Kamati za Bunge zinazo shughulikia masuala ya Nishati pamoja na Serikali za Mitaa, zinategemewa kukutana na uongozi wa mkoa wa Mwanza hivi leo.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo kuninewsblog imezipata, imesema lengo kuu la kukutana na uongozi wa Mkoa wa Mwanza ni pamoja na kukagua shughuli mbali mbali za maendeleo zinazo tekelezwa mkoani hapa.

Habari zimesema kwamba, kamati hizo zitafika nyakati za asubuhi na kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza na baadhi ya watendaji katika sekretarieti ya mkoa wa mwanza na badae watakwenda halmashauri ya Jiji kabla ya kwenda kukagua Miradi ya Maendeleo.

Miradi inayotazamiwa kutembelewa ni pamoja na Ujenzi wa bara bara za mradi wa TSCP ambao ni watekelezaji wa ujenzi wa bara bara za lami katika jiji la Mwanza na majiji mengine matano ya Tanzania.

Endelea kufatilia kuninews kwa habari hizi na zingine...
Axact

Post A Comment: