.Ni katika Zahanati ya Nyanguge Iliyoko Mkoani Mwanza.
.Wilaya yajipanga kukamilisha Jengo la X- Ray ili Ahadi yao itimie kama alivyo ahidi Rais ya kupatiwa Mashine ya X Ray.
Hii ilikuwa siku ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete alipofika na kuzindua
Kisha kutoa ahadi ya X RAY pamija na Gari la Wagonjwa katika Wilaya ya Magu, kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt Athumani Pembe, Mkurugenzi wa Halmashauri Bibi Naomi Nnko, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tz. Dkt. Jakaya Kikwete, Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa Kitongosima Mhe Desdetery Kiswaga, pamoja Mbunge wa Jimbo la Magu Dkt. Festus Limbu  ( Picha zote na Afisa Habari Mkoa wa Mwanza).



Natazama kama Limekua Likiwa kamili na Gesi yake.
.
Hapa Mkuu wa Mkoa akiwasha Gari mara baada ya Uzinduzi wa gari la Wagonjwa.


Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu hapa akisoma Taarifa wakati wa kukabidhi Gari la Zahanati hiyo.
ya Lugeye, lililo tolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Kibao kilichowekwa wakati wa Uzinduzi wa Zahanati hiyo.


Hapa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akikagua Vifaa vya Ambulence.
Hili ndilo Gari lililotolewa kama Ahadi ya Mheshimiwa Rais aliyo itoa Mwishoni mwa Mwaka jana.
.


Na: Atley Kuni - Afisa Habari Mkoa wa Mwanza.

Nderemo shangwe hoi hoi na Vifijo vilitawala katika Zahanati ya Nyanguge wakati Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evaristi Ndikilo alipokuwa akikabidhi gari la Wagojwa aina ya Land Cruser iliyo ahidiwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania wakati alipofanya ziara katika Mkoa wa Mwanza Mwishoni mwa mwaka jana tarehe 07. Septemba 2013 na kufungua Zahanati ya Nyanguge na kasha kuwa ahidi mashine ya X ray pamoja na Gari la wagonjwa.
 
 
Alipokuwa akifungua zahanati hiyo rais alisema " Nimefurahishwa sana na kazi mnayo ifanya hapa Lugeye, kwa hiyo na Mimi  Rais wenu, nitashiriki nayi kwa kuwa changia kile kidogo nilicho ncho" alisema rais, na kuongeza "kwa kuanzia nita waletea gari la wagojwa lakini kama hiyo haitoshi, mkiweza kukamilisha jingo la X Ray basi mimi mchango wangu utaongezeka na kuwaletea Mashine ya X- Ray hapa Lugeye".
 
Kwamujibu wa taarifa ambazo kuni newsblog imezipata tayari Gari la wagonjwa limepatikana na tarehe 24.1.2014 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo alifika katika Kata ya Kitongosima Wilayani Magu kwa ajili ya kuikabidhi gari hilo  lenye namba za usajili STL 938  akiwa katika Ziara ya kukagua shughuli mbali mbali za Maendeleo Mkaoni humo.
 
Aidha katika hatua nyingine wananchi hao hivi sas wanaendelea na Ujenzi wa jingo la X ray, ambapo hadi siku kuninews ilipo tembelea katika mradi huo tayari, msingi ulikuwa umeanza kujengwa, Matofali zaidi ya Elfu nne yalikuwa yamesha Fyatuliwa, huku wananchi wakiwa wamesomba Tripu 10 za Mchanga zenye thamani ya Tsh. 900,000, nayo halmashauri ya Wilaya ya Magu tayari imechangia kiasi cha Mil. 10,000,000, huku ikiwa imetenga kiasi cha sh. Mil. 60,000,000 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo ili waweze kupatiwa X ray waliyo ahidiwa na Mheshimiwa Rais.
 
Kwa upande wao wananchi katika Eneo hilo hawa kuficha furaha yao kwa kusema "kama ni hivi hakika ndio maana huyu ni mtu wa watu, ameahidi Samaki kweli kaleta samaki"
 
Naye Mganga mkuu wa Wilaya ya Magu, akisoma taarifa mbele ya Mkuu wa Mkoa alisema, kupatikana kwa gari hilo kutasaidia kupunguza vifo vya mama na mototo kwani itasaidia kuwafikia wananchi kwa haraka na kisha kuwapeleka katika Zahanati kwa ajili yakupata huduma iliyo bora".
 
Akikabidhi gari hilo kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, amewatasa wananchi hao kulitunza gari hilo, ili liweze kuwa msaada kwa watu wote bila kujali Itikadi zao za Kisiasa, " Kwa hiyo ndigu zangu mimi rai yangu kwenu ni kwamba, Gari hili sasa liwe linapatika kituoni muda wote na isitokee sasa mtu akaanza kulifanyia shughuli zake Binafsi, alisema na kuongeza, lakini pia hakikisheni linafanyiwa matengenezo kwa wakati. sio gari limesha fikisha kilometa za Service ninyi mnaendele kulitumia hapana" samba mba na hilo akawashi kuwa wanaliwekea mafuta mara kwa mara ili pindi linapo hitajika liwe tayari.
 
Mwisho aliuagiza uongozi wa Wilaya ya Magu kuhakikisha bara bara ziendazo Vijijini zina imarishwa ili kufanya gari hili liweze kudumu kwa muda mrefu, " Nimuombe ndugu yangu mkurugenzi aone sasa umuhimu wa kuzifanyia ukarabati bara bara mara kwa mara.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya magu, ameithibitishia kuninews.blogspot.com kwamba kutokana na ahadi ya Rais wanategemea kukamilisha Jengo la X ray ifikapo mwishini mwa Februari 2014.
Wilaya ya magu yenye wakaazi 299,759 inavituo vya kutolea huduma za Afya 46 ambavyo ni Hospitali moja Zahanati za Serikali 30, vya watu binafsi 11 na vituo vya afya 4.
 
 Mkuu wa Mkoa wa mwanza alikuwa katika ziara ya kikazi Wilayani humo ikiwa ni sehemu ya kukagua shughuli za maendeleo, kuzungumza na wana nchi pamoja na kusikiliza kero zao.
 

Axact

Post A Comment: