·       Leo kujadili Taarifaya halmashauri ya Jiji kwa mara ya pili.

·       Jengo la Uwekezaji latengewa siku yake.
Na Atley Kuni- Mwanza.


Hapa Mheshimiwa Kigwangala Mwenyekiti wa Kamati akiwa amepanda yeye na Wabunge
wenzake, katika Tanki la Maji katika Kijiji cha kayenze.
Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na serikali za Mikoa(TAMISEMI), hapo jana ili endelea na ziara katika halmashauri ya jiji, huku ikianzaidi kwenye  miradi inayosimamiwa na halmashauri ya Jiji la Mwanza na baadae leo itakutana na kwa mara ya pili na watendaji wa Halmashauri hiyo wakingozwa na Mkurugenzi wao Halipha Hida na Wenyeviti kwa ajili ya kufanya marejeo ya taarifa mara baada yakutoa maelekezo ya kufanyia kazi.

Kwa mujibu wa habari ambazo mtandao huu imezipata, hapo jana Timu hiyo inayo ongozwa na Mhe. Kigwangala(MB) ilitembelea miradi ya Usambazaji wa maji katika Kijiji cha Kayenze, Ujenzi  wa kituo cha kukusanyia, kupozea na kuuza maziwa katika Kata ya Mkolani, kikundi ambacho kinamilikiwa na UWAMKO, miradi mingine iliyotembelewa hapo jana ni mradi wa kuongeza thamani ya mazao ya nafaka kwenye kata ya Buhongwa.

Ukaguzi wa bara bara.
 
Mtoa taarifa wetu ametueleza kwamba, miradi  mingine iliyotembelewa na wabunge hao ni matengenezo ya bara bara ya mawe Capripoint Nyakurunduma, barabara ya majengo mapya, Kiwanda cha bia Pasiansi

Tunaendelea na Ujenza

Lumala  kijiji cha kiloleli, vile vile  kama haitoshi na hali ya mshangao mkubwa , wabunge hao, waliomba kubadishiwa uelekeo baada ya kumaliza kukagua miradi waliyo pangiwa na wakaomba kwenda Shule ya Sekondari Mahina, ambapo kuna mradi wa ujenzi wa madarasa 3 yanayo tekelezwa na TASAF sambamba na kituo cha Afya makongoro ambacho kilijengwa baada ya kubomolewa kile kilicho kuwapo katika bara bara ya Airport.

Kwa mujibu wa ratiba yao wabunge hao hivi leo wanaendelea na Ziara yao hiyo, lakini hivi leo wakijikita zaidi katika kupokea Taarifa ambayo hapo juzi waliikataa na wakaomba ikafanyiwe marekebisho.

Katika hatua nyingine kamati hiyo itakutana siku ya kesho kujadili na kutathmini mgawanyo wa mali za Jiji na Ilemela, ambazo zimekuwa na kizungumkuti tangu kutenganishwa kwa Halmashauri hizo mbili.
Mkoa wa Mwanza wenye Halmshauri saba za Wilaya zinategemea kufikiwa na kamati hiyo, ambayo inashughulika zaidi na Mamlaka za mikoa pamoja na Halmashauri.
Zaidi ona katika picha ziara ilivyokuwa.
Axact

Post A Comment: