Leseni za kutoa huduma za Mawasiliano, Leseni za kutoa huduma( Application Services Licence pamoja na Leseni za Utangazaji.
 
 
Eng. Lawi Odiero Meneja wa kanda ya Ziwa akiongea na vyombo vya habari.
 
 
 
Axact

Post A Comment: