Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amekutana na viongozi wa dini pamoja watendaji wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza kwa ajili yakuzungumzia suala la maendeleo ya Mkoa huo na wa kwanza kukutana nao walikuwa watendaji wa Sekretarieti Mkoa na badaye jioni viongozi wa dini.
 
·        Awapa rungu watendaji, awaambia wasifanye kazi kwa mazoea.

·        Viongozi wa Dini wakerwa na Uchawi, Ukame, na hali duni katika zao la Pamba.

·        “Vijana wengi wana ndoto za kuhamia  Mwanza kuwa Machinga”- Askofu AIC asema.
 

 

SHEKHE HASSAN FEREJI WA MKOA WA MWANZA AKICHANGIA JAMBO KATIKA KIKAO KILICHO WAKUTANISHA VIONGOZI WA DINI NA MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO.
MKUU WA MKOA WA MWANZA MAGESA MULONGO AKIFUNGUA KIKAO NA VIONGOZI WA DINI MKOANI HAPA.

VIONGOZI WA DINI WAKIFURAHIA JAMBO, ANAYE PIGA MAKOFI NI KIONGOZI WA KANISA LA SDA, AITWAE BULENGELA. KUTOKA DAYOSISI YA NYANZA


ASKOFU ANDREW GULLE WA KKKT DAYOSISI YA MASHARIKI YA ZIWA VIKTORIA AKICHANGIA MADA KATIKA KIKAO HICHO.

KATIBU TAWALA MKOA WA MWANZA ALIYE SIMAMA FAISAL ISSA AKIWA ANATOA MUONGOZO JUU YAKUCHANGIA KATIKA KIKAO HICHO.








KIKAO NA WATENDAJI WA RS MWANZA.

Katika kile kinachoonekana nikuendeleza  harakati za kuwakumbusha majukumu yao na kuwahimiza kuacha kufanya kazi kwa mazoea, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo amekutana na watendaji wa Menejimenti na kuwaagiza kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wabadilike na kutoa matokeo chanya kwa umma wa wana Mwanza.
Mulongo alikuwa akizungumza katika kikao cha ndani kilicho wakutanisha wakuu wa seksheni na vitengo wa sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza kwa ajili yakuwaweka sawa watendaji hao, amesema haipendezi Mwananchi asikie tu kwamba kuna suala la Mkongo wa taifa lakini kiutendaji au kimatokeo Mwananchi huyo unakuta hajui hata maana ya mkongo wa taifa “ Ndugu zangu tunafanya vitu vingi vizuri lakini vitu hivyo hatuvitafsiri kwa Wananchi kwa maisha yao ya kila siku alisema Mulongo na kuongeza kuwa “nilazima tuende kwa malengo ili kuweza kufikia malengo tuliojiwekea”.
Mulongo amesema kwa mfano, hata suala la score card bado ni msamiati mgumu kwa mwananchi wa kawaida kwakuwa hajui ni kwa namna gani unafanyakazi lakini pia namna unavyoweza kumsaidia.
Mulongo amekwenda mbali zaidi na kusema kazi kubwa aliyo nayo Katibu Tawala wa Mkoa pamoja na wataalam wa sekretarieti ni kuhakikisha yanapatikana maendeleo kwakusimamia ipasavyo na kuelekeza Halmashauri za Wilaya nini wanapaswa kufanya katika kuwaletea maendeleo Wananchi.
Huku akisema kutokana na kutosimamiwa ipasavyo ndio maana Mkoa wa Mwanza na Halmashauri zake katika kipindi cha 2010/2011 na kipindi/2012/2013 zilipata hati za mashaka jambo ambalo linatia shaka juu ya usimamizi wa halmashauri hizo” Utaona katika kipindi cha 2010/2011 sawa mlipata hati safi lakini katika kipindi cha 2011/2012 mkapata hati safi zenye msisitizo na 2012/2013 mkapata hati ya mashaka ni dhahiri kwamba kuna mahali mlipo lega”.
Mbali ya masuala ya hati chafu Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwa Mkoa wa Mwanza vyanzo vya mapato vipo vingi lakini havijaunganishwa vizuri huku akitolea mfano waendesha Boda boda ambao amesema robo tatu ya waendesha boda boda hawalipi kodi kwasababu yakutokuwepo kwa mfumo rasmi wakuwatoza “Our source collection they are not formalize hence ¾ of revenue collection lost, eg. Machinga and Boda boda” alisema Mulongo.
Sekta nyingine alizo zigusia Mkuu huyo wa Mkoa ni pamoja na uwekezaji hasa kwenye maeneo ya ardhi ambayo haijatendewa haki ipasavyo ambapo amesema hata kama ardhi ya Mwanza ni ndogo lakini kama itawekezwa ipasavyo itasaidia Wananchi kuondokana na umaskini “ kila mtu afanye kazi yake kiufasaha ili kuweza kumuokoa Mwananchi wa Mkoa huu” alisema Mulongo. “ Mimi kama RC jeuri yangu ipo kwenu ninyi hivyo mfanye mfanyavyo ninyi pamoja na RAS kuhakikisha tunasonga mbele.

MKUTANO NA VIONGOZI WA DINI

Mkoa, mbali yakukutana na Wakuu hao wa seksheni vile vile jioni hii amekutana na Viongozi wa Madhehebu ya dini Mkoani hapa kwa ajili yakufahamiana lakini pia kujua ni kwa namna gani wote kwa pamoja watasaidia katika kusukuma gurudumu la mandeleo. “ Jamani mimi leo nimewaiteni lakini sina ajenda kubwa ambayo ninyi hamuijui, suala hapa ni maendeleo ninyi kama viongozi wa kiroho ndio wenye watu, sasa tufanyeje ili tuweze kwenda mbele na kuinua Mkoa wetu? Naomba kila mmoja wetu atapata nafasi yakuchangia”.
Wakitoa mawazo yao, viongozi dini  walisema pamoja na ushirikiano, yapo mengi yakufanya lakini kwakuwa haiwezekani yote yakafanyika kwa siku moja ni vema kuanza na machache na kadri muda utakavyokuwa unasogea ndivyo watakuwa wanashauriana, ambapo Askofu Andrew Gulle wa KKKT Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria, alikuwa wa kwanza kusema na kumshauri Mkuu huyo wa Mkoa kudumisha umoja uliokuwepo wakati wa uongozi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa aliyepita Mhandisi Evarist Ndikilo.” Mhe. Mkuu wa Mkoa mimi ninalo moja nalo ni kuwa kupitia ule umoja wetu ambao tuna viongozi 20 kutoka pande zote mbili za dini zetu hizi sisi tutakupa ushirikiano wakutosha”.
Katika kikao hicho, viongozi hao wa dini wamemshauri Mkuu wa Mkoa kurudisha heshma ya zao la pamba katika Mkoa huo kwakuwa, zao hilo ndilo lilikuwa mkombozi wa watu wa kanda ya Ziwa ukiwapo Mkoa wa Mwanza “Mkuu wa mkoa hivi sasa kuna shida kubwa sana ya ajira na vijana wote wanawaza kukimbilia Mwanza au Dar es salaam, huku wakiwaza kuwa ndio kuna maisha bora kwakuwa huko vijijini hakuna kazi” alisema mmoja ya maaskofu wa AICT.
Kwa upande mwingine viongozi hao wamemuasa Mkuu wa Mkoa kukomesha suala la milio ya mabomu, kushirikina, ulevi, uharibifu wa mazingira wa kupindukia ambavyo imekuwa kero kubwa kwa Mkoa huo “Mkuu wa mkoa sula la mazingira bado nalo ni shida, hivi sasa chakula kwa Mkoa huu tunategemea Wilaya ya Sengerema pekee, tofauti na miaka ya nyuma” walisema viongozi hao wa dini
Naye Askofu Sekelwa, akichangia katika kikao hicho aliamua kutoa kilio kwa  watendaji wa Halmashauri ya Jiji na kusema “ Suala la Bilioni 40 katika Jiji la Mwanza ambazo zinatajwa zimefisadiwa,  limefanya hata watu washindwe kuelewa endapo kuna viongozi waliopewa dhamana yakuwasimamia watu, alisema Sekelwa na kuongeza tunakuomba mkuu wa mkoa suala hilo ulichukue na ulifanyie kazi, haingii akilini mamlaka zipo halafu fedha kiasi kiukubwa kiasi hicho zinapotea kienyeji, kweli ni suala lisilo leta afya mbele ya jamii” alisisitiza askofu huyo
Mkoa wa mwanza ambao unatajwa kuwa moja ya mikoa inayo changia kwa kiasi kikubwa katika pato la Taifa, bado umekumbwa na changamoto kubwa ya ukusanyaji mapato na hivyo kumfanya mkuu wa mkoa kuwa na mikutano na makundi mbali mbali katika mkoa huo, aidha hivi karibuni anakusudia kukutana na wakuu wa Taasisi zilizopo mkoani hapa kwa ajili yakuzungumza nao kuona ni kwa jinsi gani wanaweza kukuza uchumi wa mkoa huu.
Axact

Post A Comment: