Na Julius Kithuure, Nairobi.

MAMBO YA UGATUZI KENYA.
Kadri serikali za kaunti za Kenya zinapokaribia adhimisho ya mwaka mmoja, raia wasema wamekutana na ucheleweshaji zaidi wa huduma kuliko faida kutokana na ugatuzi wa madaraka na mfumo mpya umeshindwa kufikia matarajio.

Francis Mokaya, ambaye anamiliki duka dogo katika kaunti ya Kisii na majengo matatu ya ghorofa ya makaazi katika mji wa Kisii, alisema alitarajia huduma mara tu gavana alipoapishwa kuingia katika kazi mwezi Machi uliopita.

"Nilitumaini kwamba hadi sasa majosho mengi yaliyoharibika yangekuwa yamekarabatiwa lakini kwa bahati mbaya, hakuna kilichotokea na inaonekana nitasubiri kwa muda mrefu," alisema Mokaya, ambaye pia anamiliki mifugo, kama zilivyo familia nyingi za vijijini." Sina jinsi nyingine zaidi ya kunyunyuzia dawa mifugo yangu nyumbani ambayo ni ghali na inatakiwa jitihada."

Majosho ya ng'ombe, ambayo ni ya kawaida katika maeneo ya vijijini, ni mashimo marefu ambapo mifugo wanatumbukia katika maji ambayo yana kemikali za kuua kupe na vimelea vingine.

Mokaya alisema serikali ya kaunti pia inazuia mapato yake ya kodi kwani haijawahi kutoa viwango vya kodi kwa huduma na umiliki wa mali, ambayo matokeo yake inazifanya zishindwe kutoza vizuri wapangaji wake.

Sijui ni kiasi gani ninapaswa kutoza kwani sijui tozo gani ambazo serikali ya kaunti [itanitoza] mimi," Mokaya alisema.

Kero ya Mokaya inawakabili wakaazi wengi nchini kote Kenya. Kaunti nyingi hazijajadili na kupitisha viwango vya mwisho vya kodi kama ilivyoelezwa katika miswada yao ya fedha ya 2013, ambayo imewapa mamlaka kusimamia kodi, tozo na adhabu kwa wasiolipa.

"Inachanganya, lakini nina matumaini kwamba wajumbe wa baraza la Kaunti watatoa kipaumbele katika kupitisha miswada hii ambayo imecheleweshwa baada ya [wajumbe wa baraza la kaunti] kugoma mwezi Novemba kudai kuongezewa mishahara ," alisema Charity Ngina, mwenye umri wa miaka 37, mfugaji wa kuku huko Nyandarua.

Ngina alisema ana matumaini ya kuongeza bei yake mara tu serikali ya Kaunti ya Nyandarua itakapoamua kiasi cha tozo anachopaswa kulipa kwa ugugaji wa ndege.

Kukosekana kwa mipango, uwekaji vipaumbele

Stephen Manoti, mbunge wa jimbo la Bobasi katika Kaunti ya Kisii, alisema maendeleo ya polepole katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika nchi nyingi hutokana na kukosekana kwa mipango mizuri na uwekaji wa vipaumbele.

"Magavana wengi na wajumbe wa mabaraza ya nchi hawana nyaraka za kutunga sheria au nakala kwa ajili ya matamko yao. Malengo yao yalikuwa kwanza kupata mamlaka, kisha mambo mengine yatafuata -- na hii ndiyo sababu wanapambana kuweka miradi yoyote ya maendeleo yenye mafanikio, lakini wanahitaji kulenga upya na kuweka mikakati," aliiambia Sabahi.

Damaris Wanja, mama wa watoto watatu mwenye umri wa maiaka 51 na mmiliki wa mgahawa huko Machakos, alisema hakuwa na furaha kutokana na kushindikana kwa maendeleo katika nchi yake.

"Gavana wangu, Dkt. Alfred Mutua, ameanzisha miradi ya mabilioni ya shilingi kujenga mji mpya wa Machakos kuanzia chini. Ninamkosoa kwa hili," alisema. "Je, tunahitaji jiji la kisasa wakati nchi haina maji ya kutosha [na] vituo vya afya vipo katika hali mbaya vikiwa na dawa muhimu chache? Hapana. Tunahitaji miradi ya umwagiliaji kusaidia upatikanaji wa kudumu wa vyakula na umeme vijijini kuwezesha vijana kuanzisha biashara ndogondogo."

Katika Kaunti ambazo kuna sera ya kodi, wananchi kama wajumbe wa baraza hawaachi kushauriana na jamii na kulumbana hadharani kuhusu sera kabla ya kutoa mamlaka ya kodi mpya.

Serikali ya Kaunti ya Kiambu imependekeza kuwatoza wakulima kodi ya shilingi 2,000 kwa kila eka ya ardhi wanayolima, kuleta upinzani kutoka kwa wakulima wadogo kama David Kariuki mwenye umri wa miaka 43.

"Kodi hizi na adhabu zinaanzisha vikwazo visivyo vya lazima kwa wafanyabiashara. Wanaadhibu na kuumiza uwekezaji," aliiambia Sabahi. "Je, wanasema kuwa ninapaswa kuacha na kutoilima ardhi yangu? Hii si kukatisha tamaa kufanya kazi kwa bidii na kualika njaa nchini?"

Kariuki alisema alitarajia serikali kuanza jitihada kama vile za kuwapa wakulima miche inayotoa mazao mengi, mbolea za msaada na upatikanaji wa kilimo cha kutumia zana rahisi za kilimo, badala ya kuanzisha "ushuru wa kuturejesha nyuma kwa ajili tu ya kukusanya fedha zaidi, ambazo hazimfaidishi mtu wa kawaida".

Kariuki aliliomba bunge la taifa na seneti kubana bajeti na kudhibiti matumizi katika kaunti 47 na kuanzisha kamati ya usimamizi kufuatilia matumizi ya kaunti ili "fursa za mabadiliko yaliyokusudiwa kwa ajili ya watu wa kawaida yasidharauliwe wala kupotea".

Serikali za mitaa zinapaswa kuanzia chini

Hata hivyo, magavana wa kaunti ambao walizungumza na Sabahi walipinga malalamiko hayo, wakisema kuanza taratibu ilikuwa ni kwa sababu ya urefu wa muda iliotumia kupokea rasilimali kutoka katika serikali ya taifa na kupanga miundo ya serikali za kaunti kwa mara ya kwanza.

Sasa ofisi hizo na wafanyakazi wake tayari wapo, magavana walisema wapo tayari kusongesha mbele huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo wananchi wamekuwa na wakiitarajia kwa shauku, kama vile ujenzi wa barabara, kukarabati shule, masoko na taasisi nyingine za serikali, uanzishaji wa mikopo isiyo na riba na misaada, maendeleo ya kilimo na programu za kuanzisha ajira.

Gavana wa Kaunti ya Meru Peter Munya aliiambia Sabahi anasikitika kwamba maendeleo yaliyotarajiwa bado hayajakamilika, lakini alizitetea serikali za mitaa, akisema zilipaswa kuimarisha utawala wake kuanzia chini.

"Ni kweli bado hatujatekeleza sera yoyote kuhusu kilimo, usafirishaji, leseni za biashara, usafi wa mazingira, elimu ya shule za awali na vituo vya afya, ambavyo ni mamlaka muhimu zinazoangukia katika serikali za kaunti," alisema.

Lakini sasa, kwa kuwa na mabaraza ya kaunti yanayofanya kazi, kupitisha bajeti za mwaka, wafanyakazi na fedha, watu wataanza kuona tofauti na mabadiliko waliyokuwa wakiyatarajia, alisema Munya.

"Kwa Hazina ya Taifa kutoa shilingi bilioni 20 (Dola milioni 233) katika serikali ya kaunti Alhamisi tarehe 16 [Januari], tupo tayari kuanza kutekeleza miradi kama ukarabati wa masoko, zahanati na barabara," alisema

 
Axact

Post A Comment: